Mipango ya Ofisi ya Tawi Kuhusu Ujenzi Ni Sehemu ya Maana ya Utumishi Mtakatifu
1 Miaka mitano iliyopita, Majumba ya Ufalme 564 yalijengwa au kutengenezwa katika eneo linalosimamiwa na ofisi yetu. Tunathamini sana kazi ngumu ambayo ndugu na dada wa makutaniko mbalimbali wamefanya, ndugu na dada ambao wamesaidia wafanyakazi wa wakati wote waliotumwa na ofisi ya tawi. Ijapokuwa kazi kubwa imetimizwa, bado kungali mambo mengi ya kufanya kuhusiana na ujenzi wa Majumba ya Ufalme na mipango mingine ya ujenzi kama vile ujenzi wa Majumba ya Mikusanyiko katika Limete, mjini Kinshasa, Kisangani katika province orientale, na Brazzaville katika Jamhuri ya Congo. Namna gani sisi wote tunaweza kutegemeza sehemu hii ya maana ya utumishi wetu mtakatifu kwa Yehova?—Ufu. 7:15.
2 Uwe na Nia Tayari: Ikiwa wewe ni mhubiri aliyebatizwa, tunakuomba ujitolee ili kutumika katika mipango mbalimbali ya ujenzi, hasa wakati Jumba lenu la Ufalme ni lenye kujengwa au kutengenezwa. (Zab. 110:3) Wote wanaojitolea wanapaswa kuwa wenye nia tayari na kuwa na roho ya kushirikiana na wengine. (Zab. 133:1) Hata ikiwa hauna ujuzi katika mambo ya ujenzi, unaweza kusaidia sana ili mpango wa ujenzi ufanikiwe. Unaweza pia kupata mazoezi yatakayokusaidia kushiriki katika mipango ya ujenzi wakati ujao.
3 Ikiwa hauwezi kujitolea, unaweza kutegemeza kazi hiyo kwa kutia moyo wale wanaoweza kushiriki katika mpango huo. Unaweza kusaidia kwa kutimiza migawo yao katika kutaniko wakati wanapoenda kushiriki katika ujenzi. Kwa kupanga mambo kimbele, wazee wanaweza kusaidia kutaniko ili lisipungukiwe na chochote wakati ndugu na dada fulani wanashiriki katika mpango wa ujenzi wa Jumba la Ufalme au katika mpango wowote wa ujenzi unaoanzishwa na ofisi ya tawi. Bila shaka, Yehova anapendezwa tunapotumika pamoja kwa umoja ili kuendeleza faida za Ufalme.—Ebr. 13:16.
4 Uwe Mwenye Kutia Moyo: Kujenga mahali pa ibada na kufanya kazi nyingine ya Ufalme inayohusiana na ujenzi kunataka wakati mwingi na kazi ngumu. Ni wazi kwamba, nyakati nyingine, wale wanaoalikwa ili kusaidia katika mipango ya ujenzi watakuwa mbali na makutaniko yao. Basi, tusikose kuwapongeza na kuwatia moyo wale wanaojitolea kwa kazi ya ujenzi na wanaojinyima ili kufanya “kazi hii ya lazima.”—Mdo. 6:3; Rom. 14:19.
5 Uwe Mwenye Kusawazika: Kuhubiri Ufalme wa Mungu ndio utendaji wetu wa kitheokrasi wa maana sana. (Marko 13:10) Kwa hiyo, ofisi ya ujenzi inajitahidi kufanya mipango ili wanaojitolea wasikose kushiriki katika mikutano yao bila sababu yenye kufaa. Vivyohivyo, wanaojitolea kufanya kazi ya ujenzi wanajitahidi kusawazika ili kutimiza madaraka yao mengine mengi. Wanachukua mipango ya lazima ili migawo yao itimizwe wakati hawako katika kutaniko. Wale walio mapainia wanapaswa kukazia uangalifu wao kwenye mgawo wao wa kuhubiri wakati wote. Hata hivyo, wanaweza kusaidia kwa kutumika na wengine wakitumia kiasi fulani cha wakati kwa ajili ya mpango fulani wa ujenzi.
6 Mtume Paulo alionyesha kwamba washiriki wa kutaniko wanapaswa kutumika pamoja kwa umoja kwa ajili ya “ukuzi wa mwili ili huo ujijenge wenyewe katika upendo.” (Efe. 4:16) Upendo wetu kwa Yehova na kwa ibada ya kweli unatuchochea kutumika pamoja ili kutegemeza kazi ya kuhubiri na pia mipango ya Ufalme inayohusu ujenzi.
[Maulizo ya Funzo]
1. Ni jambo gani ambalo limetimizwa kuhusiana na ujenzi wa Majumba ya Ufalme na mipango mingine ya ujenzi inayoongozwa na ofisi yetu, lakini bado kungali uhitaji wa kufanya nini?
2. Namna gani tunaweza kutegemeza moja kwa moja kazi ya ujenzi inayoanzishwa na ofisi ya tawi?
3. Ni katika njia gani nyingine tunaweza kuonyesha kwamba tunategemeza mpango huo?
4. Namna gani tunaweza kutia moyo wale wanaoshiriki katika mipango mbalimbali ya ujenzi?
5. Namna gani wale wanaojitolea katika kazi ya ujenzi wanaonyesha kuwa wenye kusawazika?
6. Ni jambo gani linalotimizwa wakati washiriki wote wa kutaniko wanatumika pamoja ili kuendeleza ibada ya kweli?