Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb23 Mwezi wa 3 uku. 3
  • Tunaweza Kusaidia Namna Gani Kisha Musiba?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tunaweza Kusaidia Namna Gani Kisha Musiba?
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mashahidi wa Yehova Wanasaidiaka Wale Wenye Wanafikiwa na Misiba?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Namna Gani Tunaweza Kusaidia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
mwb23 Mwezi wa 3 uku. 3

MAISHA YA MUKRISTO

Tunaweza Kusaidia Namna Gani Kisha Musiba?

Leo, misiba ya asili inaendelea kuongezeka. Ndugu wanapangaka muzuri na kusimamia muzuri kazi ya kutoa misaada. Njo maana Baraza Yenye Kuongoza imeweka Idara ya Kutoa Misaada mu kila tawi.

Wakati ndugu wenye kutumika mu ile idara wanapata habari kama kumetokea musiba mu eneo fulani, mara moya wanapashana habari na wazee wa mu ile eneo juu ya kujua wahubiri wako na lazima ya musaada gani. Kama kulikuwa uharibifu mukubwa, na wahubiri hawataweza kuushugulikia wao wenyewe, tawi itaweka ndugu wenye uzoefu juu wasimamie kazi ya kutoa misaada. Wale ndugu wanaweza kuomba ndugu na dada wajitolee ili kusaidia ao wanaweza kuwaomba watoe vitu fulani, ao tena wanaweza kuuza vile vitu mu eneo na kuvigabulia wenye kuwa na lazima ya musaada.

Kuko faida mingi ya kushugulikia mambo mu ile njia. Ile inafanya tusichoke bure, kusikuwe muvurugo, na tusipoteze makuta na vitu; mambo yenye inatokeaka kama kila mutu anaamua kufanya mambo yeye peke.

Ndugu wenye walichaguliwa na tawi wanaweza kuamua ni feza ngapi na ni wajitoleaji ngapi watahitajiwa mu kazi ya kutoa misaada. Wanaweza pia kupashana habari na wakubwa wa serikali wa mu eneo, juu mara mingi wanasaidiaka ili kazi ya kutoa misaada iende mbio. Kwa hiyo, mutu hapaswe kukamata mipango yeye mwenyewe ya kukusanya michango, kutuma misaada, ao kuenda fasi kwenye kulitokea musiba kama hakuombwa kufanya vile.

Lakini, wakati musiba unatokea, tunapendaka kusaidia. (Ebr 13:16) Tunapenda ndugu zetu! Sasa tunaweza kufanya nini? Jambo ya maana zaidi yenye tunaweza kufanya, ni kusali kwa ajili ya wale wenye walipatwa na musiba na wale wenye kuwatolea misaada. Tunaweza pia kutoa michango kwa ajili ya kazi ya mu dunia yote. Chini ya muongozo wa Baraza Yenye Kuongoza, biro za tawi njo zinajua muzuri ni wapi na ni namna gani ile michango itasaidia zaidi. Na kama tunapenda kuenda kusaidia, tunaweza kuonyesha vile kwa kujaza fomu Demande d’Admission Comme Volontaire Local de Développement-construction (DC-50).

MUANGALIE VIDEO MVUA YENYE MAJI MINGI KATIKA BRAZILI, KISHA MUJIBIE ULIZO YENYE KUFUATA:

Picha yenye kutoka mu video “Mvua Yenye Maji Mingi Katika Brazili.” Picha yenye ilikamatwa juu yenye kuonyesha nyumba na miti yenye inakaribia kuzama mu eneo yenye kuyala maji.

Nini njo inakushangaza kuhusu kazi ya kutoa misaada yenye Mashahidi wa Yehova walifanya kisha mvua yenye maji mingi yenye ilitokea Brazili mu 2020?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine