Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb20 Mwezi wa 9 uku. 3
  • Fanya Angalisho ili Usieneze Habari za Uongo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Fanya Angalisho ili Usieneze Habari za Uongo
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Mutu Asiye na Uzoefu Anaamini Kila Neno’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Unajua Ukweli wa Mambo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Matumizi ya Internet—Fanyeni angalisho kwa hatari!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Intaneti Kutumia kwa Hekima Kifaa cha Ulimwenguni Pote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
mwb20 Mwezi wa 9 uku. 3

MAISHA YA MUKRISTO

Fanya Angalisho ili Usieneze Habari za Uongo

Mwanamuke mwenye kuuza vitu iko anashangaa mambo yenye anaona mu telefone yake.

Leo, watu wengi wanaweza kupata habari haraka sana kupitia magazeti, radio, televizyo, na Enternete. Lakini watu wenye wanamuabudu “Mungu wa ukweli” wanaepuka kabisa kueneza habari za uongo. (Zb 31:5; Kut 23:1) Habari za uongo zenye mutu anaeneza zinaweza kuwaumiza sana wengine. Ukipenda kujua kama habari fulani ni ya kweli, ujiulize hivi:

  • ‘Mwenye aliniambia ile habari ni mutu mwenye kutumainika?’ Pengine mutu mwenye kueleza habari hajue mambo yote. Kama habari inatoka kwa mutu moja kisha inaenda kwa mutu mwingine, mara mingi inabadilikaka. Kwa hiyo, ukuwe muangalifu sana kama haujue vile ile habari ilianza. Wale wenye kuwa na mapendeleo hawapaswe kuzungumuzia habari yenye haijulikane kama ni ya kweli; kwa sababu ndugu na dada wanawatumainiaka sana na kuwaza kama mambo yote yenye watasema ni ya kweli

  • ‘Ile habari ni ya kusingizia tu mutu?’ Kama ile habari ni ya kuharibisha tu sifa ya mutu ao ya watu fulani, haiko muzuri kuielezea wengine.​—Mez 18:8; Flp 4:8

  • ‘Ni habari ya kweli kabisa?’ Ukuwe muangalifu na utulie kwanza kama unasikia habari yenye inakushitua sana

MUANGALIE VIDEO NAMNA GANI NAWEZA KUACHA KUSEMA WENGINE MUBAYA? KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Kijana mwanaume iko ndani ya kitu fulani cha muviringo na pembeni ya kile kitu kuko visu vyenye kuchomekwa kila upande.

    Kulingana na Mezali 12:18, mambo yenye mutu anasema inaweza kuwa na matokeo gani?

  • Kikundi ya watu wenye wako wanasema mambo ya mubaya juu ya wengine.

    Namna gani Wafilipi 2:4 inaweza kutusaidia tuchunguze kwa hekima mambo yenye tuko tunasema juu ya wengine?

  • Mwanaume fulani anakataa kusikia mambo ya mubaya yenye mutu fulani iko anasema juu ya wengine.

    Tunaweza kufanya nini kama watu wanaanza kusema mubaya juu ya wengine?

  • Mwanaume fulani iko anasema mubaya juu ya watu wengine na pembeni yake kuko mwanaume mwenye kuvala kama journaliste mwenye kuandika mambo yenye ule mwanaume iko anasema.

    Tunapaswa kujiuliza maulizo gani mbele ya kuanza kuzungumuza juu ya wengine?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine