Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 10 uku. 12-17
  • Upendo wa Mungu Ni wa Milele

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Upendo wa Mungu Ni wa Milele
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • UONE UPENDO WA YEHOVA KUWA FUNDISHO YA MUSINGI
  • FIKIRI SANA JUU YA NAMNA YEHOVA ‘ANAKUPENDA’
  • UELEWE JUU YA NINI UKO NA MASHAKA
  • ENDELEA KUWA MUSHIKAMANIFU
  • Yehova Anakupenda Sana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Itika Kama Yehova Anakupenda
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Namna ya Kupiganisha Mashaka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Upendo Mushikamanifu wa Yehova Uko na Faida Gani Kwako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 10 uku. 12-17

HABARI YA KUJIFUNZA YA 41

WIMBO 108 Mungu Iko na Upendo Mushikamanifu

Upendo wa Mungu Ni wa Milele

“Mumushukuru Yehova, kwa maana ni mwema;upendo wake mushikamanifu unadumu milele.”—ZB. 136:1.

WAZO KUBWA

Kukumbuka kama upendo wa Yehova ni fundisho ya musingi kunaweza kututia moyo wakati tuko na magumu.

1-2. Bakristo ba mingi biko napambana na hali gani?

WAZIA mashua iko katikati ya bahari na kuko upepo mukali. Ule upepo uko nasukuma-sukuma mashua huku na huku. Ile mashua itaenda kote kwenye upepo unaibeba. Lakini juu ile mashua isiyumbe-yumbe, itaomba mutu atie nanga. Nanga itasaidia mashua ibakie fasi moya, na isiende kwenye haingepaswa kuenda.

2 Wakati uko napambana na magumu, unaweza kuwa sawa vile ile mashua. Unaweza jisikia muzuri saa moya kisha saa ingine unajisikia tena mubaya. Iko sawa vile upepo uko nakubeba huku na huku. Leo uko hakika kama Yehova anakupenda na anakutegemeza, kisha kesho unaanza jiuliza kama Yehova iko naona kabisa mambo yenye uko napitia. (Zb. 10:1; 13:1) Pengine rafiki yako anakutia moyo na unajisikia muzuri kwa wakati fulani. (Mez. 17:17; 25:11) Kisha tena mashaka inarudia. Unaweza hata kuanza kuwaza kama Yehova alishakuacha. Namna gani unaweza kutia nanga mu njia ya mufano wakati uko mu hali ya vile? Ao mu maneno ingine, namna gani unaweza kuwa hakika na kuendelea kuwa hakika kama Yehova anakupenda na kukutegemeza?

3. (a) Maneno “upendo mushikamanifu” yenye kuzungumuziwa mu Zaburi 31:7 na 136:1 maana yake nini? (b) Juu ya nini tunasema kama Yehova njo mufano muzuri zaidi wa upendo mushikamanifu? (Ona pia picha.)

3 Jambo moya yenye inaweza kutusaidia tusibebwe huku na huku wakati tuko na magumu, ni kukumbuka upendo mushikamanifu wa Yehova. (Soma Zaburi 31:7; 136:1.) Maneno “upendo mushikamanifu” inaleta wazo ya mutu kuendelea kushikamana sana na mwingine. Yehova njo mufano mukubwa zaidi wa upendo mushikamanifu. Na hata, Biblia inasema kama iko na “upendo mwingi mushikamanifu.” (Kut. 34:6, 7) Biblia inasema tena hivi juu ya Yehova: “Uko na upendo mwingi mushikamanifu kwa ajili ya wale wote wenye wanakuitia.” (Zb. 86:5) Pima kufikiria maana ya ile maneno: Yehova haachake hata kidogo batumishi yake baaminifu! Kukumbuka kama Yehova ni mushikamanifu kunaweza kukusaidia usiyumbe-yumbe wakati uko napambana na magumu.—Zb. 23:4.

Nanga inatupwa mu mayi juu ya kusaidia mashua isibebwe na upepo.

Sawa vile nanga inasaidiaka upepo isibebe mashua wakati wa zoruba, kuwa hakika kama Yehova anatupenda kunatusaidia tusibebwe huku na huku wakati tuko na magumu (Ona fungu ya 3)


UONE UPENDO WA YEHOVA KUWA FUNDISHO YA MUSINGI

4. Taya mafundisho fulani ya musingi ya Biblia, na ufasirie juu ya nini tunaiamini kabisa.

4 Jambo ingine yenye inaweza kutusaidia tusibebwe huku na huku wakati tuko na magumu, ni kukumbuka kama upendo wa Yehova ni fundisho ya musingi ya Biblia. Saa unasikia maneno “fundisho ya musingi ya Biblia” nini njo inakukuya mu akili? Pengine unafikiria mafundisho ya kweli yenye umejifunza mu Biblia. Kwa mufano, umejifunza kama jina ya Mungu ni Yehova, Mwana wa pekee wa Mungu ni Yesu, wafu hawajue kitu, na wanadamu wataishi milele mu paradiso ku dunia. (Zb. 83:18; Muh. 9:5; Yoh. 3:16; Ufu. 21:3, 4) Wakati ulijifunza ile mambo, uliiamini kabisa. Juu ya nini? Juu ulielewa kama iko na musingi wa kweli. Tuzungumuzie sasa namna kuona upendo wa Yehova kuwa fundisho ya musingi kunaweza kukusaidia usishakie kama Yehova anakuhangaikia na anakuona wakati uko na magumu.

5. Fasiria namna mutu anaweza kuachana na mafundisho ya bongo.

5 Wakati ulianza kujifunza Biblia, nini njo ilikusaidia uachane na mafundisho ya bongo? Pengine yenye ilikusaidia ni kulinganisha byenye ulijifunza mu kanisa yako na byenye Biblia inafundisha. Kwa mufano: Tuseme zamani ulikuwa naamini kama Yesu njo Mungu Mweza-yote. Lakini wakati ulikuwa najifunza Biblia, ulianza kujiuliza ikiwa ile fundisho ni ya kweli kabisa. Wakati ulichunguza mambo yenye Biblia inafundisha, ulielewa kama ile fundisho haiko ya kweli. Uliachana na ile fundisho ya bongo na ukaamini fundisho ya kweli ya Biblia ni kusema, Yesu ni “muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote” na “Mwana muzaliwa-pekee wa Mungu.” (Kol. 1:15; Yoh. 3:18) Kusema kweli, haiko mwepesi kuachana na mafundisho ya bongo juu inaweza kuwa ‘imetia mizizi kabisa.’ (2 Ko. 10:4, 5) Lakini wakati uliachana nayo, haukuirudilia tena.—Flp. 3:13.

6. Juu ya nini unaweza kuwa hakika kama “upendo mushikamanifu [wa Yehova] unadumu milele”?

6 Wakati uko na magumu na unaanza kuwa na mashaka kama Yehova anakupenda, ufanye vile ulifanyaka wakati ulianzaka kujifunza Biblia. Uchunguze mambo yenye Biblia inafundisha juu ya upendo wa Yehova na ujiulize hivi: ‘Hii mawazo yenye niko nayo iko ku mustari kweli?’ Linganisha mashaka yenye uko nayo juu ya upendo wa Yehova na maneno ya andiko ya musingi ya hii habari, Zaburi 136:1. Juu ya nini Yehova anasema kama upendo wake ni “mushikamanifu”? Juu ya nini maneno “upendo wake mushikamanifu unadumu milele” inarudiliwa mara 26 mu Zaburi ya 136? Sawa tu mafundisho ingine ya musingi ya Biblia yenye uliamini, upendo mushikamanifu wa Yehova kwa watumishi wake nayo ni fundisho ya musingi ya Biblia. Wazo ya kama uko wa bure na Yehova hawezi kukupenda, ni ya bongo. Uachane kabisa na ile mawazo, sawa vile tu uliweza kuachana kabisa na mafundisho ingine ya bongo!

7. Taya maandiko fulani yenye inahakikisha kama Yehova anatupenda.

7 Mu Biblia muko maandiko ya mingi yenye inahakikisha kama Yehova anatupenda. Kwa mufano, Yesu aliambia hivi banafunzi yake: “Ninyi ni wa maana kuliko ndege shomoro wengi.” (Mt. 10:31) Yehova yeye peke aliambia hivi batu yake: “Nitakutia nguvu, ndiyo, nitakusaidia, nitakushika kwelikweli kwa mukono wangu wa kuume wa haki.” (Isa. 41:10) Unaona vile ile maneno iko wazi kabisa? Yesu haseme kama ‘Munaweza kuwa ba maana,” lakini anasema: “Ninyi ni wa maana.” Na Yehova naye haseme ‘Ninaweza kukusaidia,’ lakini anasema: “Nitakusaidia.” Kama unashakia upendo wa Yehova wakati wa magumu, maandiko ya vile inaweza kukusaidia ujisikie muzuri. Lakini haiko ile tu, itakusaidia ukuwe hakika kama Yehova anakupenda. Ile maandiko inasema kweli kabisa. Kama unasali juu ya mashaka yako na unafikiri sana juu ya ile maandiko, utaweza kusema hii maneno yenye iko mu 1 Yohana 4:16: “Tumejua na tumeamini upendo wenye Mungu iko nao kutuelekea.”a

8. Unaweza kufanya nini kama uko na mashaka kama Yehova anakupenda?

8 Sasa utafanya nini kama mu moyo wako, saa moya hivi, unajisikia tu sawa vile Yehova hakupendi? Linganisha byenye biko mu moyo wako na byenye unajua juu ya Yehova. Byenye biko mu moyo binaweza kubadilika saa ni saa, lakini kweli haiwezi kubadilika. Mambo yenye Biblia inasema juu ya upendo wa Yehova ni kweli. Kama tunawaza Yehova hatupendi, ni kusema tunatia pembeni sifa yake kubwa zaidi, upendo.—1 Yo. 4:8.

FIKIRI SANA JUU YA NAMNA YEHOVA ‘ANAKUPENDA’

9-10. Yesu alikuwa nazungumuzia nini wakati alisema maneno “Baba mwenyewe anawapenda ninyi” yenye kuwa mu Yohana 16:26, 27? (Ona pia picha.)

9 Maneno yenye Yesu aliambia banafunzi yake inaweza kutufundisha mambo ingine juu ya upendo wa Yehova. Alibaambia hivi: “Baba mwenyewe anawapenda ninyi.” (Soma Yohana 16:26, 27.) Yesu hakusema ile maneno juu tu ya kufurahisha banafunzi yake. Kama unasoma mistari yenye inatangulia, utaona kama Yesu hakukuwa nazungumuzia vile banafunzi yake balikuwa najisikia ile wakati, lakini alikuwa nazungumuzia jambo ingine. Alikuwa nazungumuzia sala.

10 Yesu alitoka tu kuambia banafunzi yake kama habapaswe kusali kwake lakini kupitia yeye. (Yoh. 16:23, 24) Ilikuwa jambo ya maana bajue ile. Juu ya nini? Juu kisha Yesu kufufuliwa, pengine banafunzi yake bangeangukia mu mutego wa kusali kwake juu balimujua muzuri na alikuwa rafiki yabo. Pengine bangewaza kama juu Yesu alikuwa nabapenda, bangesali kwake na kisha angebasemea kwa Baba yake. Lakini, Yesu alibaambia kama habapaswe kuwaza vile. Juu ya nini? Alibaambia hivi: “Baba mwenyewe anawapenda ninyi.” Ile kweli iko kati ya mafundisho ya musingi ya Biblia kuhusu sala. Kujua ile fundisho inakusaidia namna gani? Kupitia funzo yako ya Biblia, umemujua Yesu na kumupenda. (Yoh. 14:21) Lakini, sawa tu vile banafunzi ya Yesu ba mu karne ya kwanza, unaweza kusali kwa Mungu na kuwa hakika kama atakusikiliza, juu unajua kama ‘anakupenda.’ Kila wakati unasali kwa Yehova, unaonyesha kama unaamini ile maneno.—1 Yo. 5:14.

Picha: Ndugu anaikala inje na iko nasali juu ya mambo tatu ya maana. 1. Analetea bibi yake chakula, bibi yake iko mugonjwa na analala ku kitanda. 2. Iko najifunza Biblia pamoya na mutoto wake mwanamuke. 3. Iko nachunguza madokima ya mambo ya makuta.

Unaweza kusali kwa Yehova na kuwa hakika kama atakusikiliza, juu unajua kama ‘anakupenda.’ (Ona fungu ya 9-10)b


UELEWE JUU YA NINI UKO NA MASHAKA

11. Juu ya nini Shetani atafurahi kama unakuwa na mashaka kama Yehova anakupenda?

11 Juu ya nini tunaweza kuwa na mashaka kama Yehova anatupenda? Pengine unaweza kujibia, ‘ni juu ya Shetani,’ na uko na sheria. Shetani iko kati ya sababu zenye zinatufanya tukuwe na mashaka. Ibilisi iko ‘anatafuta kutumeza,’ na anapenda tushakie kama Yehova anatupenda. (1 Pe. 5:8) Lakini Yehova anatupenda njo maana alitutolea bei ya ukombozi. Shetani yeye anapenda tuwaze kama hatustahili ile bei ya ukombozi. (Ebr. 2:9) Kwa hiyo, nani njo atafurahi kama tunashakia kuwa Yehova anatupenda? Ni Shetani. Na nani njo atafurahi kama tunavunjika moyo na tunaacha kumutumikia Yehova wakati wa magumu? Ni Shetani. Ni bya kushangaza sana! Shetani njo Yehova hawezi kupenda, lakini anapenda siye njo tuwaze kama Yehova hapendi na alishatuacha. Ile ni kati ya “matendo ya ujanja” ya Shetani. (Efe. 6:11) Wakati tunaelewa ile mutego yenye Shetani anapenda tuangukie ndani, tunaazimia kabisa ‘kumupinga.’—Yak. 4:7.

12-13. Namna gani hali ya kutokamilika yenye tuliriti inaweza kufanya tushakie kama Yehova anatupenda?

12 Kuko sababu ingine yenye inaweza kufanya tushakie kama Yehova anatupenda. Ni sababu gani? Ni hali yetu ya kutokamilika yenye tuliriti. (Zb. 51:5; Ro. 5:12) Zambi imeharibisha uhusiano wetu pamoya na Muumbaji wetu. Lakini, imeharibisha pia namna yetu ya kuwaza, namna tunajisikia, na afya yetu.

13 Zambi iko na matokeo ya mubaya juu yetu. Inafanya tujihukumu, tukuwe na mahangaiko, tusijisikie salama, na tusikie haya. Tunaweza kujisikia vile wakati tunafanya jambo ya mubaya. Tunaweza pia kujisikia vile juu tunajua kama tuko batenda-zambi. Na inaeleweka kujisikia vile juu Yehova hakutuumba juu tukuwe batenda-zambi. (Ro. 8:20, 21) Sawa tu vile pneu ya kutoboka haiwezi tumika muzuri sawa vile ilikuwa natumika wakati ilikuwa ya mupya, na siye hatuwezi tu kuwa muzuri sawa vile tungekuwa kama hakungekuwa zambi. Njo maana wakati fulani tunakuwaka na mashaka kama Yehova anatupenda. Kama ile inatufikia, ni muzuri tukumbuke kama Yehova ni “Mungu mukubwa na mwenye kuogopesha sana, mwenye . . . kuonyesha upendo mushikamanifu kwa wale wenye wanamupenda na kushika amri zake.”—Ne. 1:5.

14. Namna gani kufikiri juu ya bei ya ukombozi kunaweza kutusaidia tukuwe hakika kama Yehova anatupenda? (Waroma 5:8) (Ona pia kisanduku “Fanya Angalisho na ‘Nguvu za Udanganyifu za Zambi.’”)

