HABARI YA KUJIFUNZA YA 41
Tunatumikia Mungu Mwenye Iko “Tajiri Katika Rehema”
“Yehova ni mwema kwa wote, na rehema yake inaonekana katika kazi zake zote.”—ZB. 145:9.
WIMBO 44 Sala ya Mutu wa Hali ya Chini
KIFUPI YA HABARIa
1. Ni nini inaweza kuya mu akili yako wakati unafikiria mutu mwenye rehema?
WAKATI unafikiria mutu mwenye rehema, pengine unaona ni mutu mwenye kuwa muzuri, mutu wa roho ya muzuri, mwenye kuwa na huruma na mukarimu. Na pengine, habari yenye Yesu alisema juu ya Musamaria mwema njo inakukuya mu akili. Ule mwanaume wa taifa ingine “alimutendea kwa rehema” Muyahudi mwenye aliangukiaka mu mikono ya bamwizi. Ule Musamaria “akamusikilia huruma” ule Muyahudi mwenye aliumizwa na kwa upendo akakamata mipango fulani ili apate matunzo. (Lu. 10:29-37) Ile mufano inaonyesha waziwazi sifa ya muzuri sana ya Mungu wetu: Rehema. Ile sifa, ni alama ya upendo wa Mungu na anatuonyesha ile sifa mu njia mingi kila siku.
2. Ni mu njia gani ingine rehema inaweza kuonyeshwa?
2 Kuko jambo ingine pia kuhusu rehema yenye inaweza kuya mu akili yetu. Mutu mwenye rehema anaweza kuamua kama hatapatia mutu mwingine nizamu, hata kama alistahili kuipata. Kuhusu ile jambo, Yehova pia alituonyesha rehema yake. Mutunga-zaburi mumoja alisema hivi: “Hajatutendea kulingana na zambi zetu.” (Zb. 103:10) Lakini wakati fulani, Yehova anaweza kupatia nizamu ya kweli kabisa mutu mwenye alifanya zambi.
3. Ni maulizo gani tutazungumuzia mu hii habari?
3 Mu hii habari, tutazungumuzia maulizo tatu: Juu ya nini Yehova anaonyesha rehema? Je, inawezekana kupatia mutu nizamu na wakati ileile kumuonyesha rehema? Na ni nini inaweza kutusaidia tuonyeshe rehema? Tuone vile Neno ya Mungu inajibia ile maulizo.
JUU YA NINI YEHOVA ANAONYESHA REHEMA?
4. Juu ya nini Yehova anaonyesha rehema?
4 Yehova anapenda kuwa mwenye rehema. Mutume Paulo aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandika kama Mungu iko “tajiri katika rehema.” Mu ile andiko, Paulo alikuwa anafasiria kama Mungu ni mwenye rehema juu anapatia tumaini ya mbinguni watumishi wake watiwa-mafuta wenye hawakamilike. (Efe. 2:4-7) Lakini, Yehova haonyeshe rehema yake tu kwa watumishi wake watiwa-mafuta. Mutunga-zaburi Daudi aliandika hivi: “Yehova ni mwema kwa wote, na rehema yake inaonekana katika kazi zake zote.” (Zb. 145:9) Juu Yehova anapenda watu, anaonyesha rehema yake kila mara wakati anaona kuko sababu ya kufanya vile.
5. Namna gani Yesu alijifunza rehema ya Yehova?
5 Hakuna mutu anajua muzuri kabisa vile Yehova anaonyeshaka rehema yake, sawa vile Yesu. Yehova na Yesu waliishi mbinguni kwa miaka mingi sana, mbele Yesu akuye hapa ku dunia. (Mez. 8:30, 31) Na mu hali za mingi, Yesu aliona namna baba yake alionyesha wanadamu watenda-zambi rehema yake. (Zb. 78:37-42) Na mu mafundisho yake, mara mingi Yesu alikazia ile sifa ya rehema ya baba yake.
Baba hakumushushia heshima mwana wake mupotevu; alimukaribisha kwake (Ona fungu ya 6)c
6. Yesu alitumia mufano gani ili kutusaidia kuelewa rehema ya Baba yake?
6 Sawa vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, Yesu alitumia mufano wa mwana mupotevu ili kutusaidia kuelewa namna Yehova anapenda kuonyesha rehema yake. Ule mwana alitoka kwao na “akatumia mubaya mali yake kwa kuishi maisha ya upotovu.” (Lu. 15:13) Kisha, alitubu juu ya mwenendo wake, akajinyenyekeza na akarudia kwao. Baba yake alifanya nini? Haikukawia kwa ule kijana kuona mambo yenye baba yake alifanya. Yesu alisema hivi: “Wakati [ule kijana] alikuwa angali mbali, baba yake akamuona na akamusikilia huruma, akamukimbilia, akamukumbatia kwa upole wote na kumubusu.” Ule baba hakumushushia heshima mutoto yake. Lakini, alimusamehe na alimukaribisha kwa furaha katika familia yake. Huyu mwana mupotevu alifanya zambi kubwa lakini baba yake alimusamehe juu mutoto alitubu. Huyu baba mwenye rehema wa mu ile mufano, anafananisha Yehova. Mu njia yenye kugusa moyo, Yesu anaonyesha vile baba yake iko tayari kusamahe watenda-zambi wenye wanatubu kikweli.—Lu. 15:17-24.
7. Vile Yehova anaonyesha rehema inaonyesha namna gani kama iko na hekima sana?
7 Yehova anaonyesha rehema juu iko na hekima sana. Kila mara Yehova anakamata maamuzi kwa faida ya viumbe wake. Njo maana Biblia inasema hivi: “Hekima yenye inatoka juu ni yenye kujaa rehema na matunda ya muzuri.” (Yak. 3:17) Sawa vile muzazi mwenye kuwa na upendo, Yehova anajua kama ni muzuri kuonyesha watumishi wake rehema. (Zb. 103:13; Isa. 49:15) Rehema ya Yehova inapatia watoto wake tumaini hata kama hawakamilike. Kwa hiyo, juu Yehova iko na hekima sana, kila mara anaonyesha rehema yake wakati anaona kama kuko sababu ya kufanya vile. Lakini wakati ileile, rehema ya Yehova ni yenye usawaziko. Yehova iko na hekima. Haonyeshake rehema yake ikiwa kufanya vile itavunja sheria yake.
8. Wakati fulani, ni mupango gani uko wa lazima na juu ya nini?
8 Waza mutumishi fulani wa Yehova anaamua kuishi maisha ya upotovu. Siye tunapaswa kufanya nini? Akiongozwa na roho ya Mungu, Paulo aliandika hivi: “Muache kushirikiana” naye. (1 Ko. 5:11) Watenda-zambi wenye hawatubu wanatengwa na kutaniko. Ule mupango ni wa lazima sana juu unalinda ndugu na dada waaminifu, na ile inaonyesha kama tunaunga mukono kanuni za Yehova. Lakini ni nguvu kwa watu fulani kuona kama kutengwa ni alama ya rehema ya Mungu. Je, wako na sheria? Muache tuone.
JE, KUTENGA MUTU FULANI NI ALAMA YA REHEMA?
Kondoo anaweza kutengwa na kondoo wengine wakati iko mugonjwa. Lakini muchungaji ataendelea tu kumuhangaikia (Ona fungu ya 9-11)
9-10. Kulingana na Waebrania 12:5, 6, juu ya nini tunaweza kusema kama kutenga mutenda-zambi mwenye hatubu ni alama ya rehema? Leta mufano.
9 Wakati tunasikia tangazo fulani ku mukutano yenye inasema kama mutu fulani mwenye tunajua na mwenye tunapenda “haiko tena Shahidi wa Yehova,” ile inaletaka huzuni sana. Pengine tunaweza kujiuliza kama ilikuwa lazima kabisa ule mupendwa wetu atengwe. Je, kutenga mutu ni alama kabisa ya rehema? Ndiyo kabisa. Kukosa kupatia nizamu mutu mwenye anastahili kuipata, ni alama ya kukosa hekima, rehema ao upendo. (Mez. 13:24) Kutenga mutenda-zambi mwenye hatubu, kunaweza kumusaidia abadilishe matendo yake ya mubaya? Ndiyo, kunaweza kumusaidia. Wengi wenye waliangukia mu zambi nzito waliona kama nizamu yenye wazee waliwapatia njo yenye walikuwa nayo lazima ili kurudiwa na ufahamu, kubadilisha mwenendo wao, na kumurudilia Yehova baba mwenye upendo.—Soma Waebrania 12:5, 6.
10 Fikiria hii mufano. Muchungaji fulani anaona kama moja kati ya kondoo zake iko mugonjwa. Anajua kama, juu amutunze muzuri, ni lazima amutenge na kondoo wengine. Lakini, kondoo ni wanyama wenye wanapenda kuishi pamoja. Na wakati kondoo fulani anatengwa na wengine, ile inaweza kumuhangaisha sana. Lakini, wakati ule mchungaji anamutenga na kondoo wengine, ile inaonyesha kama ni muchungaji mubaya ao namna yake ya kutunza haiko ya muzuri? Jibu ni hapana. Anajua kama akimuacha ule kondoo mumoja kati ya kondoo wengine anaweza kuwaambukiza. Lakini wakati anamutenga na wengine, ile inasaidia kulinda kundi yote ya kondoo.—Linganisha na Mambo ya Walawi 13:3, 4.
11. (a) Ni mu njia gani tunaweza kulinganisha ule mutu mwenye alitengwa na kondoo mwenye iko mugonjwa? (b) Ni chakula gani ya kiroho na musaada gani wa wazee wenye watengwa wanaweza kupata?
11 Wakati Mukristo fulani anatengwa, tunaweza kumulinganisha na kondoo mwenye iko mugonjwa. Iko mugonjwa kiroho. (Yak. 5:14) Sawa vile ugonjwa wa kawaida, ugonjwa wa kiroho unaweza kuambukizia watu wengine. Njo maana ni jambo ya lazima mu hali fulani kumutenga Mukristo mwenye iko mugonjwa kiroho na kutaniko. Ile nizamu inaonyesha kama Yehova anapenda ndugu na dada waaminifu wa mu kutaniko, na ile inaweza kusaidia mutenda-zambi abadilishe matendo yake na hata kumusaidia atubu. Wakati mutu fulani anatengwa, anaweza kukusanyika juu akulishwe na kujengwa kiroho. Anaweza pia kupata vichapo vyenye anaweza kutumia na anaweza kuangalia JW Télédiffusion. Na kadiri wazee wanaangalia namna iko anafanya mabadiliko, wakati fulani wanaweza kumupatia mashauri na muongozo fulani wenye utamusaidia arudishe afya yake ya kiroho ili afikie kurudishwa.b
12. Ni jambo gani yenye upendo na yenye rehema wazee wanaweza kufanyia mutenda-zambi mwenye hatubu?
12 Tusisahau kama, ni mutenda-zambi tu mwenye hatubu njo anatengewaka. Wazee wanakuwaka wanafikiri kwa uzito sana mbele ya kuamua kama mutu fulani atatengwa ao hapana. Wanajua kama ni Yehova njo anatoa nizamu kwa “kiasi chenye kufaa.” (Yer. 30:11) Wazee wanapenda ndugu zao, na hawapende kuwafanyia mambo yenye inaweza kuharibisha hali yao ya kiroho. Lakini wakati fulani, ni alama ya upendo na ya rehema kuondoa mu kutaniko mutenda-zambi mwenye hatubu.
13. Juu ya nini Mukristo moja wa Korinto alipaswa kutengwa?
13 Ona vile mutume Paulo alitendea mutenda-zambi mumoja kwa karne ya kwanza, mwenye hakutubu. Ule Mukristo alikuwa anafanya uasherati pamoja na bibi ya baba yake. Ile ni jambo ya mubaya sana! Kuhusu ile jambo, Yehova aliambiaka hivi taifa ya Israeli: “Mwanaume mwenye analala na bibi ya baba yake amemuletea baba yake haya. Wote wawili wanapaswa kabisa kuuawa.” (Law. 20:11) Lakini kusema kweli, Paulo hangeambia ndugu wa mu ile kutaniko waue ule mwanaume mutenda-zambi. Lakini aliwaomba wamutenge. Ile matendo ya uasherati ya ule mwanaume ilikuwa na uvutano mubaya mu kutaniko na hata wengine mu kutaniko waliona kama ile haikukuwa zambi nzito kabisa!—1 Ko. 5:1, 2, 13.
14. Namna gani Paulo alionyesha rehema kuelekea mwanaume fulani mwenye alitengwa mu kutaniko ya Korinto, na juu ya nini alifanya vile? (2 Wakorinto 2:5-8, 11)
14 Kisha wakati fulani, Paulo alipata habari kama ule Mukristo alifanya mabadiliko. Ule mutenda-zambi alitubu kabisa! Hata kama ule mwanaume aliletea kutaniko haya, Paulo aliambia wazee kama wasikuwe “wakali sana.” Aliwaambia hivi: ‘Musamehe kwa fazili na kumufariji.’ Ona sababu yenye ilifanya Paulo aseme kama wanapaswa kufanya vile: “Ili asilemewe na huzuni yenye kupita kiasi.” Paulo alimusikilia huruma ule mwanaume mwenye alikuwa ametubu. Hakupenda ule mwanaume aendelee kulemewa, aendelee kulia ndani yake juu ya mambo yenye alifanya na hivi aache kutafuta musamaha.—Soma 2 Wakorinto 2:5-8, 11.
15. Namna gani wazee wanaweza kutoa nizamu ikiwa ni lazima na wakati ileile kuonyesha rehema?
15 Kama vile Yehova, wazee wanapenda kuonyesha rehema. Wanatoa nizamu wakati ni lazima. Lakini, wanaonyesha pia rehema kama kunaweza kuwa sababu ya kufanya vile. Kama wazee hawapatie nizamu mutenda-zambi, ile haiko tena rehema lakini ni kuachilia tu mambo na ile inaonyesha kama wanakubaliana na matendo ya mubaya yenye ule mutu alifanya. Je, ni wazee tu njo wanapaswa kuonyesha rehema?
NI NINI INAWEZA KUTUSAIDIA SIYE WOTE TUONYESHE REHEMA?
16. Kulingana na Mezali 21:13, Yehova anatendea namna gani wale wenye wanakatala kuonyesha wengine rehema?
16 Wakristo wote wanajikaza kuiga rehema ya Yehova. Juu ya nini? Sababu moja ni kwamba, Yehova hatasikiliza sala za wale wenye wanakatala kuonyesha wengine rehema. (Soma Mezali 21:13.) Hakuna mutu kati yetu mwenye atapenda Yehova akatale kusikiliza sala zake. Njo maana tunajikaza sana ili kuepuka roho ya mubaya. Kuliko kukatala kusikiliza Mukristo mwenye iko mu magumu, tunapaswa kuwa tayari kila wakati ili kusikiliza “kilio cha mutu wa hali ya chini.” Vilevile pia, tunakamata kwa uzito hii maneno yenye iliongozwa na roho ya Mungu: “Ule mwenye hazoee kuonyesha rehema atapata hukumu yake bila rehema.” (Yak. 2:13) Kama kwa unyenyekevu tunakumbuka kama siye wote tuko na lazima ya rehema, ile itatusaidia pia kuonyesha rehema. Tunapenda zaidi sana kuonyesha rehema wakati mutenda-zambi mwenye anatubu, anarudia katika kutaniko.
17. Namna gani Mufalme Daudi alionyesha rehema ya kweli?
17 Mifano fulani yenye kuwa mu Biblia inaweza kutusaidia kuonyesha rehema na kuepuka kutosikilia wengine huruma. Fikiria mufano wa Mufalme Daudi. Mara mingi alikuwa naonyesha rehema. Hata kama Sauli alipenda kumuua, Daudi alionyesha rehema mutiwa-mafuta wa Mungu. Hakupenda kulipiza kisasi hata siku moja, ao kupenda kumutendea mubaya Sauli.—1 Sa. 24:9-12, 18, 19.
18-19. Ni hali gani mbili zenye zinaonyesha kama Daudi hakutenda kwa rehema?
18 Lakini, haiko kila mara njo Daudi alionyesha rehema. Kwa mufano, wakati Nabali, mwanaume moja mwenye alikuwa mubaya sana, alitumia maneno ya kumukosea heshima Daudi, na alikatala kumupatia Daudi na wanaume wake chakula, ile ilifanya Daudi akasirike sana na akaamua kuenda kumuua Nabali na wanaume wote wenye walikuwa mu nyumba yake. Lakini bibi ya Nabali, Abigaili, alikuwa mutu muzuri na muvumilivu. Alifanya kwa uharaka ili kumupatia Daudi chakula. Ile ilisaidia Daudi asikuwe na hatia ya damu.—1 Sa. 25:9-22, 32-35.
19 Siku ingine, nabii Natani alimuambia Daudi kama kuko mutu fulani tajiri mwenye aliiba kondoo moja wa maskini. Daudi alikasirika sana na akasema: “Kama vile hakika Yehova anaishi, mutu mwenye alifanya vile anastahili kufa!” (2 Sa. 12:1-6) Lakini, Daudi alijua sheria ya Musa. Mutu mwenye aliiba kondoo moja, alipaswa kupatia mwenye ile kondoo, kondoo ine. (Kut. 22:1) Lakini yeye anasema alipaswa kuuawa! Ile ilikuwa hukumu kali kabisa. Kusema kweli, Natani alikuwa anatumia tu mufano ili kumusaidia Daudi aelewe kama alikuwa amefanya mambo ya mubaya sana! Na Yehova alimuonyesha Daudi rehema sana kuliko rehema yenye Daudi alionyesha ule mutu mwenye aliiba kondoo, kama vile Natani alizungumuzia mu mufano wake!—2 Sa. 12:7-13.
Mufalme Daudi hakuonyesha rehema ule mwanaume mwenye Natani alizungumuzia mu mufano wake (Ona fungu ya 19-20)d
20. Mufano wa Daudi unaweza kutufundisha nini?
20 Kumbuka kama wakati Daudi alikasirika, aliamua kama Nabali na wanaume wake wote walipaswa kuuawa. Na kisha, Daudi alisema tena kama, ule mwanaume mwenye Natani alizungumuzia mu mufano wake, alipaswa kuuawa. Daudi alikuwa mwanaume muzuri. Sasa juu ya nini alihukumu ule mwizi mwenye Natani alizungumuzia bila huruma. Fikiria hali. Ile wakati, zamiri ya Daudi ilikuwa inamuhukumu. Kama mutu iko anahukumu-hukumu wengine, ile inaonyesha kama hana hali ya muzuri ya kiroho. Yesu alionya hivi wafuasi wake: “Muache kuhukumu ili musihukumiwe; kwa maana mutahukumiwa kwa hukumu yenye munahukumu wengine.” (Mt. 7:1, 2) Kwa hiyo basi, tunapaswa kufanya yetu yote ili kuepuka kuhukumu wengine, lakini kujikaza kuwa “tajiri katika rehema,” sawa vile Mungu wetu.
21-22. Ni njia gani mbalimbali tunaweza kutumia ili kuonyesha rehema?
21 Rehema haiko tu hisia. Kwa kweli, mutu mwenye iko na rehema anafanyaka mambo fulani ili kusaidia wengine. Kwa hiyo, siye wote tunaweza kuchunguza ili kujua ni nani mu familia yetu, mu kutaniko yetu, ao watu wenye tunaishi nao, wenye wako na lazima ya musaada. Kusema kweli, kuko njia mingi zenye tunaweza kutumia ili kuonyesha rehema! Je, kuko mutu mwenye iko na lazima ya faraja? Tunaweza kumusaidia, kwa mufano kwa kumupatia chakula ao kumusaidia na mambo ingine ya lazima? Je, Mukristo mwenye amerudishwa, iko na lazima ya faraja? Iko na lazima ya rafiki wa muzuri mwenye atamutia moyo? Je, tunaweza kutangazia wengine ujumbe wa habari njema wenye kufariji? Ile ni moja kati ya njia za muzuri sana zenye tunaweza kutumia ili kuonyesha kila mutu rehema.—Yob. 29:12, 13; Ro. 10:14, 15; Yak. 1:27.
22 Tukijua kama watu fulani wako na lazima ya musaada, ile inaweza kutupatia nafasi ya muzuri ya kuwaonyesha rehema. Na wakati tunaonyesha rehema, tunamufurahisha sana baba yetu wa mbinguni, Mungu mwenye ni “tajiri katika rehema”!
WIMBO 43 Sala ya Shukrani
a Rehema ni moja kati ya sifa zenye kuvutia sana za Yehova, na ni muzuri kwa kila mumoja wetu kuwa na ile sifa. Mu hii habari, tutaona juu ya nini Yehova anaonyesha rehema. Tena, tutaona juu ya nini tunasema kama nizamu yake ni yenye rehema. Na ku mwisho tutaona namna tunaweza kuonyesha rehema yake.
b Ili kujua namna ule mwenye alishatengwa anaweza tena kurudisha urafiki wake pamoja na Mungu na namna wazee wanaweza kumusaidia, ona habari “Namna Unaweza Kurudisha Tena Urafiki Wako Pamoja na Yehova,” yenye kuwa mu hii gazeti.
c MAFASIRIO YA PICHA: Wakati iko ku sehemu ya juu ya nyumba yake, baba anaona mwana wake mupotevu iko anarudia ku nyumba, na anakimbia ili kuenda kumukumbatia.
d MAFASIRIO YA PICHA: Akiwa na zamiri yenye kumuhukumu, Mufalme Daudi anakasirika sana wakati Natani anamufasiria mufano fulani, na anasema kama ule mwanaume tajiri anastahili kufa.