MAISHA YA MUKRISTO
Ukuwe na Imani Kama Unaweza Kupambana na Magumu ya Kupata Makuta
Maisha iko nguvu sana mu hizi siku za mwisho. Kwa kweli, kadiri tunakaribia mwisho wa hii dunia, magumu itaongezeka. Wakati fulani tunaweza kukosa mambo fulani yenye tuko nayo lazima. (Hab 3:16-18) Ni nini itatusaidia tukuwe na imani kama tunaweza kupambana na magumu ya kupata makuta? Tunapaswa kuendelea kumutumainia Mungu wetu, Yehova. Alitoa ahadi ya kuhangaikia watumishi wake, na anaweza kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima hata tukuwe mu hali gani.—Zb 37:18, 19; Ebr 13:5, 6.
Mambo yenye unaweza kufanya:
Omba Yehova akuongoze, akupatie hekima, na akutegemeze.—Zb 62:8
Ukuwe tayari kuitika kufanya kazi yenye pengine hauyafanyaka.—g-SW 1/10 uku. 8-9, visanduku
Endelea kufanya mambo ya kiroho, kutia ndani kusoma Neno ya Mungu kila siku, kukusanyika kwa ukawaida, na kuhubiri
MUANGALIE VIDEO JENGA NYUMBA YENYE HAITABOMOKA—“MUTOSHEKE NA VITU VYA SASA,” NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Ni magumu gani yenye familia fulani zilipambana nayo?
Ni jambo gani njo ya maana zaidi mu maisha?
Namna gani tunaweza kusaidia wale wenye kuwa na magumu ya kupata makuta?