Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 8 uku. 8-13
  • Itika Kama Yehova Anakupenda

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Itika Kama Yehova Anakupenda
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA TUKUWE HAKIKA KAMA YEHOVA ANATUPENDA?
  • NINI NJO ITATUSAIDIA TUKUWE HAKIKA KAMA YEHOVA ANATUPENDA?
  • NAMNA YESU ANATUSAIDIA KUWA HAKIKA KAMA YEHOVA ANATUPENDA
  • FANYA YAKO YOTE JUU UENDELEE KUWA HAKIKA KAMA YEHOVA ANAKUPENDA
  • Yehova Anakupenda Sana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Bei ya Ukombozi Inatufundisha Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Upendo wa Mungu Ni wa Milele
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 8 uku. 8-13

HABARI YA KUJIFUNZA YA 33

WIMBO 4 “Yehova Ni Muchungaji Wangu”

Itika Kama Yehova Anakupenda

“Nimekuvuta kwangu kwa upendo mushikamanifu.”—YER. 31:3.

WAZO KUBWA

Juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama Yehova anatupenda na mambo yenye tunaweza kufanya juu tuendelee kuwa hakika na ile jambo.

1. Juu ya nini ulijitoa kwa Yehova? (Ona pia picha.)

UNAKUMBUKA siku ulijitoa kwa Yehova? Ulikamata ule uamuzi juu ulifikia kumujua na kumupenda. Ulimuahidi kama utatia mapenzi yake fasi ya kwanza mu maisha yako na utaendelea kumupenda kwa moyo wako wote, nafsi yako yote, akili yako yote, na nguvu yako yote. (Mk. 12:30) Kuanzia pale upendo wako kwa Yehova umeendelea kuongezeka. Sasa utajibu namna gani kama mutu anakuuliza: “Uko hakika kama unamupenda Yehova?” Inawezekana utajibu palepale: “Namupenda sana kupita byote!”

Picha: Dada iko nafikiria namna alijitoa kwa Yehova na kubatizwa. 1. Anaikala inje na iko nasali. 2. Anabatizwa mu mutoni.

Unakumbuka vile ulikuwa namupenda Yehova sana wakati ulijitoa kwake na kubatizwa? (Ona fungu ya 1)


2-3. Yehova anapenda tukuwe hakika na nini, na tutazungumuzia nini mu hii habari? (Yeremia 31:3)

2 Utajibu sasa namna gani kama mutu anakuuliza: “Uko hakika kama Yehova anakupenda?” Pengine itakuwa nguvu kwako kujibu palepale. Unaweza kuanza kuwaza kama haustahili upendo wa Yehova. Dada moya mwenye alikomala mu hali ya nguvu alisema hivi: “Ninajua kama ninamupenda Yehova, niko hakika na ile jambo. Lakini mara mingi sikuwake hakika kama Yehova ananipenda. Sasa nini njo itakusaidia kujua kama Yehova anakupenda kabisa?

3 Yehova anapenda ukuwe hakika kama anakupenda. (Soma Yeremia 31:3.) Kusema kweli, ni Yehova njo alikuvuta kwake. Na wakati ulijitoa kwake na kubatizwa alianza kukuonyesha upendo wa pekee sana, upendo mushikamanifu. Ni kusema anakupenda sana na hatakuacha hata siku moya. Ile upendo inafanya aone batumishi yake bote baaminifu kuwa “mali yenye kupendwa sana,” ni kusema ni vile anakuona na weye. (Mal. 3:17, maelezo ya chini) Yehova anapenda ukuwe hakika kama anakupenda, sawa tu vile mutume Paulo alikuwa hakika kama Yehova anamupenda. Njo maana Paulo aliandika hivi: “Kwa maana nimesadiki kwamba ikuwe kifo ao uzima ao malaika ao serikali ao mambo yenye kuwa sasa ao mambo yenye yatakuja ao nguvu ao urefu kuenda juu ao urefu kuenda chini ao uumbaji mwingine wowote havitaweza kututenganisha na upendo wa Mungu.” (Ro. 8:38, 39) Mu hii habari tutaona juu ya nini ni jambo ya maana tukuwe hakika kama Yehova anatupenda, na tutaona mambo yenye tunaweza kufanya juu tukuwe hakika na ile jambo.

JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA TUKUWE HAKIKA KAMA YEHOVA ANATUPENDA?

4. Tunaweza kufanya nini juu ya kupinga Shetani?

4 Kama tuko hakika kama Yehova anatupenda, tutaweza kupiganisha moya kati ya “matendo ya ujanja” ya Shetani. (Efe. 6:11) Shetani atafanya yake yote juu tumuache Yehova. Njia moya yenye anatumikishaka ni kutuchochea tuamini kama Yehova hatupendi. Lakini tusisaabu kama Shetani ni mujanja, anatafutaka wakati tuko zaifu juu atushambulie; pengine wakati tunavunjika moyo juu ya mambo yenye ilitufikiaka zamani, juu ya magumu yenye tuko nayo leo, ao juu hatujue mambo yenye itatokea kesho. (Mez. 24:10) Shetani iko sawa simba mwenye iko natafuta kukamata munyama mwenye iko zaifu. Njo maana anajaribu kutuchochea tuache kumutumikia Yehova wakati tunavunjika moyo. Lakini tukiendelea kuwa hakika kama Yehova anatupenda tutaweza ‘kumupinga’ Shetani na matendo yake ya ujanja.—1 Pe. 5:8, 9; Yak. 4:7.

5. Juu ya nini ni jambo ya maana tujue kama Yehova anatupenda?

5 Kama tunaitika kama Yehova anatupenda tutamukaribia. Juu ya nini tunasema vile? Banadamu banakuwa na lazima ya kupenda bengine na banakuwaka na lazima bengine babapende. Ni vile Yehova alituumbaka. Kama mutu anatupenda na siye tunamupendaka tu. Kwa hiyo, wakati tunakubali kama Yehova anatupenda na siye tutamupenda. (1 Yo. 4:19) Na wakati tunamupenda sana, ni vile naye atatupenda sana. Biblia inasema: “Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yak. 4:8) Sasa nini njo itatusaidia tukuwe hakika kama Yehova anatupenda?

NINI NJO ITATUSAIDIA TUKUWE HAKIKA KAMA YEHOVA ANATUPENDA?

6. Kama hauko hakika kama Yehova anakupenda unaweza kufanya nini?

6 Ukuwe wazi mu sala zako. (Lu. 18:1; Ro. 12:12) Umuombe Yehova akusaidie ujione vile yeye anakuona. Ikiwezekana ufanye vile mara mingi kila siku. Kusema kweli, kama moyo wako uko nakuhukumu, haiko mwepesi kuamini kama Yehova anakupenda. Lakini kumbuka kama Yehova ni mukubwa kupita moyo wako. (1 Yo. 3:19, 20) Anakujua muzuri kupita vile weye unajijua, anaona mu moyo wako mambo yenye pengine weye hauwezi kuona. (1 Sa. 16:7; 2 Ny. 6:30) Kwa hiyo usijizuie, ‘umumwangie’ moyo wako, umuombe akusaidie uitike kama anakupenda. (Zb. 62:8) Kisha utende kulingana na sala zako kwa kufanya mambo yenye kufuata.

7-8. Namna gani maandiko yenye kuwa mu Zaburi inatuhakikishia kama Yehova anatupenda?

7 Amini mambo yenye Yehova anasema. Yehova aliongoza benye baliandika Biblia baandike namna anakuwaka kabisa. Kwa mufano, fikiria mambo yenye Daudi alisema juu ya Yehova. Alisema hivi: “Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo; anaokoa wale wenye kuvunjika moyo.” (Zb. 34:18, maelezo ya chini) Wakati unavunjika moyo unaweza kuwaza kama uko weye peke, lakini Yehova anaahidi kama wakati ya vile iko karibu na weye juu anajua kama uko na lazima yake sana mu ile wakati. Daudi aliandika hivi mu Zaburi ingine: “Kusanya machozi yangu katika chupa yako ya ngozi.” (Zb. 56:8) Ni kusema Yehova anaona wakati uko na maumivu na huzuni. Anakuhangaikia sana na anasikia mubaya sana kuona uko napitia mu hali za nguvu. Sawa vile kila tone ya mayi ni ya maana kwa mutu mwenye iko nasafiri mu jangwa, machozi yenye unamwanga ni ya maana kwa Yehova na anaona kila wakati unaumia na kulia. Zaburi 139:3, inasema: “[Yehova] unajua njia zangu zote.” (Ebr. 6:10) Kwa kweli, Yehova anajua njia zako zote, lakini anakazia akili mambo ya muzuri yenye unafanya. Juu ya nini? Juu anafurahia sana mambo yote yenye uko najikaza kufanya ili kumufurahisha.a

