Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/02 uku. 8
  • Epuka Ufuatiaji wa ‘Mambo Yasiyo na Maana’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Epuka Ufuatiaji wa ‘Mambo Yasiyo na Maana’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Matumizi ya Internet—Fanyeni angalisho kwa hatari!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Njema Kwenye Internet
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Intaneti Kutumia kwa Hekima Kifaa cha Ulimwenguni Pote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • ‘Mutu Asiye na Uzoefu Anaamini Kila Neno’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 9/02 uku. 8

Epuka Ufuatiaji wa ‘Mambo Yasiyo na Maana’

1 Njia moja ya kupashana habari inayopendwa na watu wengi leo ni barua za kielektroniki. Ingawa kushiriki mambo yaliyoonwa na mawazo pamoja na familia na marafiki kupitia njia hiyo kunaweza kuwa jambo lenye kufaa, ni ‘mambo gani yasiyo na maana’ yanayoweza kushirikishwa na matumizi yasiyozuiwa ya barua za kielektroniki?—Mez. 12:11.

2 Mambo Yanayoomba Uangalifu Kuhusiana na Barua za Kielektroniki: Wengi husema kwamba wanahisi wanapashana habari vizuri zaidi na tengenezo la Yehova wanapopokea yale wanayofikiri kuwa habari za sasa kupitia barua za kielektroniki. Huenda habari hizo zikatia ndani mambo yaliyoonwa, barua fupi kuhusu mambo yaliyotukia Betheli, ripoti kuhusu misiba au mnyanyaso, na hata habari za siri zinazotangazwa kwenye Shule za Huduma ya Ufalme. Wengine wanaonekana kuwa na hamu nyingi mno ya kutuma habari kama hizo, wakitumaini kwamba watakuwa wa kwanza kufunua habari hizo kwa marafiki zao.

3 Nyakati nyingine, habari na mambo yaliyoonwa yamepotoshwa au kutiwa chumvi. Au huenda watu fulani wametoa mawazo yasiyo ya kweli kwa sababu ya kujitahidi kusisimua wengine. Mara nyingi wale walio haraka kufunua mambo kama hayo hawajui ukweli wote. (Mez. 29:20) Katika hali fulani, hata ikiwa hadithi ni isiyoweza kuaminiwa, inapitishwa kwa wengine kuwa jambo la udadisi. Ripoti hizo zisizo sahihi au zenye kudanganya ni “hadithi zisizo za kweli,” ambazo haziendelezi ujitoaji-kimungu wa kweli.—1 Tim. 4:6, 7.

4 Ikiwa unatuma habari ambayo inaonekana kuwa si sahihi, unachukua kiasi fulani cha daraka kuhusiana na huzuni na mvurugo ambao hiyo inaweza kutokeza. Daudi alipopokea ripoti yenye kutiwa chumvi kwamba watoto wake wote walikuwa wameuawa, ‘akapasua mavazi yake’ kwa huzuni. Hata hivyo, kwa kweli, ni mmoja tu wa wana wake ndiye aliyekuwa ameuawa. Hilo lilikuwa jambo lenye kuhuzunisha vya kutosha, lakini habari hiyo iliyotiwa chumvi ilimwongezea Daudi huzuni. (2 Sam. 13:30-33) Bila shaka hatungependa kufanya jambo lolote ambalo lingedanganya au kuvunja moyo yeyote kati ya ndugu zetu.

5 Njia Iliyowekwa Rasmi na Mungu: Kumbuka kwamba Baba yetu wa mbinguni ana njia iliyowekwa rasmi ya kupasha habari, yaani “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” Huyo “mtumwa” ana daraka la kuamua habari inayofaa kutolea nyumba ya imani, na pia “wakati ufaao” wa kutoa habari hiyo. Chakula hicho cha kiroho kinapatikana tu kupitia tengenezo la kitheokrasi. Tunapaswa sikuzote kutafuta habari yenye kuaminika kupitia njia iliyowekwa rasmi na Mungu, si kupitia mtandao wa watumiaji wa Internet.—Mt. 24:45.

6 Vituo vya Internet: Tunacho kituo cha Internet kinachojulikana kisheria: www.watchtower.org. Kituo hicho kinatosha ili kutolea watu wote habari. Hakuna uhitaji wa mtu yeyote, halmashauri yoyote, au kutaniko lolote kutayarisha ukurasa wa Internet kuhusu Mashahidi wa Yehova. Watu fulani wametia habari zinazopatikana katika vichapo vyetu pamoja na maandiko na mitajo iliyotolewa kwa ukamili, na wametoa hata nakala za habari iliyozungumziwa kwenye kusanyiko huku wakiomba michango. Iwe kwamba kuna faida inayohusika au hakuna, zoea la kutoa upya na kugawa vichapo vya Mashahidi wa Yehova vikiwa hati ya kielektroniki ni uvunjaji wa sheria za haki ya kunakili. Ingawa huenda watu fulani wakaona hilo kuwa msaada kwa akina ndugu, jambo hilo halikubaliwi na halipaswi kuendelea.

7 Kutumikisha uamuzi mzuri na utimamu wa akili tunapotumia mfumo wa kielektroniki wa kupashana habari kutahakikisha kwamba akili zetu zinajaa ‘mali zote za thamani na za kupendeza.’—Mez. 24:4.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine