Tuige Mufano wa Manabii—Habakuki
1. Sababu gani tunaweza kujisikia kama nabii Habakuki?
1 Mambo mabaya yanaendelea kuongezeka katika ulimwengu huu. Tunaweza kujisikia sawa vile nabii Habakuki alijisikia wakati tunaona mambo mabaya; alimuuliza Yehova hivi: ‘Kwa nini unanionyesha jambo lenye kuzuru, nawe unaendelea kutazama taabu?’ (Hab. 1:3; 2 Tim. 3:1, 13) Kufikiri sana juu ya ujumbe wa Habakuki kunaweza kutusaidia kuendelea kungojea siku ya hukumu ya Yehova pasipo kuchoka.—2 Pet. 3:7.
2. Namna gani leo tunaweza kuonyesha kwamba tunaishi kwa imani?
2 Kuishi kwa Uaminifu: Kuliko kuvunjika moyo, Habakuki aliendelea kuwa macho kiroho na kumutumikia Yehova. (Hab. 2:1) Yehova alimuhakikishia nabii Habakuki kwamba neno Lake litatimia kwa wakati wenye kufaa na mutu “mwadilifu [mwenye kutenda haki], ataendelea kuishi kwa uaminifu wake.” (Hab. 2:2-4) Hilo linamaanisha nini kwa Wakristo wenye wanaishi katika mwisho wa siku za mwisho? Jambo la maana sana haiko kujua wakati gani mwisho utafika, lakini ni kuamini kabisa kwamba mwisho utafika. Imani inatuchochea tuendelee kuwa macho na kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza.—Ebr. 10:38, 39.
3. Sababu gani tunapaswa kulinda furaha yetu wakati tunamutumikia Yehova?
3 Kufurahi Katika Yehova: Wakati Gogu wa Magogu atashambulia watu wa Yehova, imani yetu itajaribiwa. (Eze. 38:2, 10-12) Vita inatokeza mateso hata kwa watu wenye wanapata ushindi. Pengine chakula kitakosekana, pengine tutapoteza vitu vyetu, na pengine hali ya maisha itakuwa mubaya zaidi. Tutafanya nini wakati magumu hayo yatatokea? Habakuki alifikiria mbele ya wakati mambo hayo, kwa hiyo aliamua kuendelea kulinda furaha yake ya kumutumikia Yehova. (Hab. 3:16-19) “Shangwe [furaha] ya Yehova” itatusaidia pia kuvumilia magumu yenye itatokea wakati unaokuja.—Neh. 8:10; Ebr. 12:2.
4. Tunaweza kupata furaha gani leo na pia wakati unaokuja?
4 Wale wenye Yehova atalinda katika siku yake ya hukumu yenye kuja wataendelea kujifunza kufanya mapenzi yake. (Hab. 2:14) Wenye watafufuliwa watajifunza pia kumujua Yehova. Leo, tunatumia kila nafasi ili kuzungumuza juu ya Yehova na kazi zake za ajabu!—Zab. 34:1; 71:17.