8 Kupitia ile maandiko yote yenye kufariji yenye iko mu Biblia, ni sawa vile Yehova anakuambia hivi: “Ninapenda ujue kama ninakupenda sana, na ninakuhangaikia sana.” Lakini sawa vile tuliona, Shetani ni muongo na anapenda uwaze kama Yehova hakupendi. Kwa hiyo kama wakati fulani unajiuliza ikiwa Yehova anakupenda, waza kidogo na ujiulize hivi: ‘Nitaamini nani? “Baba ya uongo” ao “Mungu wa ukweli”?’—Yoh. 8:44; Zb. 31:5.

9. Yehova anahakikishia nini benye banamupenda? (Kutoka 20:5, 6)

9 Fikiria namna Yehova anaona bale wenye banamupenda. Fikiria mambo yenye Yehova aliambia Musa na Baisraeli. (Soma Kutoka 20:5, 6.) Aliahidi kama ataendelea kuonyesha upendo mushikamanifu benye wanamupenda. Ile maneno inatuhakikishia kama haiwezekane Yehova akose kupenda batumishi yake benye banamupenda. (Ne. 1:5) Kwa hiyo kama wakati fulani uko na lazima ya kuwa hakika kama Yehova anakupenda, ujiulize hivi: ‘Ninamupenda Yehova?’ Kama unamupenda Yehova na uko najikaza sana kumufurahisha ukuwe hakika kama naye anakupenda sana. (Da. 9:4; 1 Ko. 8:3) Mu maneno ingine tunaweza kusema hivi: Kama uko hakika kama unamupenda Yehova, juu ya nini usikuwe hakika kama yeye anakupenda? Kila siku ukuwe hakika kama Yehova anakupenda na hatakuacha hata siku moya.

10-11. Yehova anapenda uone bei ya ukombozi namna gani? (Wagalatia 2:20)

10 Fikiri sana juu ya bei ya ukombozi. Zabihu ya bei ya ukombozi yenye Yesu alitoa njo zawadi ya mukubwa sana yenye Yehova amepatia banadamu. (Yoh. 3:16) Ni zawadi yenye Yehova alikupatia weye kipekee? Ndiyo! Fikiria mufano wa mutume Paulo. Kumbuka kama mbele akuwe Mukristo alifanya makosa makubwa-makubwa, na pia alipaswa kuendelea kupiganisha uzaifu wake. (Ro. 7:24, 25; 1 Ti. 1:12-14) Lakini kisha kuwa Mukristo, aliona bei ya ukombozi kuwa zawadi yenye Yehova alimupatia yeye kipekee. (Soma Wagalatia 2:20.) Kumbuka kama Yehova alimuongoza Paulo aandike juu ya ile mambo mu Neno yake Biblia, na mambo yote yenye iko mu Biblia iko pale juu ya kutufundisha. (Ro. 15:4) Maneno ya Paulo inaonyesha namna Yehova anapenda uone bei ya ukombozi, anapenda uione kuwa zawadi yenye alikupatia weye. Wakati unaiona vile, unakuwa hakika zaidi kama Yehova anakupenda weye kipekee.

11 Tunamushukuru sana Yehova juu alituma Yesu ku dunia akufe kwa ajili yetu. Lakini kuko sababu ingine yenye ilifanya Yesu akuye hapa ku dunia, alikuya kutufundisha kweli juu ya Mungu. (Yoh. 18:37) Na kati ya kweli zenye Yesu alifundisha, alionyesha kama Yehova anatupenda sana.

NAMNA YESU ANATUSAIDIA KUWA HAKIKA KAMA YEHOVA ANATUPENDA

12. Juu ya nini tunaweza kuamini mambo yenye Yesu alisema juu ya Yehova?

12 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alifurahia kuelezea batu namna Yehova anakuwaka. (Lu. 10:22) Tunaweza kuamini mambo yenye Yesu alisema juu ya Yehova. Juu ya nini? Juu Yesu aliishi wakati murefu sana pamoya na Yehova mbele akuye ku dunia. (Kol. 1:15) Yesu amejionea namna Yehova anapenda sana batoto yake baaminifu ikuwe mbinguni ao ku dunia. Namna gani Yesu alisaidia bengine bakuwe hakika kama Yehova anabapenda?

13. Yesu anapenda tumuone Yehova namna gani?

13 Yesu anapenda tumuone Yehova vile yeye anamuona. Mu vitabu vya Injili, Yesu alimuita Yehova “Baba” zaidi ya mara 160. Na wakati alikuwa nazungumuza na banafunzi yake alikuwa natumia maneno sawa vile “Baba yenu” ao “Baba yenu wa mbinguni.” (Mt. 5:16; 6:26) Mbele Yesu akuye ku dunia batumishi baaminifu balizoea kumuita Yehova majina sawa vile ‘Mweza-yote,’ ‘Mwenye kuwa juu zaidi,’ ‘Muumbaji Mukubwa,’ na majina ingine ya cheo. Lakini Yesu yeye mara mingi alimuita Yehova ‘Baba.’ Kumuita Yehova Baba inaonyesha kama Yehova anapenda batumishi yake bajisikie kuwa karibu naye sawa vile mutoto anajisikiaka kuwa karibu na baba yake mwenye upendo. Ni wazi kama Yesu anapenda tumuone Yehova vile yeye anamuona, tumuone kuwa Baba yetu mwenye upendo, mwenye anapenda sana batoto yake. Tuzungumuzie mifano mbili kwenye Yesu anatumia neno “Baba.”

14. Namna gani Yesu alionyesha kama kila mumoya wetu ni wa maana sana kwa Baba yetu Yehova? (Matayo 10:29-31) (Ona pia picha.)

14 Kwanza, tuzungumuzie maneno ya Yesu yenye iko mu Matayo 10:29-31. (Soma.) Shomoro ni tundege twa kidogo-kidogo twenye hatutamutumikiaka Yehova wala kumupenda. Lakini, Baba yetu Yehova anaona tule tundege kuwa twa maana sana mupaka hata kamoya kakianguka anajua. Kama Yehova anaona ka ndege ka kidogo vile kuwa ka maana, tunaweza kuwa hakika kama anahangaikia sana kila mumoya wetu juu tunamupenda na kumuabudu. Yesu alisema pia kama Baba yetu anajua hesabu ya nywele zenye kila mutu iko nazo ku kichwa. Juu Yehova anajua hata mambo ya kidogo-kidogo juu yetu, tunaweza kuwa hakika kama anatuhangaikia sana. Kwa kweli, Yesu anapenda tukuwe hakika kama kila mumoya wetu ni wa maana sana kwa Baba yetu wa mbinguni.

Yesu anaonyesha ndege shomoro mwenye iko nashuka ku udongo. Banafunzi yake banamusikiliza kwa uangalifu.

Yehova anaona shomoro moya kuwa ya maana sana mupaka anajuaka saa inaanguka. Kama Yehova anaona kandege ka kidogo vile kuwa ka maana, ukuwe hakika kama anakuhangaikia juu unamupenda na kumuabudu! (Ona fungu ya 14)


15. Maneno ya Yesu yenye iko mu Yohana 6:44 inakufundisha nini juu ya Baba yako wa mbinguni?

15 Tuone mufano wa pili kwenye Yesu anatumikisha neno “Baba.” (Soma Yohana 6:44.) Baba yetu wa mbinguni yeye peke njo alikuvuta kwake juu ujifunze kweli. Juu ya nini alikuvuta kwake? Juu aliona kama uko na moyo wa muzuri. (Mdo. 13:48) Wakati Yesu alitaya maneno yenye iko mu Yohana 6:44 pengine alikuwa nazungumuzia maneno ya Yehova yenye iko mu Yeremia 31:3. Mu ile andiko Yehova anaambia hivi batu yake: “Nimekuvuta kwangu kwa upendo mushikamanifu [ao nimeendelea kukuonyesha upendo mushikamanifu].” (Linganisha na Hosea 11:4.) Fikiria maana ya ile maneno, Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo anaendelea kuona mambo ya muzuri mu moyo wako yenye pengine weye hauwezi kuona.

16. (a)  Wakati Yesu anamuita Yehova Baba yetu, anapenda kutufundisha nini na juu ya nini tunapaswa kumuamini? (b) Nini njo inaweza kukusaidia kuwa hakika kama Yehova njo Baba muzuri? (Ona kisanduku “Baba Ambaye Sote Tunamhitaji.”)

16 Wakati Yesu alimuita Yehova Baba yetu ni sawa vile alikuwa nasema: “Yehova haiko Baba yangu miye peke ni Baba yako na weye, na ninakuhakikishia kama anakupenda na anakuhangaikia sana.” Kwa hiyo kama wakati fulani hauko hakika kama Yehova anakupenda, kumbuka mambo yenye Yesu alisema na uiamini juu Yesu anasemaka tu kweli na anamujua Yehova muzuri sana.’—1 Pe. 2:22.

“Baba Ambaye Sote Tunamhitaji”

Ile maneno inapatikana mu utangulizi ya kitabu Mkaribie Yehova. Inasema hivi juu ya kusudi ya kile kitabu: “Tutaona kwamba Yehova ndiye . . . Baba ambaye sote tunamhitaji. Akiwa mwenye nguvu, haki, hekima, na mwenye upendo, yeye hawaachi kamwe watoto wake waaminifu.”

Dada moya mwenye baba yake alikuwa natendea mubaya anafasiria namna ile kitabu ilimusaidia, anasema hivi: “Ilinifundisha kama neno baba haiko ya kuogopa, ninaelewa sasa namna baba muzuri anakuwaka. Najua kama Yehova ananikubali na miye ninamukubali kuwa Baba yangu.” Kisha kusoma ile kitabu, dada mwingine alisema hivi: “Kama kuko baba muzuri sana ni Yehova, hakuna mwingine!”

Juu ukuwe hakika kama Yehova njo Baba mwenye uko naye lazima, hauone kama ni muzuri kusoma ao kusoma tena ile kitabu?

FANYA YAKO YOTE JUU UENDELEE KUWA HAKIKA KAMA YEHOVA ANAKUPENDA

17. Juu ya nini tunapaswa kuendelea kufanya yetu yote juu tukuwe hakika kama Yehova anatupenda?

17 Ni jambo ya maana tuendelee kufanya yetu yote juu tukuwe hakika kama Yehova anatupenda. Sawa vile tuliona, Shetani adui yetu ni mujanja na ataendelea kufanya yake yote juu tuache kumutumikia Yehova. Juu anapenda tukuwe zaifu, ataendelea kutuchochea tuwaze kama Yehova hatupendi. Hatupaswe kuamini ile bongo ya Shetani.—Yob. 27:5.

18. Unaweza kufanya mambo gani juu ukuwe hakika kama Yehova anakupenda?

18 Juu uendelee kuwa hakika kama Yehova anakupenda, uendelee kusali akusaidie ujione vile yeye anakuona. Fikiria mambo yenye baandikaji ba Biblia balisema juu ya upendo wake. Fikiria namna Yehova anaona batumishi yake benye banamupenda, haiwezekane tumupende kisha yeye ashindwe kutupenda. Fikiria juu ya nini ni muzuri uone bei ya ukombozi kuwa zawadi yenye Mungu alikupatia weye kipekee. Na uamini kama Yehova ni Baba yako, vile tu Yesu alisema. Kisha kama mutu anakuuliza: “Uko hakika kama Yehova anakupenda?” Utajibu hivi kwa uhakika: “Ndiyo ananipenda na niko nafanya yangu yote juu ya kumuonyesha kama na miye namupenda.”

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama Yehova anatupenda?

  • Nini njo inatusaidia kuwa hakika kama Yehova anatupenda?

  • Namna gani Yesu anatusaidia tuitike kama Yehova anatupenda?

WIMBO 154 Upendo Haushindwe

a Juu ya kupata maandiko ingine yenye inahakikisha kama Yehova anatupenda ona sehemu “Mashaka” mu kitabu Maandiko ya Kutusaidia mu Maisha ya Kikristo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine