Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb23 Mwezi wa 5 uku. 3
  • Ujione Vile Yehova Anakuona

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ujione Vile Yehova Anakuona
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maamuzi Yenye Inaonyesha Kama Tunamutegemea Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Itika Kama Yehova Anakupenda
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Yehova “Anaponyesha Wenye Kuvunjika Moyo”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
mwb23 Mwezi wa 5 uku. 3

MAISHA YA MUKRISTO

Ujione Vile Yehova Anakuona

“Yehova anafurahia watu wake.” (Zb 149:4) Hata kama hatukamilike, Yehova anaonaka sifa zetu za muzuri na mambo ya muzuri yenye tunaweza kufikia kufanya. Lakini, wakati fulani inaweza kuwa nguvu kwetu kuona sifa za muzuri zenye tuko nazo. Wakati fulani, tunaweza kujiona kuwa hatuko wa maana kwa sababu ya namna watu wanatutendea. Ao kama tunakazia akili makosa yetu ya zamani, tunaweza kushakia kama Yehova anatupenda. Nini inaweza kutusaidia ikiwa tuko na mawazo ya vile?

Kumbuka kama Yehova anaonaka mambo yenye wanadamu hawawezi kuona. (1Sa 16:7) Ile inamaanisha kama Yehova anaonaka mambo yenye hata siye wenyewe hatuonake ndani yetu. Tuko wenye shukrani kwa sababu Biblia inatusaidia kuelewa namna Yehova anatuonaka. Tunaelewa ile wakati tunasoma maandiko na habari za Biblia zenye kuonyesha namna Yehova anapenda watu wake.

MUANGALIE VIDEO HAKIKISHIA MOYO WAKO MBELE YA YEHOVA, NA KISHA MUJIBIE MAULIZO YENYE KUFUATA:

  • Mufano wa ule kijana mwenye kukimbia na baba yake unatufundisha nini juu ya namna Yehova anatuona?

  • Kama mutu mwenye amefanya zambi nzito amekamata hatua zote zenye zinaombwa juu ya kurudisha urafiki wake na Yehova, namna gani anaweza kuhakikishia moyo wake mbele ya Yehova?​—1Yo 3:19, 20

  • Namna gani kusoma na kufikiri sana juu ya habari ya Daudi na ya Yehoshafati kulimusaidia ule ndugu?

Habari za Biblia zenye zinatuhakikishia kama . . .

Yehova anatupenda hata wengine watuone namna gani

  • Enoko (Mwa 5:24; Ebr 11:5; Yud 14, 15)

  • Hana (1Sa 1:1–2:11, 18-21, 26)

Yehova anasamehe kabisa watenda-zambi wenye kutubu

  • Manase (2Ny 33:1-7, 12, 13)

  • Paulo (1Ti 1:12-16)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine