MAISHA YA MUKRISTO
Fanya Angalisho ili Usieneze Habari za Uongo
Leo, watu wengi wanaweza kupata habari haraka sana kupitia magazeti, radio, televizyo, na Enternete. Lakini watu wenye wanamuabudu “Mungu wa ukweli” wanaepuka kabisa kueneza habari za uongo. (Zb 31:5; Kut 23:1) Habari za uongo zenye mutu anaeneza zinaweza kuwaumiza sana wengine. Ukipenda kujua kama habari fulani ni ya kweli, ujiulize hivi:
‘Mwenye aliniambia ile habari ni mutu mwenye kutumainika?’ Pengine mutu mwenye kueleza habari hajue mambo yote. Kama habari inatoka kwa mutu moja kisha inaenda kwa mutu mwingine, mara mingi inabadilikaka. Kwa hiyo, ukuwe muangalifu sana kama haujue vile ile habari ilianza. Wale wenye kuwa na mapendeleo hawapaswe kuzungumuzia habari yenye haijulikane kama ni ya kweli; kwa sababu ndugu na dada wanawatumainiaka sana na kuwaza kama mambo yote yenye watasema ni ya kweli
‘Ile habari ni ya kusingizia tu mutu?’ Kama ile habari ni ya kuharibisha tu sifa ya mutu ao ya watu fulani, haiko muzuri kuielezea wengine.—Mez 18:8; Flp 4:8
‘Ni habari ya kweli kabisa?’ Ukuwe muangalifu na utulie kwanza kama unasikia habari yenye inakushitua sana
MUANGALIE VIDEO NAMNA GANI NAWEZA KUACHA KUSEMA WENGINE MUBAYA? KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Kulingana na Mezali 12:18, mambo yenye mutu anasema inaweza kuwa na matokeo gani?
Namna gani Wafilipi 2:4 inaweza kutusaidia tuchunguze kwa hekima mambo yenye tuko tunasema juu ya wengine?
Tunaweza kufanya nini kama watu wanaanza kusema mubaya juu ya wengine?
Tunapaswa kujiuliza maulizo gani mbele ya kuanza kuzungumuza juu ya wengine?