TUJITOE KABISA KATIKA KAZI YA KUHUBIRI | ONGEZA FURAHA YAKO MU KAZI YA KUHUBIRI
Jitie pa Nafasi ya Wengine
Huruma ao kujitia pa nafasi ya wengine ni uwezo wa kuelewa mawazo ya mutu mwingine, namna anajisikia, namna yake ya kuona mambo, na mahitaji yake. Ni mwepesi wengine kuona vile tunawasikilia huruma. Na ile inatusukuma tukuwe tayari kuwasaidia. Wakati tunajitia pa nafasi ya wengine mu kazi ya kuhubiri, sawa vile Yehova, tunaonyesha kuwa tunawapenda na tunawahangaikia, na ile inafanya wamukaribie.—Flp 2:4.
Hatuone kujitia pa nafasi ya wengine kuwa tu ufundi wa kutumia mu mahubiri. Lakini, ile inaonekana mu namna yetu ya kusikiliza na ya kusema; na pia inaonekana mu mutazamo na mu ishara zetu za uso na za mwili. Tunaonyesha kama tunajitia pa nafasi ya mutu fulani, wakati tunapendezwa naye kipekee. Tunahangaikia mambo yenye anapenda, imani na hali yake. Tunasaidia mwanafunzi na kumupatia habari zenye iko nazo lazima. Lakini, hatutamukaza kufanya mabadiliko. Wakati watu wanakubali tuwasaidie, ile inafanya furaha yetu iongezeke mu kazi ya kuhubiri.
MUANGALIE VIDEO PATA FURAHA KATIKA KAZI YA KUFANYA WANAFUNZI—KOMALISHA UFUNDI WAKO—KWA KUJITIA PA NAFASI YA WENGINE, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Namna gani Neeta alijitia pa nafasi ya Rose wakati alichelewa?
Namna gani Neeta alijitia pa nafasi ya Rose wakati alimuambia kama hana nguvu ya kujifunza?
Watu watamukaribia Yehova kama tunajitia pa nafasi yao
Namna gani Neeta alijitia pa nafasi ya Rose wakati alimuambia kama hawezake kupanga vitu muzuri?