MAISHA YA MUKRISTO
“Upendo . . . Haufurahie Ukosefu wa Haki”
Mu mambo yote yenye Wakristo wanafanyaka, wanajikazaka kuacha upendo uwaongoze. Upendo “haufurahie ukosefu wa haki.” (1Ko 13:4, 6) Kwa hiyo, tunaepuka mambo ya kujifurahisha yenye inasifu uasherati na jeuri. Pia, hatufurahi wakati wengine wanapatwa na mambo ya mubaya, hata kama ni wale wenye walituumiza.—Mez 17:5.
MUANGALIE VIDEO KUMBUKA NAMNA UPENDO UNAJIENDESHA—HAUFURAHIE UKOSEFU WA HAKI, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Daudi alitenda namna gani wakati alipata habari kama Sauli na Yonatani wamekufa?
Ni wimbo gani wa huzuni wenye Daudi alitunga kwa ajili ya Sauli na Yonatani?
Juu ya nini Daudi hakufurahi wakati Sauli alikufa?