Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb21 Mwezi wa 1 uku. 11
  • Amua Kumutumikia Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Amua Kumutumikia Yehova
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Utapata Faida Kama Unajikaza Juu Ufikie Kubatizwa?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Ubatizo—Ni wa Maana Sana kwa Wakristo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Ubatizo Ni Hatua Inayomuongoza Mutu Kwenye Uhusiano Muzuri Pamoja na Mungu
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Uko Tayari Kubatizwa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
mwb21 Mwezi wa 1 uku. 11
Njia yenye kujikunjakunja yenye inafananisha barabara ya kumutumikia Yehova. Alama zenye kuwa pembeni ya barabara zenye zinafananisha hatua ya kujifunza Biblia, kuhuzuria mikutano, na ya kubatizwa.

Unafikia wapi mu barabara yenye kuongoza kwenye ubatizo?

MAISHA YA MUKRISTO

Amua Kumutumikia Yehova

Kama uko kijana Mukristo ao mwanafunzi wa Biblia, unapenda kubatizwa? Juu ya nini unapaswa kubatizwa? Kujitoa kwa Yehova katika sala na kubatizwa, ni mambo yenye inakusaidia uanzishe urafiki wa pekee pamoja na Yehova. (Zb 91:1) Itakusaidia pia uokolewe wakati wenye kuja. (1Pe 3:21) Ni mambo gani yenye unapaswa kufanya juu ufikie kubatizwa?

Ujihakikishie kama hii njo kweli. Tafuta habari juu upate majibu ya maulizo fulani yenye uko nayo. (Ro 12:2) Ona kama kuko mambo fulani yenye unaweza kubadilisha, na ufanye vile juu ya kumufurahisha Yehova. (Mez 27:11; Efe 4:23, 24) Ukuwe na zoezi ya kusali kwa Yehova kila siku ili akusaidie. Ukuwe hakika kama Yehova atakupatia roho yake takatifu ili kukutegemeza na kukupatia nguvu. (1Pe 5:10, 11) Bidii yako haiko ya bure. Kumutumikia Yehova njo jambo la maana sana mu maisha!​—Zb 16:11.

MUANGALIE VIDEO BARABARA YENYE KUONGOZA KWENYE UBATIZO, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Watu fulani walipiganisha vizuizi gani juu wafikie kubatizwa?

  • Unaweza kufanya nini ili imani yako ikuwe nguvu na ufikie kutoa maisha yako kwa Yehova katika sala?

  • Ni mambo gani yenye ilisukuma wengine waamue kubatizwa?

  • Wale wenye wanaamua kumutumikia Yehova wanapata baraka gani?

  • Kujitoa kwa Yehova katika sala na kubatizwa viko na maana gani?

Mu maneno ya kumalizia hotuba ya ubatizo, musemaji ataomba wale wenye watabatizwa wasimame na wajibu kwa sauti maulizo mbili yenye kuwa hapa chini:

Umetubu zambi zako, umejitoa mwenyewe kwa Yehova katika sala, na umekubali wokovu wenye anatoa kupitia Yesu Kristo?

Unaelewa kama wakati unabatizwa unakuwa Shahidi wa Yehova na unaingia sasa mu tengenezo la Yehova?

Wakati wale wenye watabatizwa wanajibu ndiyo ku hii maulizo mbili, ‘wanatangaza mbele ya watu wote’ kama wanaamini bei ya ukombozi na kama wamejitoa kabisa kwa Yehova katika sala.​—Ro 10:9, 10.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine