Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/99 uku. 3
  • Matumizi ya Internet—Fanyeni angalisho kwa hatari!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Matumizi ya Internet—Fanyeni angalisho kwa hatari!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Intaneti Kutumia kwa Hekima Kifaa cha Ulimwenguni Pote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari Njema Kwenye Internet
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kisanduku Cha Maulizo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Epuka Ufuatiaji wa ‘Mambo Yasiyo na Maana’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 11/99 uku. 3

Matumizi ya Internet—Fanyeni angalisho kwa hatari!

1 Watu wa Yehova hufurahia ushirika pamoja wenye kujenga. Wanafurahia kushiriki mambo yaliyoonwa kutoka katika huduma ya shambani na wanathamini kusikia matukio yanayopata Mashahidi wa Yehova na kazi ya Ufalme ulimwenguni pote. Wao hupenda kujulishwa jambo lolote lenye kutokeza ambalo laweza kupata ndugu zetu, kama vile hali mbaya au msiba wa kiasili, na wao hutaka kujua ikiwa kuna jambo fulani wanaloweza kufanya ili kusaidia. Kupendezwa na wengine kama huko huonyesha umoja wa udugu, kukihakikisha kwamba kwa kweli sisi tunapendana.​​—Yn. 13:​34, 35.

2 Leo, tunasikia kuhusu matukio ya ulimwengu kwa haraka. Redio na televisheni hupeleka moja kwa moja habari kuhusu mambo madogo-madogo ya matukio kwa vikundi vya wasikilizaji kuzunguka dunia nzima. Simu pia inafanya iwezekane kupashana habari mara moja na watu ulimwenguni pote. Tukio la karibuni katika upashanaji-habari ambalo ni lenye kuenea sana ni Internet (mfumo wa kupashana habari kupitia kompyuta).​​—Ona Amkeni!, Julai 22, 1997.

3 Uvumbuzi wa simu ulifungua njia kwa upashanaji-habari wa haraka kati ya watu ulimwenguni pote. Ingawa simu ni yenye mafaa sana, uangalifu unahitajiwa kuhusiana na jinsi hiyo inavyotumiwa, kwa kuwa hiyo inaweza kuwa kifaa kwa ajili ya ushirika na utendaji usiofaa, na kutumia simu kupita kiasi kunaweza kugharimu fedha nyingi. Televisheni na redio hutoa uwezekano kuhusiana na elimu. Walakini, kwa kusikitisha, mambo mengi yanayotiwa katika programu hizo ni yenye ufisadi kiadili, na kuitolea uangalifu ni kupoteza wakati. Hekima inatuomba tuwe wenye uchaguzi katika kutumia televisheni na redio.

4 Internet inawezesha mtu kupashana habari na mamilioni ya wengine ulimwenguni pote bila kugharimu fedha nyingi, na inafungua mlango kwa kiasi kikubwa cha habari. (Amkeni!, Januari 8, 1998) Hata hivyo, matumizi ya ovyoovyo ya Internet yanaweza kuweka mtu mbele ya hatari kubwa za kiroho na za kiadili. Namna gani hivyo?

5 Wengi hupendezwa na habari inayopatikana kwa urahisi ambayo huonyesha jinsi ya kutengeneza silaha, kutia ndani mabomu. Mashirika ya kazi yanalalamika kuhusu kiasi cha wakati ambacho wafanyakazi hupoteza kwa kutumia Internet. Mengi yamesemwa katika vichapo vyetu kuhusu hatari za kiroho zilizo wazi ambazo hupatikana kwenye Internet. Vituo vingi vya Web huonyesha mambo ya jeuri na pornografia ambayo haifai hata kidogo kwa Wakristo. (Zab. 119:37) Zaidi ya hatari hizo, kuna hatari yenye kudhuru zaidi kwa siri ambayo Mashahidi wa Yehova kipekee wanapaswa kujilinda wasipatwe nayo. Hatari hiyo ni nini?

6 Je! unaweza kualika mtu usiyemjua katika nyumba yako bila kujua kwanza yeye ni nani? Namna gani ikiwa hakuna namna ya kujua? Je! utaruhusu mtu kama huyo usiyemjua abaki peke yake pamoja na watoto wako? Huo ni uwezekano usiotiliwa shaka kuhusu Internet.

7 Barua za kielektroniki zinaweza kutumwa na kupokewa kutoka kwa watu usiowajua. Ni vivyo hivyo wakati unapoongea mahali pa kupigia gumzo (mazungumzo) kwenye Internet. Wale wanaoshiriki katika mazungumzo hayo wanaweza nyakati nyingine kujidai kuwa Mashahidi wa Yehova, lakini mara nyingi wao si Mashahidi. Mtu fulani anaweza kujidai kuwa kijana, japo hiyo yeye si kijana. Au mtu fulani anaweza kwa uwongo kujidai kuwa wa jinsia fulani.

8 Habari inayopitishwa kwako inaweza kuja kama vile mambo yaliyoonwa au maelezo kuhusu imani zetu. Habari hiyo inapitishwa kwa wengine ambao, kwa upande wao, huipitisha pia kwa watu wengine. Kwa kawaida, habari hiyo haiwezi kuhakikishwa, na inaweza kuwa ya uwongo. Maelezo hayo yanaweza kuwa kificho kwa ajili ya kueneza mawazo ya waasi-imani.​​—2 Thes. 2:​1-3.

9 Kwa kuwa na hatari hiyo akilini, ikiwa unatumia Internet, jiulize: ‘Ninaitumia kwa kusudi gani? Je! inawezekana jinsi ninavyoitumia iniletee madhara ya kiroho? Je! ninaweza kuwa mwenye kuchangia katika kuumiza wengine kiroho?’

10 Vituo vya Web vya “Mashahidi wa Yehova”: Fikiria, kwa mfano, vituo fulani vya Internet vinavyofanywa na watu wanaojidai kuwa Mashahidi wa Yehova. Wanakualika utembelee vituo vyao ili kusoma mambo yaliyoonwa ambayo yaliwekwa na wengine wanaojidai kuwa Mashahidi. Unatiwa moyo kushiriki mawazo na maoni yako kuhusu vichapo vya Sosaiti. Wengine hupendekeza utoaji mbalimbali ambao ungeweza kutumiwa katika huduma ya shambani. Vituo hivyo hutoa mahali pa kupigia gumzo ambapo kwa hapo watu wanaweza kujiunganisha, wakifanya upashanaji-habari wa moja kwa moja na wengine uwezekane, kama ilivyo kwenye simu. Wao mara nyingi huonyesha vituo vingine ambavyo kwenye hivyo unaweza kushirikiana na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote kupitia kompyuta. Lakini, je! unaweza kuhakikisha kwamba njia hizo za kupashana habari hazikuwekwa na waasi-imani?

11 Kuwa na ushirika kupitia Internet kunaweza kuwa kusikopatana na pendekezo linalopatikana kwenye Waefeso 5:​15-​17. Mtume Paulo aliandika: “Fulizeni kuangalia sana kwamba jinsi mnavyotembea si kama wasio na hekima bali kama watu wenye hekima, mkijinunulia kabisa wakati unaofaa, kwa sababu siku ni za uovu. Kwa ajili ya hili acheni kuwa wenye kukosa akili, bali endeleeni kufahamu mapenzi ya Yehova ni nini.”

12 Kutaniko la Kikristo ndiyo njia ya kitheokrasi ambayo kupitia hiyo tunalishwa kiroho na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:​45-​47) Ndani ya tengenezo la Mungu, tunapata mwongozo na ulinzi ili kutufanya tuendelee kuwa si sehemu ya ulimwengu, na pia kichocheo ili kubaki wenye shughuli katika kazi ya Bwana. (1 Kor. 15:58) Mtunga-zaburi alionyesha kwamba alipata furaha na alijisikia mwenye usalama kati ya watu wa Mungu waliokutanika. (Zab. 27:​4, 5; 55:14; 122:1) Kutaniko linatoa pia utegemezo wa kiroho na msaada kwa ajili ya wale walio na ushirika nalo. Humo, unaweza kupata kikundi cha marafiki wenye upendo, wenye kuhangaikia wengine, na wenye kujali​—watu unaowajua binafsi ambao wako tayari na wenye kutaka kusaidia na kufariji wengine wakati wa taabu. (2 Kor. 7:​5-7) Washiriki wa kutaniko hulindwa kupitia ule mpango wa Kimaandiko wa kutenga wale wanaofanya dhambi bila kutubu au wanaoendeleza mawazo ya waasi-imani. (1 Kor. 5:​9-​13; Tito 3:​10, 11) Je! tunaweza kutazamia kupata mipango hiyohiyo yenye upendo wakati tunaposhirikiana na wengine kupitia Internet?

13 Imeonekana kwamba kinyume cha hilo ni kweli. Kwa wazi, vituo fulani vya Web ni njia zinazotumiwa ili kueneza propaganda za waasi-imani. Vituo vya Web kama hivyo vinaweza kusema mambo yaliyo tofauti na haya, na wale wanaogharimia kituo wanaweza kutoa mafasirio yenye habari nyingi ili kuhakikisha kwamba wao kwa kweli ni Mashahidi wa Yehova. Wanaweza hata kuomba habari kutoka kwako ili wahakikishe kwamba wewe ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova.

14 Yehova anataka wewe uonyeshe ufahamu. Kwa nini? Kwa kuwa anajua kwamba huo utakulinda usipatwe na hatari mbalimbali. Mezali 2:​10-​19 linaanza kwa kusema: “Maana hekima itaingia moyoni mwako, na maarifa yatapendeza nafsi yako; akili njema itakulinda, ufahamu utakuchunga.” Kukulinda usipatwe na nini? Na mambo kama vile “njia mbaya,” wale wanaoacha njia za haki, na watu wasio na adili na wenye hila katika mwenendo wao kwa ujumla.

15 Wakati tunapokwenda kwenye Jumba la Ufalme, hakuna shaka kwamba sisi tuko pamoja na ndugu zetu. Tunawajua. Hakuna mtu anayehitaji uhakikisho wa jambo hilo kwa kuwa upendo wa kidugu unaoonyeshwa unafanya hilo liwe wazi. Hatuombwi binafsi kutoa vitambulisho vinavyohakikisha kwamba kwa kweli sisi ni Mashahidi wa Yehova. Ni hapo ndipo tunapata badilishano la kweli la kitia-moyo ambalo Paulo alizungumzia kwenye Waebrania 10:​24, 25. Vituo vya Web vinavyotia moyo kuwa na ushirika kupitia kompyuta haviwezi kutegemewa ili kutoa badilishano hilo la kitia-moyo. Kukumbuka maneno ya Zaburi 26:​4, 5 kunaweza kutuonya tusipatwe na hatari ambazo tungeweza kukutana nazo kwa urahisi wakati tunapotumia vituo vya Web kwenye Internet.

16 Hakuna mipaka wala vizuizi kwa aina ya habari inayodumishwa na inayoweza kufikiwa na watumiaji wa Internet. Mara nyingi, watoto na matineja hupatwa na uhalifu na kutendewa vibaya kwa urahisi katika mazingira hayo. Watoto ni wenye kuamini mambo yote, ni wenye kutafuta kujua mambo, na ni wenye kuhangaikia kufahamiana na ulimwengu wa kompyuta ulio mpya kwa njia fulani. Kwa hiyo, wazazi wanahitaji kuangalia watoto wao na kuwapa mwongozo mzuri wa Kimaandiko kuhusu matumizi ya Internet, kama vile tu wangewaongoza katika uchaguzi wa muziki na sinema.​​—1 Kor. 15:33.

17 Kwa kusikitisha, wengine ambao wakati fulani walikuwa ndugu na dada zetu wamelazimika kutengwa kwa sababu ya ushirika ulioanza kwa kukutana na watu wa ulimwengu katika mahali pa kupigia gumzo kwenye Internet na ambao uliwaongoza hatimaye kwenye ukosefu wa adili. Wazee wamejulisha kwa barua kwamba wengine kwa kweli walikuwa wameacha waume au wake wao ili kufuatia uhusiano ulioanza kwenye Internet. (2 Tim. 3:6) Watu wengine wameikana kweli kwa sababu ya kuamini habari zilizotolewa na waasi-imani. (1 Tim. 4:​1, 2) Kwa kufikiria hatari hizo zilizo kubwa sana, je! halionekani kuwa jambo lenye kupatana na akili nzuri kuwa waangalifu kuhusu kujihusisha katika vipindi vya kupiga gumzo kwenye Internet? Bila shaka, kuonyesha hekima, maarifa, uwezo wa kufikiri, na ufahamu vinavyozungumziwa kwenye Mezali 2:​10-​19 kungepaswa kutulinda katika njia hiyo.

18 Jambo la maana ni kwamba kumekuwa watu fulani ambao wameunda vituo vya Web ili, kama inavyoonekana kwa nje, kuhubiri habari njema. Vingi vya vituo hivyo hugharimiwa na ndugu wasio na busara. Vituo vingine vinaweza kugharimiwa na waasi-imani wanaotaka kuvuta wale wasioshakia mambo. (2 Yn. 9-​11) Ikieleza ikiwa kuna uhitaji kwa ndugu zetu kuunda vituo kama hivyo vya Web, Huduma Yetu ya Ufalme ya Desemba 1997, ukurasa 5 ilisema: “Si lazima mtu kibinafsi kufanya kurasa za Internet juu ya Mashahidi wa Yehova, utendaji wetu mbalimbali na imani yetu. Nafasi [kituo] yetu yenye kujulikana kisheria [www.watchtower.org] hutoa habari kamili zinazoweza kufikia kila mtumiaji wa Internet.”

19 Vichapo vinavyosaidia kwa ajili ya funzo kupitia Internet Wengine wamefikiri kwamba wanasaidia akina ndugu kwa kuweka habari zilizofanyiwa utafiti kuhusu utendaji mbalimbali wa kitheokrasi. Kwa mfano, mtu fulani anaweza kufanya utafiti wenye msingi juu ya muhtasari wa hotuba ya watu wote na kisha aweke utafiti huo kwenye Internet, akifikiri kwamba habari hiyo itafaidi wale wanaohitaji kutayarisha muhtasari huohuo. Wengine wataweka maandiko yote kwa ajili ya Funzo lijalo la Mnara wa Mlinzi au kutoa vyanzo vya habari (vichapo) kwa ajili ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi au Funzo la Kitabu la Kutaniko. Wengine wanaweza kutoa madokezo kwa ajili ya utoaji katika huduma ya shambani. Je! hivyo ni vyenye kusaidia kwelikweli?

20 Vichapo vinavyotolewa na tengenezo la Yehova huchochea akili zetu kupitia mawazo yenye kujenga, na hivyo hutuzoeza “kutofautisha lililo sahihi na lililo kosa pia.” (Ebr. 5:​14) Je! tunaweza kusema kwamba hilo hutimizwa ikiwa watu wengine wanafanya utafiti kwa ajili yetu?

21 Ilisemwa kwamba Wakristo katika Beroya walikuwa “wenye akili ya uelekevu bora zaidi kuliko wale katika Thesalonike.” Kwa nini? Kwa kuwa “walilipokea neno kwa hamu ya akili iliyo kubwa zaidi sana, wakiyachunguza Maandiko kwa uangalifu kila siku juu ya kama mambo hayo yalikuwa hivyo.” (Mdo. 17:11) Ijapokuwa Paulo na Sila waliwahubiria, wao hawangeweza kufanya kweli iwe mali yao wenyewe bila kushiriki wao binafsi.

22 Kutumia utafiti wa mtu mwingine kwa ajili ya hotuba au kwa ajili ya matayarisho mengine ya mikutano kunafanya kusudi la funzo la binafsi liwe bure. Je! wewe hautamani kujenga imani yako binafsi katika Neno la Mungu? Kwa msingi wa usadikisho wa binafsi, ndipo unaweza kueleza imani yako peupe​—katika hotuba zako, katika maelezo kwenye mikutano, na katika huduma ya shambani. (Rom. 10:10) Kutumia utafiti wa mtu mwingine hakupatani na maelezo yanayotolewa kwenye Mezali 2:​4, 5 ya mtu binafsi ‘kutafuta na kutafutatafuta maarifa ya Mungu kama hazina zilizofichwa.’

23 Kwa mfano, wakati unapotafuta maandiko katika nakala yako mwenyewe ya Biblia, unaweza kurudilia kwa kifupi mawazo yanayozunguka kila andiko. Unaweza ‘kufuatisha mambo yote kwa usahihi,’ kama alivyofanya Luka wakati alipoandika Injili yake. (Luka 1:3) Jitihada ya ziada itakusaidia pia kuwa fundi katika kutafuta maandiko katika huduma ya shambani na wakati unapotoa hotuba. Wengi wamesema kwamba Mashahidi wa Yehova huwagusa moyo kwa sababu wanajua jinsi ya kutumia Biblia zao. Jambo hilo linaweza kuwa kweli kwetu ikiwa tu tunafanya liwe zoea letu binafsi kutafuta maandiko katika Biblia zetu wenyewe.

24 Kutumia wakati wetu kwa hekima: Jambo jingine la kufikiria kwa upande huo linahusiana na kiasi cha wakati tunachopitisha kwa kuunda, kwa kusoma, na kwa kujibu habari zinazowekwa kwenye Internet. Zaburi 90:12 linatutia moyo kusali: “Utufundishe kuhesabu siku zetu, tujipatie moyo wa hekima.” Paulo alisema: “Wakati ubakio umepunguzwa.” (1 Kor. 7:​29) Alisema pia: “Basi, kwa kweli maadamu tuna wakati wenye kufaa kwa ajili ya hilo, acheni sisi tufanye lililo jema kuelekea wote, lakini hasa kuelekea wale ambao katika imani ni jamaa zetu.”​​—Gal. 6:​10.

25 Shauri kama hilo linatia mkazo juu ya uhitaji tulio nao wa kuwa wenye busara katika matumizi ya wakati wetu. Ni jambo lenye kufaidi zaidi kama nini kupitisha wakati kwa kusoma Neno la Mungu! (Zab. 1:​1, 2) Huo ndio ushirika mzuri zaidi tunaoweza kuwa nao. (2 Tim. 3:​16, 17) Wazazi, je! nyinyi ni wenye kufundisha watoto wenu waone thamani ya kutumia wakati kwa hekima katika kufuatia Ufalme? (Mhu. 12:1) Wakati unaotumiwa katika funzo la Biblia la binafsi na la familia, katika kuhudhuria mikutano, na katika huduma ya shambani unapita kwa mbali faida yoyote inayofikiriwa ambayo wengine hutazamia kupata kutokana na kupekua Internet.

26 Kwa upande huo, ni mwendo wa hekima kukaza uangalifu wetu kwenye mambo ya kiroho, na yale yanayohusu maisha yetu tukiwa Wakristo na yaliyo ya lazima kwa maisha hayo. Hilo laomba kufanya uchaguzi wenye kufikiriwa vizuri kuhusu habari inayostahili tuitolee wakati na mawazo yetu. Tukiwa Wakristo, lile linalohusiana na maisha yetu lilielezwa kwa kifupi na Yesu, ambaye alisema: “Fulizeni kutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake [wa Mungu], na vitu vingine vyote hivi mtaongezewa.” (Mt. 6:​33) Je! wewe si mwenye furaha zaidi wakati maisha yako yanajaa ufuatiaji wa Ufalme badala ya utendaji mwingine wowote?

27 Barua za kielektroniki kupitia Internet: Ingawa kushiriki mambo yaliyoonwa au mawazo ya binafsi pamoja na familia au marafiki wanaoishi mbali ni jambo lenye kufaa, je! ni jambo lenye upendo kwelikweli kutoa hayo kwa wengine ambao huenda hawajui familia na marafiki wako? Au je! hayo yanapaswa kuwekwa kwenye ukurasa wa Web ili kila mtu ayasome? Je! jumbe hizo za binafsi zinapaswa kuandikwa na kutumwa ovyoovyo kwa watu ambao huenda unawajua au hauwajui? Vivyo hivyo, ikiwa unapokea kutoka kwa wengine jumbe ambazo kwa wazi hazikukusudiwa kutumwa kwako, je! ni jambo lenye upendo kuzituma tena kwa wengine?

28 Namna gani ikiwa jambo lililoonwa ambalo unatoa si la kweli? Je! huko hakungekuwa kushiriki katika kuendeleza uwongo? (Mez. 12:19; 21:28; 30:8; Kol. 3:9) Bila shaka, kufuliza ‘kuangalia sana kwamba jinsi tunavyotembea si kama wasio na hekima bali kama watu wenye hekima’ kungepaswa kutuchochea tufikirie jambo hilo. (Efe. 5:​15) Sisi ni wenye furaha kama nini kuona kwamba Kitabu-Mwaka, Mnara wa Mlinzi, na Amkeni! vinajaa mambo yaliyoonwa yanayoweza kuhakikishwa ambayo hututia moyo na kutuchochea tuendelee kutembea katika ile “njia”!​​—Isa. 30:​20, 21.

29 Kuna hatari nyingine pia. Mtume Paulo alisema kuhusu watu fulani: “Wao hujifunza pia kuwa wasio na shughuli, wakizurura huku na huku kwenye nyumba; ndiyo, si wakiwa wasio na shughuli tu, bali pia wapiga-porojo na wajiingizaji katika mambo ya watu wengine, wakiongea juu ya mambo yasiyowapasa.” (1 Tim. 5:​13) Hilo linatoa sababu za kuepuka kutumia wakati na jitihada kwa kutoa habari zisizo na maana kwa ndugu zetu.

30 Fikiria pia kiasi cha wakati ambacho kinahitajiwa ili kuendelea na kiasi kikubwa cha barua za kielektroniki. Kwa kupendeza, kitabu Data Smog kilisema: “Kadiri mtu anavyopitisha wakati mwingi zaidi akizungumza kupitia kompyuta, barua za kielektroniki hubadilika kwa haraka: hizo haziwi tena mambo mapya yenye kuchochea, lakini zinageuka kuwa mzigo wenye kula wakati, zikiwa na makumi ya jumbe za kusoma na kujibu kila siku kutoka kwa washiriki wenzi, marafiki, familia, . . . na habari zisizotakwa za kuvumisha biashara.” Kitabu hicho kinaendelea kusema: “Watu wengi wenye kupenda sana habari za kielektroniki wamekuwa na zoea mbaya sana la kutuma habari yote yenye kuburudisha wanayopokea​—mizaha, ngano za mijini, barua za kielektroniki ambazo mtu mwenye kuzipokea anapaswa kutuma kwa watu wengine, na zaidi​—kwa kila mtu aliye katika kitabu chao cha anwani cha kielektroniki.”

31 Hilo limekuwa wazi katika barua za kielektroniki zilizozunguka kati ya akina ndugu​—mambo kama vile mizaha au habari za kuchekesha kuhusu huduma; mashairi yanayodhaniwa kuwa yenye msingi juu ya imani zetu; mifano kutoka katika hotuba mbalimbali zilizosikiwa kwenye mikusanyiko, makusanyiko, au kwenye Jumba la Ufalme; mambo yaliyoonwa kutoka katika huduma ya shambani; na kadhalika​—mambo yanayoonekana kuwa hayana ubaya wowote. Kwa kawaida, wengi hutuma barua hizo za kielektroniki bila kujihakikishia chanzo, wakifanya iwe vigumu kujua kwa kweli ni nani aliye mwanzishi, jambo linalofanya mtu ajiulize ikiwa habari hiyo ni sahihi kwelikweli.​​—Mez. 22:​20, 21.

32 Jumbe hizo ambazo mara nyingi hazina maana ni tofauti na aina ya maneno yenye afya ambayo Paulo alikuwa akifikiria wakati alipoandikia Timotheo, akisema: “Fuliza kushika kiolezo cha maneno yenye afya ulichosikia kutoka kwangu pamoja na imani na upendo vinavyohusiana na Kristo Yesu.” (2 Tim. 1:​13) Ile “lugha safi” ya kweli za Kimaandiko inacho “kiolezo cha maneno yenye afya” ambayo ni yenye msingi zaidi juu ya kichwa cha Biblia, yaani kule kutetewa kwa enzi kuu ya Yehova kupitia Ufalme. (Zef. 3:9) Tunapaswa kufanya jitihada yote ili kutoa wakati na nguvu tulivyo navyo ili kutegemeza uteteaji huo wa enzi kuu ya Yehova.

33 Kwa kuwa tuko mbali katika wakati wa mwisho wa mfumo huu wa mambo, huu si wakati wa kupunguza uangalifu wetu. Biblia inatuonya: “Tunzeni akili zenu, iweni wenye kulinda. Mpinzani wenu, Ibilisi, hutembea huku na huku kama simba anayenguruma, akitafuta sana kunyafua mtu fulani.” (1 Pet. 5:8) Kwa kuongezea, hiyo inasema: “Vaeni suti kamili ya silaha kutoka kwa Mungu ili mpate kuweza kusimama imara dhidi ya mbinu za Ibilisi.”​​—Efe. 6:​11.

34 Ikiwa inatumiwa vibaya, Internet inaweza kuwa njia ambayo Shetani anatumia ili kushinda wale wanaoshawishwa na uwezo wa hiyo. Ingawa hiyo inaweza kuwa na mafaa yenye mipaka, kuna hatari ikiwa hiyo haiangaliwi kwa uangalifu. Wazazi zaidi wanahitaji kuhangaikia matumizi ya watoto wao ya Internet.

35 Kudumisha maoni yenye usawaziko kuhusu Internet ni ulinzi. Tunathamini kikumbusho kinachotolewa kwa wakati wenye kufaa na Paulo: “Acheni . . . wale wanaoutumia ulimwengu [wawe] kama wale wasioutumia kwa ukamili; kwa maana mandhari ya ulimwengu huu inabadilika.” (1 Kor. 7:​29-31) Kuwa na mambo hayo akilini kutasaidia kutufanya, sisi na familia zetu, tusikengeushwe na yale yote ambayo ulimwengu huu unatoa, kutia ndani mambo yanayopatikana kwenye Internet.

36 Ni jambo la lazima kwetu kubaki karibu na ndugu zetu katika kutaniko na kutumia kwa hekima wakati unaobaki, hivyo tukijifanya wenyewe kuwa tayari kwa ajili ya kuendeleza faida za Ufalme. Kwa kuwa mfumo huu unakaribia mwisho wake, acheni ‘tusiendelee tena kutembea kama vile mataifa watembeavyo pia katika ukosefu wa faida wa akili zao,’ lakini ‘tuendelee kufahamu mapenzi ya Yehova ni nini.’​​—Efe. 4:​17; 5:​17.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine