MAISHA YA MUKRISTO
Musimame Imara kwa Sababu Mwisho Unakaribia
JUU YA NINI NI JAMBO LA MAANA: Hivi karibuni kutakuwa matukio yenye kuogopesha yenye itatuomba tuonyeshe uhodari na kumutegemea kabisa Yehova kuliko zamani. Taabu kubwa itaanza wakati dini ya uongo itaharibiwa. (Mt 24:21; Ufu 17:16, 17) Ile wakati, pengine tutatangaza habari kali ya hukumu. (Ufu 16:21) Gogu wa Magogu atatushambulia. (Eze 38:10-12, 14-16) Ili kupigania watu wake, Yehova ataleta “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufu 16:14, 16) Tunapaswa kuwa waaminifu leo wakati tunajaribiwa; ile njo itafanya tukuwe na uhodari kabisa wakati ile matukio yenye kuogopesha itakuja.
NAMNA YA KUFANYA VILE:
Ujikaze kuishi kulingana na kanuni za Yehova.—Isa 5:20
Endelea kumuabudu Yehova pamoja na Wakristo wenzako.—Ebr 10:24, 25
Ukuwe tayari kutii muongozo wenye tengenezo la Yehova linatoa.—Ebr 13:17
Ufikiri sana juu ya namna Yehova aliokoa watu wake wakati wa zamani.—2Pe 2:9
Usali kwa Yehova na umutegemee.—Zb 112:7, 8
MUANGALIE VIDEO MATUKIO YA WAKATI WENYE KUJA YENYE YATAOMBA UHODARI—SEHEMU, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Juu ya nini ilikuwa nguvu kwa wahubiri kutii wakati walitumwa mu makutaniko tofauti?
Namna gani kutii kunatusaidia tukomalishe sifa ya uhodari?
Juu ya nini tutakuwa na lazima ya uhodari wakati Armagedoni itafika?
Hii njo wakati wa kujitayarisha kwa ajili ya matukio ya wakati wenye kuja yenye itaomba uonyeshe uhodari
Ni habari gani yenye kuwa mu Biblia yenye inaweza kutusaidia tukuwe hakika kama Yehova atatuokoa?—2Ny 20:1-24