MAISHA YA MUKRISTO
Unaweza Kujitolea?
Sawa vile Isaya alitabiri, leo mu sehemu ya ku dunia ya tengenezo la Yehova, muko maendeleo sana kupita zamani. (Isa 54:2) Njo maana inaomba kujenga Majumba ingine ya Ufalme, Majumba ya Mikusanyiko, na majengo mbalimbali ya Beteli. Zaidi tu ya kujenga, inaomba kuendelea kuitunza muzuri na kuitengeneza kama inaharibika. Ni mambo gani tunaweza kufanya ili kutegemeza ile kazi?
Kama ni siku ya kikundi chetu cha mahubiri kusafisha Jumba la Ufalme, tunapaswa kuunga mukono
Tunaweza kujitolea ili kupata mazoezi juu ya namna ya kutunza muzuri Jumba la Ufalme
Tunaweza kujaza fomu Demande d’admission comme volontaire local développement/construction (DC-50) juu tukuwe tunasaidia wakati kuko kazi ya kujenga na kutunza majengo yenye iko karibu na kwetu
Tunaweza kujaza fomu Demande d’admission comme volontaire (A-19) na kujitoa ili kutumika juma moja ao zaidi ku Beteli ao ku majengo ingine ya Beteli
MUANGALIE VIDEO MIPANGO YA KUJENGA MAKAO INGINE YA MUPYA—SEHEMU, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Namna gani, kuanzia 2014, tuko tunatumia sana video kuliko zamani?
Juu tupate video zote zenye tuko nazo lazima ili kumuabudu Yehova, ni mipango gani yenye iko inafanywa, na itaanza na kuisha wakati gani?
Namna gani wajitoleaji wanaweza kusaidia?
Kama tunapenda kusaidia kazi ya kujenga yenye itafanywa Ramapo, juu ya nini tunapaswa kujaza fomu (DC-50) na kusaidia kazi za LDC zenye kufanywa karibu na kwetu?
Ni mambo gani inaonyesha kama Yehova iko anaongoza hii mupango?
Namna gani naweza kutegemeza hii mupango hata kama hali yangu hainiruhusu nikuwe kwenye ile kazi itafanywa?