Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/05 uku. 5
  • Namna Gani Tunaweza Kusaidia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Gani Tunaweza Kusaidia?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mashahidi wa Yehova Wanasaidiaka Wale Wenye Wanafikiwa na Misiba?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • “Zawadi kwa Ajili ya Yehova”
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Kazi ya Kutolea Ndugu Misaada Wakati wa Magumu
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Tunaweza Kusaidia Namna Gani Kisha Musiba?
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 11/05 uku. 5

Namna Gani Tunaweza Kusaidia?

1 Ulizo “Namna gani tunaweza kusaidia?” linatokezwa mara nyingi na Mashahidi wa Yehova wanaposikia habari juu ya msiba ambao umetukia sehemu fulani ya ulimwengu. Kama vile simulizi kwenye andiko la Matendo 11:27-30 linavyoonyesha, Wakristo katika karne ya kwanza walitoa msaada kwa ndugu ambao walikaa katika Yudea kwa sababu ya njaa iliyotukia.

2 Nyakati za kisasa, sheria zinazohalalisha tengenezo letu zimeruhusu fedha zitumiwe kwa ajili ya utendaji wa kutoa misaada ya kifadhili kwa wale wenye kuteseka kutokana na misiba ya asili au yenye kusababishwa na watu na pia wakati misaada mingine inapohitajiwa.

3 Kwa mfano, mwaka uliopita ndugu wengi walitoa michango ili kusaidia wale waliopatwa na msiba wa tsunami katika Asia ya Kusini. Itikio hilo lenye kutoka moyoni la kutuma michango ya kifedha katika hazina ya msaada wa kitulizo wa tengenezo lilithaminiwa sana. Hata hivyo, michango ya kifedha inapotumwa kwa ajili ya msiba fulani tu, katika nchi nyingine sheria inaomba kutumia fedha hizo kwa ajili tu ya kusudi lililoonyeshwa wazi na mtoaji na hilo katika kipindi cha wakati fulani, iwe kwamba mahitaji ya ndugu zetu yameshughulikiwa mahali kwao au sivyo.

4 Kwa sababu hiyo, inapendekezwa kwamba michango ya kifedha kwa ajili ya misaada ya kitulizo na ya kifadhili itolewe kwa kazi ya ulimwenguni pote. Fedha hizo zinatumiwa kwa ajili ya jitihada zenye kufanywa ili kutoa misaada na pia kwa ajili ya kuendeleza mahitaji ya kiroho ya undugu wa Kikristo. Ikiwa, kwa sababu fulani, mtu anataka kutoa mchango wa kifedha kwa ajili ya msaada wa kitulizo tu tofauti na michango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote, mchango huo utakubaliwa na kutumiwa mahali popote ambako msaada wa kitulizo unahitajiwa. Lakini, lingekuwa jambo lenye kufaa ikiwa michango kama hiyo ingefanywa bila kuonyesha mahali na jinsi fedha hizo zinaweza kutumiwa.

5 Kutoa michango ya kifedha kwanza kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote kunafanya fedha zipatikane zaidi ili kuzitumia kuhusiana na sehemu zote za kazi ya Ufalme badala ya kuzilinda tu kwa ajili ya misaada ya kitulizo ya wakati ujao. Jambo hilo linapatana na wazo la Waefeso 4:16, kwamba tufanye kazi pamoja ili kutoa kile kinachohitajiwa ‘ili kutokeza ukuzi wa mwili ili huo ujijenge wenyewe katika upendo.’

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine