Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb20 Mwezi wa 12 uku. 3
  • Tunaonyesha Upendo kwa Kuunga Mukono Maamuzi ya Yehova Kuhusu Nizamu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tunaonyesha Upendo kwa Kuunga Mukono Maamuzi ya Yehova Kuhusu Nizamu
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Nizamu Inaonyesha Kama Yehova Anatupenda
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
  • Sababu Gani Kutengwa na Kutaniko ni Mupango Wenye Upendo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Wakati Mupendwa Wako Anamuacha Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Nizamu—Inaonyesha Upendo wa Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
mwb20 Mwezi wa 12 uku. 3

MAISHA YA MUKRISTO

Tunaonyesha Upendo kwa Kuunga Mukono Maamuzi ya Yehova Kuhusu Nizamu

Kutenga watenda-zambi wenye hawatubu kunalinda kutaniko na kunawapatia nizamu. (1Ko 5:6, 11) Tunaonyesha upendo wakati tunaunga mukono ile nizamu kutoka kwa Yehova. Tunajua kama kutengwa kunaumizaka halmashauri ya hukumu na watu wa familia ya mutengwa; sasa namna gani kuunga mukono ule uamuzi ni alama ya upendo?

Sababu ya kwanza kabisa, ni kuonyesha kama tunapenda Yehova asifiwe na tunapenda kubakia watakatifu kulingana na kanuni zake. (1Pe 1:14-16) Pia tunaonyesha kama tunapenda mutu mwenye alitengwa. Hata kama nizamu inaumizaka sana, inaweza kuzaa “tunda lenye amani la haki.” (Ebr 12:5, 6, 11) Tunaweza kuzarau nizamu ya Yehova kama tuko tunashirikiana na mutu mwenye kutengwa ao na ule mwenye alijitenga na kutaniko. Tukumbuke kama Yehova anapatiaka watu wake nizamu “kwa kiasi chenye kufaa.” (Yer 30:11) Wakati tuko tunaunga mukono uamuzi wa Yehova kuhusu nizamu na kuendelea kufanya urafiki wetu na Yehova ukuwe nguvu, tusisahau kama ule mutengwa anaweza kumurudilia Baba yetu mwenye rehema.​—Isa 1:16-18; 55:7.

MUANGALIE VIDEO ENDELEA KUWA MUSHIKAMANIFU KWA MOYO WOTE, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Sehemu moja ya video ‘Endelea Kuwa Mushikamanifu kwa Moyo Wote.’ Gabriella na Ben wanahuzunika kisha kusoma barua ya mutoto wao mwanaume mwenye aliamua kutoka ku nyumba.

    Wazazi Wakristo wanajisikiaka namna gani wakati mutoto wao anamuacha Yehova?

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Endelea Kuwa Mushikamanifu kwa Moyo Wote.’ Marafiki wa Gabriella na Ben wanawakumbatia na kuwatia moyo kisha mukutano.

    Ndugu na dada wanaweza kufanya nini ili kusaidia watu wa familia ya mutengwa wenye wangali waaminifu?

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Endelea Kuwa Mushikamanifu kwa Moyo Wote.’ Gabriella iko anafikiria habari kuhusu uasi wa Kora.

    Ni habari gani yenye kuwa mu Biblia yenye inaonyesha kama ushikamanifu wetu kwa Yehova unapaswa kuwa nguvu sana kupita ushikamanifu wetu kwa familia?

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Endelea Kuwa Mushikamanifu kwa Moyo Wote.’ Kisha mukutano, Gabriella anaonyesha Ben ujumbe wenye mutoto wao alimutumia.

    Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunashikamana sana na Yehova kuliko familia yetu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine