MAISHA YA MUKRISTO
Wazazi—Mufundishe Watoto Wenu Namna ya Kumufurahisha Mungu
Yehova anaonaka vijana kuwa wa maana sana. Anaonaka maendeleo ya kiroho yenye wako nafanya na uvumilivu wao. (1Sa 2:26; Lu 2:52) Hata kama wangali wadogo sana, watoto wanaweza kumufurahisha Yehova kupitia mwenendo wao wa muzuri. (Mez 27:11) Kupitia tengenezo yake, Yehova ametolea wazazi vyombo vya muzuri sana vyenye wanaweza kutumia juu ya kusaidia watoto wao wamupende na kumutii Yehova.
MUANGALIE VIDEO WATOTO—UVUMILIVU WENU UNAMUFURAHISHA YEHOVA! NA KISHA MUZUNGUMUZIE MAULIZO YENYE KUFUATA:
Kwa miaka mingi, namna gani Yehova amesaidia na kuongoza vijana?
Tuko na vifaa gani vyenye vinaweza kusaidia wazazi?
Kama uko kijana, ni jambo gani yenye Yehova ametutolea yenye imekusaidia, na juu ya nini?