Habari Njema Kwenye Internet
Wakati huu wa tekinolojia, watu fulani hutafuta habari kutokana na vyianzo vya elektroniki, kama vile Internet (kupashana habari kupitia kompyuta). Ni kwa sababu hiyo Sosaiti imetoa kwa ajili ya watumiaji wa Internet habari kamili kuhusu imani na utendaji mbalimbali wa Mashahidi wa Yehova.
Anwani ya nafasi yetu Web kwenye Internet ni http://www.watchtower.org. Inatoa mchanganyiko wa trakti zilichaguliwa vema, broshua na makala za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! katika Kiingereza, Kifaransa, Kijerumani, Kichaina (kilichorahisishwa), Kihispania, Kirusi na lugha nyingine tena. Vichapo vinavyopatikana kwenye nafasi hiyo ni vile makutaniko yalivyo navyo tayari na vinavyotolewa katika huduma. Kazi ya nafasi yetu ya Web si kutangaza mambo mapya, lakini kutoa kwa watu habari kwa njia ya elektroniki. Si lazima mtu kibinafsi kufanya kurasa za Internet juu ya Mashahidi wa Yehova, utendaji wetu mbalimbali na imani yetu. Nafasi yetu yenye kujulikana kisheria hutoa habari kamili zinazoweza kufikia kila mtumiaji wa Internet.
Ikiwa nafasi yetu Web haikufanywa ili kupokea habari za kielektroniki (E-mail), inatoa hata hivyo orodha ya anwani za matawi mahali pote ulimwenguni. Watu wanaweza kuandika kwa moja ya anwani hizo ili kupata habari nyingi zaidi au kupokea kibinafsi msaada wa Mashahidi wa Yehova wa mtaa wao. Tusisite kujulisha anwani ya Internet iliyo hapo juu kwa kila mtu ambaye angeweza kuwa na tamaa ya kuvumbua ukweli wa Biblia kwa njia hiyo.