Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb20 Mwezi wa 12 uku. 7
  • Unapendaka Kujaza Fomu kwa Ajili ya Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unapendaka Kujaza Fomu kwa Ajili ya Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme?
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wahubiri wa Ufalme Wanapewa Mazoezi
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Ujaze Fomu ya Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2022
  • Wamisionere “Mupaka Kwenye Sehemu ya Mbali Zaidi ya Dunia”
    Namna Michango Yako Inatumiwa
  • Ni Masomo Gani Yenye Kutayarishwa kwa Ajili ya Mapainia?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
mwb20 Mwezi wa 12 uku. 7
Wanafunzi wengi wako ku Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme.

MAISHA YA MUKRISTO

Unapendaka Kujaza Fomu kwa Ajili ya Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme?

Uko na miaka kati ya 23 na 65 na uko mu utumishi wa wakati wote? Uko na afya ya muzuri, na uko na uwezo wa kutumikia fasi yote kwenye kuwa lazima kubwa? Kama unajibia ndiyo ku ile maulizo yote, ulishaka fikiria kujaza fomu kwa ajili ya Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme? Tangu masomo ya kwanza ya Waeneza-Injili wa Ufalme ianze, ndugu na dada wengi wenye kuoana, na ndugu na dada wengi wenye hawajaoa ao kuolewa walishajaza fomu na wengine walishasoma. Lakini ku ile masomo, tuko na lazima sana ya ndugu wengi wenye hawajaoa. Umuombe Yehova akomalishe tamaa yako ya kumufurahisha na ya kuiga Mutoto wake, Yesu. (Zb 40:8; Mt 20:28; Ebr 10:7) Kisha, ili ustahili kusoma ile masomo, fikiria namna unaweza kufanya ili kazi yako ya kimwili ao mambo ingine ya kipekee isikuzuie.

Wale wenye wamesoma ile masomo, wamepata nafasi ya kutumikia wapi na mu migawo gani? Wamoja wametumwa mu maeneo kwenye watu wanazungumuza luga zingine ao mu miji mikubwa ili kuhubiri mahali pa watu wengi. Wengine wamefikia kuwa waangalizi wa badala, waangalizi wa mizunguko ao wamisionere. Wakati uko nawaza juu ya mambo yenye unaweza kufanya mu kazi ya Yehova, ukuwe sawa vile nabii Isaya mwenye alisema: “Mimi huyu! Unitume mimi!”​—Isa 6:8.

MUANGALIE VIDEO WAMISIONERE WENYE KUFANYA KAZI YA MAVUNO, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Wamisionere Wenye Kufanya Kazi ya Mavuno.’ Bibi na bwana wamisionere wako mu kazi ya kuhubiri.

    Wamisionere wanachaguliwaka namna gani?

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Wamisionere Wenye Kufanya Kazi ya Mavuno.’ Misionere mumoja na dada mwingine wako wanajifunza Biblia na mwanamuke.

    Ni kazi gani ya muzuri yenye wamisionere wanafanyaka?

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Wamisionere Wenye Kufanya Kazi ya Mavuno.’ Ndugu mumoja misionere iko mu eneo la luga ya ishara na iko anazungumuza na ndugu kuhusu fomu fulani ya utumishi wa pekee.

    Ni baraka gani fulani zenye wamisionere wanapataka?

Kama unapenda kujua mambo mingi juu ya masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme, fungua sehemu “Video Mbalimbali” ku jw.org, na uangalie sehemu KAZI ZETU > MASOMO MBALIMBALI YA KITEOKRASI. Angalia video Masomo ya Kiteokrasi mu Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Tumekuwa Matajiri Kiroho kwa Sababu ya Mafundisho ya Yehova, na Wanafunzi wa Masomo ya Kwanza ya Waeneza-Injili wa Ufalme Wanapewa Diplome.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine