Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb20 Mwezi wa 8 uku. 3
  • Musimame Imara kwa Sababu Mwisho Unakaribia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Musimame Imara kwa Sababu Mwisho Unakaribia
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuonyeshe Sifa Zenye Kumupendeza Mungu—Ujasiri
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Kuwa Hodari Haiko Nguvu Sana
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
  • ‘Ukuwe Hodari . . . na Utende’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Unipatie Uhodari
    ‘Tumuimbie Yehova kwa Furaha’
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
mwb20 Mwezi wa 8 uku. 3

MAISHA YA MUKRISTO

Musimame Imara kwa Sababu Mwisho Unakaribia

JUU YA NINI NI JAMBO LA MAANA: Hivi karibuni kutakuwa matukio yenye kuogopesha yenye itatuomba tuonyeshe uhodari na kumutegemea kabisa Yehova kuliko zamani. Taabu kubwa itaanza wakati dini ya uongo itaharibiwa. (Mt 24:21; Ufu 17:16, 17) Ile wakati, pengine tutatangaza habari kali ya hukumu. (Ufu 16:21) Gogu wa Magogu atatushambulia. (Eze 38:10-12, 14-16) Ili kupigania watu wake, Yehova ataleta “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufu 16:14, 16) Tunapaswa kuwa waaminifu leo wakati tunajaribiwa; ile njo itafanya tukuwe na uhodari kabisa wakati ile matukio yenye kuogopesha itakuja.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Ujikaze kuishi kulingana na kanuni za Yehova.​—Isa 5:20

  • Endelea kumuabudu Yehova pamoja na Wakristo wenzako.​—Ebr 10:24, 25

  • Ukuwe tayari kutii muongozo wenye tengenezo la Yehova linatoa.​—Ebr 13:17

  • Ufikiri sana juu ya namna Yehova aliokoa watu wake wakati wa zamani.​—2Pe 2:9

  • Usali kwa Yehova na umutegemee.​—Zb 112:7, 8

MUANGALIE VIDEO MATUKIO YA WAKATI WENYE KUJA YENYE YATAOMBA UHODARI​—SEHEMU, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Matukio ya Wakati Wenye Kuja Yenye Yataomba Uhodari.’ Ku Jumba la Ufalme, kisha kusoma juu ya kutaniko lenye ametumwa ndani, dada mumoja anahangaika na iko anaangalia mbele.

    Juu ya nini ilikuwa nguvu kwa wahubiri kutii wakati walitumwa mu makutaniko tofauti?

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Matukio ya Wakati Wenye Kuja Yenye Yataomba Uhodari.’Uleule dada iko nazungumuza na dada wengine wawili juu ya kutaniko kwenye wanatumwa.

    Namna gani kutii kunatusaidia tukomalishe sifa ya uhodari?

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Matukio ya Wakati Wenye Kuja Yenye Yataomba Uhodari.’ Kijana mwanaume anaogopa kisha kufikiri sana juu mambo yenye aliona kuhusu Armagedoni mu kitabu ‘Ufalme wa Mungu Unatawala!’

    Juu ya nini tutakuwa na lazima ya uhodari wakati Armagedoni itafika?

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Matukio ya Wakati Wenye Kuja Yenye Yataomba Uhodari.’ Yehoshafati na watu wengine wa Yuda wanafika ku uwanja wa vita na wanakuta maadui wao wote wamekufa.

    Hii njo wakati wa kujitayarisha kwa ajili ya matukio ya wakati wenye kuja yenye itaomba uonyeshe uhodari

    Ni habari gani yenye kuwa mu Biblia yenye inaweza kutusaidia tukuwe hakika kama Yehova atatuokoa?​—2Ny 20:1-24

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine