Kituo cha Habari Kinachosaidia Watu
Wakristo wa kweli wanashiriki katika huduma ya watu wote ya kueneza ile habari njema. (Flp. 2:17) Ili kutimiza hilo, broshua, trakti, na makala mbalimbali katika lugha 20 zimepatikana kwenye anwani yetu ya Internet www.watchtower.org. Kituo hicho cha Internet hakikusudiwi kugawa vichapo vya sasa kwa Mashahidi wa Yehova. Kusudi lake ni kutolea watu wote habari sahihi kuhusu yale ambayo Mashahidi wa Yehova wanafundisha kutoka Biblia.
Hivi karibuni, jambo la maana limeongezwa kwenye kituo chetu cha Internet chenye kujulikana kisheria. Hilo ni broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? katika lugha zaidi ya 220. Pia, kuanza na matoleo ya Januari 1 na Januari 8, 2004, magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! katika lugha zote ni yenye kuonyesha anwani ya kituo chetu cha Internet kwenye ukurasa wa mwisho.
Unawezaje kutumia chombo hicho? Unaweza kukutana na mtu anayeonekana kuwa mwenye kupendezwa lakini anayeelewa tu lugha nyingine. Ikiwa anatumia Internet, unaweza kumwonyesha anwani ya kituo chetu cha Internet kwenye ukurasa wa mwisho wa Mnara wa Mlinzi au Amkeni! Kwa kutumia anwani hiyo, anaweza kuchunguza broshua Anataka katika lugha yake mpaka utakaporudi ili kumletea kichapo katika lugha yake. Au unaweza kujulisha kutaniko au kikundi kinachozungumza lugha inayohusika kuhusu ziara hiyo.