14 Wakati fulani, tunaweza kujisikia kama hatustahili upendo wa Yehova. Na kusema tu kweli, hatustahili—hakuna kitu yenye tunaweza fanya juu tustahili upendo wa Yehova. Na ile njo inafanya upendo wa Yehova ukuwe wa pekee sana. Yehova alitoa bei ya ukombozi juu anatupenda, na bei ya ukombozi inafunika zambi zetu. (1 Yoh. 4:10) Tukumbuke pia kama Yesu alikuya ku dunia juu ya kukomboa batenda-zambi, hapana batu bakamilifu. (Soma Waroma 5:8.) Siye bote tunakoseaka wakati fulani, na Yehova anajua vile. Wakati tunaelewa kama hali yetu ya kutokamilika inaweza kufanya tushakie kama Yehova anatupenda, tunafanya yetu yote juu ile hali isichochee mawazo yetu.—Ro. 7:24, 25.

Fanya Angalisho na “Nguvu za Udanganyifu za Zambi”

Biblia inazungumuzia “nguvu za udanganyifu za zambi.” (Ebr. 3:13) Hali yetu ya kutokamilika inaweza kutuchochea kufanya mambo ya mubaya, lakini pia inaweza kufanya tuendelee kuwa na mashaka kama Yehova anatupenda. Kwa kweli, zambi iko na “nguvu za udanganyifu.”

Tunaweza kuwaza kama siye habawezi kutudanganya. Kwa mufano, mutu anaweza waza kama yeye habawezi kumukula makuta. Lakini, kama haiko muangalifu, banaweza mukula makuta yote.

Vilevile, tunapaswa kuwa baangalifu wakati hali yetu ya kutokamilika inajaribu “kutudanganya” na kutufanya tuamini kama Yehova hatupendi. Hali yetu ya kutokamilika inaweza kufanya tukazie sana akili uzaifu wetu na makosa yetu. Lakini ile ni ‘nguvu za udanganyifu,’ za zambi na tunapaswa kuzipiganisha.

ENDELEA KUWA MUSHIKAMANIFU

15-16. Kama tunaendelea kuwa bashikamanifu kwa Yehova, tutakuwa hakika na nini na juu ya nini? (2 Samweli 22:26)

15 Yehova anapenda tukamate uamuzi muzuri wa “kushikamana naye.” (Kum. 30:19, 20) Kama tunafanya vile, tunaweza kuwa hakika kama ataendelea kuwa mushikamanifu kwetu. (Soma 2 Samweli 22:26.) Kama tunaendelea kuwa bashikamanifu kwa Yehova, tutakuwa hakika kama atatusaidia kuvumilia hali yoyote yenye inaweza kutupata mu maisha.

16 Sawa vile tumeona, kuko sababu za mingi zenye zinatusaidia tusibebwe huku na huku wakati tuko na magumu. Tunajua kama Yehova anatupenda na atatutegemeza. Ni vile Biblia inasema. Kama wakati fulani tunashakia kama Yehova anatupenda, tufikirie mambo yenye tunajua juu ya upendo wake, kuliko kukazia akili namna tuko najisikia ile saa. Tuendelee basi kuwa hakika kama upendo mushikamanifu wa Yehova ni wa milele, sawa tu vile Biblia inasema.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Utapata faida gani kama unaona upendo wa Yehova kuwa fundisho ya musingi ya Biblia?

  • Namna gani zambi yenye tuliriti inaweza kufanya tushakie kama Yehova anatupenda?

  • Nini njo itatusaidia tuache kushakia kama Yehova anatupenda?

WIMBO 159 Mumupatie Yehova Utukufu

a Mifano ingine iko mu Kumbukumbu la Torati 31:8, Zaburi 94:14, na Isaya 49:15.

b MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu iko nasali Yehova amusaidie kuhangaikia bibi yake mwenye iko mugonjwa, kutumikisha muzuri makuta, na kufundisha mutoto wake kumupenda Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine