Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w21 Mwezi wa 10 uku. 14-17
  • Namna Unaweza Kurudisha Tena Urafiki Wako Pamoja na Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Unaweza Kurudisha Tena Urafiki Wako Pamoja na Yehova
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAGUMU
  • UJIWEKEE MIRADI YENYE UNAWEZA KUFIKIA
  • USIVUNJIKE MOYO!
  • ‘Ita Bazee’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Yehova Anakupenda Sana!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Wazee​—Muendelee Kuiga Mutume Paulo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Hauko Peke Yako Juu Sikuzote Yehova Iko na Weye
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
w21 Mwezi wa 10 uku. 14-17
Ndugu moja mwenye alishaishiwa kabisa kuona vile itamuomba wakati na kazi mingi ili kutengeneza nyumba yake yenye ilishabomoka.

Namna Unaweza Kurudisha Tena Urafiki Wako Pamoja na Yehova

KILA mwaka kondoo wengi wanarudishwa katika kutaniko ya Kikristo. Fikiria “furaha kubwa mbinguni” wakati kondoo mwenye alikuwa alishapotea anamurudilia Yehova! (Lu. 15:7, 10) Ikiwa umerudishwa unaweza kuwa hakika kama, Yesu, malaika na Yehova yeye mwenyewe wanafurahi kuona vile umerudishwa tena mu kutaniko. Unaweza kupata magumu kadiri unajikaza kurudisha tena urafiki wako pamoja na Yehova. Ni magumu gani fulani yenye utapata, na ni mambo gani inaweza kukusaidia?

MAGUMU

Ndugu na dada wengi wanaendelea kuvunjika moyo hata wakati wamerudishwa mu kutaniko. Pengine unaelewa namna Mufalme Daudi alijisikia. Hata kisha kusamehewa zambi zake, alisema hivi: “Makosa yangu mengi yananilemea.” (Zb. 40:12; 65:3) Kisha mutu kumurudilia Yehova, pengine anaweza kuendelea kujihukumu ao kusikia haya kwa miaka mingi. Isabelle alitengwa kwa zaidi ya miaka 20.a Anasema hivi: “Ilikuwa nguvu sana kwangu kuamini kuwa Yehova angenisamehe.” Kama unavunjika moyo, hali yako ya kiroho inaweza tena kuwa zaifu. (Mez. 24:10) Usiache ile jambo ikufikie.

Wengine wanaogopa pengine hawataweza kufanya jambo yoyote yenye wako nayo lazima ili kurudisha tena urafiki wao pamoja na Yehova. Kisha kurudishwa, Antoine alisema hivi: “Nilijisikia sawa vile nilikuwa nimesahau mambo mingi yenye nilikuwa nimejifunza ao yenye nilikuwa nimefanya wakati nilikuwa Shahidi.” Hali sawa za vile zinaweza kufanya watu fulani, washindwe kufanya yao yote kwa ajili ya Yehova.

Kwa mufano, kama nyumba ya mutu fulani iliharibika sana juu ya upepo mukali, anaweza kujisikia mubaya sana wakati anafikiria namna itakamata wakati na kazi mingi sana ili kujenga tena ile nyumba. Vilevile, kama urafiki wako pamoja na Yehova uliharibika juu ya zambi nzito yenye ulifanya, pengine unaweza kujisikia sawa vile itaomba kujikaza sana ili kurudisha tena urafiki wako pamoja na Yehova. Lakini kuko musaada.

Yehova anatuambia hivi: “Sasa, mukuje, tunyooshe mambo kati yetu.” (Isa. 1:18) Tayari ulishajikaza sana ili ‘kunyoosha mambo.’ Yehova anapenda bidii yenye ulionyesha. Waza kidogo: Juu ulimurudilia Yehova ile inamupatia sababu ya kuonyesha kama Shetani iko muongo!​—Mez. 27:11.

Wakati unamurudilia Yehova, tayari utakuwa karibu naye na anaahidi kama atakukaribia pia. (Yak. 4:8) Ni muzuri sana watu wajue kama umerudia tena mu kutaniko, lakini ni lazima ufanye mengi zaidi ya ile. Unapaswa kutia nguvu upendo wako kwa ajili ya Baba yako na rafiki yako Yehova. Unaweza kufanya vile namna gani?

UJIWEKEE MIRADI YENYE UNAWEZA KUFIKIA

Ujikaze kujiwekea miradi yenye unaweza kufikia. Pengine unakumbuka mambo fulani ya musingi yenye ulijifunza kuhusu Yehova na ahadi yake ya Paradiso yenye kuja. Lakini uko na lazima ya kuwa na programu ya muzuri tena, kwa mufano kuhubiri kwa ukawaida, kuenda ku mikutano na kupitisha wakati pamoja na ndugu na dada. Fikiria miradi yenye kufuata.

Uzungumuze na Yehova kila mara. Baba yako wa mbinguni Yehova anaelewa kama, kadiri unaendelea kujihukumu-hukumu juu ya kosa yenye ulifanya ile inaweza kuwa nguvu kwako kusali. (Ro. 8:26) Hata vile, “udumu katika sala,” umuambie Yehova kama unapenda kabisa kuwa rafiki yake. (Ro. 12:12) Andrej anasema hivi: “Nilikuwa najihukumu-hukumu sana na nilikuwa nasikia haya. Lakini kisha kila sala nilisikia natulia sana. Nilijisikia kuwa na amani ya akili.” Kama haujue usali juu ya nini fikiria sala za Mufalme Daudi mwenye alitubu. Zile sala zinapatikana mu Zaburi ya 51 na 65.

Ujifunze Biblia kwa ukawaida. Kufanya vile kutakusaidia ukuwe na imani yenye nguvu na kutasaidia upendo wako kwa Yehova uongezeke. (Zb. 19:7-11) Felipe anasema hivi: “Juu sikukuwa najifunza Biblia kwa ukawaida na kuisoma, nilifikia kuwa muzaifu kiroho na kisha nikamukosea Yehova. Sikupenda tena kufanya ile kosa mara mbili. Njo maana niliamua kuanza kufanya funzo ya pekee ili kujilinda kiroho.” Unaweza pia kufanya vile. Kama unapenda kuchagua habari fulani ili kufanya funzo yako ya kipekee, unaweza kuomba rafiki mwenye ni mukomavu kiroho ili akusaidie.

Urudishe tena urafiki wako pamoja na ndugu na dada zako. Watu fulani wenye walirudia mu kutaniko waliogopa kama wengine wanaweza kuwaona mubaya. Larissa anasema hivi: “Nilikuwa nasikia haya sana. Nilijisikia kama niliumiza ao kuvunja moyo ndugu zangu na dada zangu. Nilijisikia vile kwa muda murefu.” Ukuwe hakika kama wazee na Wakristo wengine wakomavu wako tayari kukusaidia kadiri unajikaza kurudisha urafiki wako pamoja na Yehova. (Ona kisanduku, “Wazee Wanaweza Kufanya Nini?” Wanafurahi sana kuona vile umerudishwa na wanapenda ukuwe na furaha!​—Mez. 17:17.

Ni nini inaweza kukusaidia kuwa karibu na kutaniko? Huzuria mikutano pamoja na ndugu na dada zako na uhubiri kwa ukawaida. Ile inaweza kukusaidia namna gani? Felix alisema hivi: “Ndugu na dada mu kutaniko walikuwa wananichunga kwa hamu nirudishwe. Nilijisikia kuwa wa maana sana. Wote walinisaidia nijisikie kuwa tena mu familia, kujisikia kuwa mwenye kusamehewa na kuendelea kumutumikia Yehova. (Ona kisanduku, “Unaweza Kufanya Nini?”

Unaweza Kufanya Nini?

Utie nguvu tena hali yako ya kiroho

Muzee moja iko anasali pamoja na ndugu fulani mwenye amemurudilia Yehova.

UZUNGUMUZE NA YEHOVA KILA MARA

Umuambie Yehova kama unapenda kuwa rafiki yake. Wazee watasali kwa ajili yako na pamoja na weye

Ule muzee anatumia kitabu “Mkaribie Yehova” ili kujifunza Biblia pamoja na ule ndugu.

UJIFUNZE BIBLIA KWA UKAWAIDA

Ujikulishe kiroho, na ile itasaidia upendo wako kwa Yehova uongezeke

Ule ndugu iko anaongea na ndugu na dada wa kutaniko wakati wanakutana fasi moja hivi ili kupitisha wakati pamoja.

URUDISHE URAFIKI WAKO NA WENGINE

Ukusanyike pamoja na ndugu na dada zako, na uhubiri kila mara

USIVUNJIKE MOYO!

Shetani ataendelea kukuletea “magumu” mingi zaidi juu aregeze bidii yenye uko unaonyesha ili kurudisha tena urafiki wako pamoja na Yehova. (Lu. 4:13) Ukuwe tayari kutia nguvu hali yako ya kiroho sasa.

Kuhusu kondoo wake Yehova anaahidi hivi: “Mwenye alipotea nitamutafuta, mwenye kutanga-tanga nitamurudisha, mwenye kuumia nitafunga vidonda vyake, na mwenye kuwa muzaifu nitamutia nguvu.” (Eze. 34:16) Yehova amesaidia watu wengi watengeneze uhusiano wao pamoja naye. Ukuwe hakika kama anapenda kukusaidia uendelee kutia nguvu uhusiano wako pamoja naye.

Wazee Wanaweza Kufanya Nini?

Ule muzee iko anasaidia ule ndugu kujenga tena nyumba yake yenye iliharibika.

Wazee wako na daraka kubwa ya kusaidia muhubiri mwenye alirudishwa arudishe tena urafiki wake pamoja na Yehova. Ona mambo wanaweza kufanya juu ya kusaidia mwenye alirudishwa.

Muwahakikishie. Mutume Paulo alijua kama mutenda-zambi mwenye alitubu kikweli angeweza ‘kulemewa na huzuni yenye kupita kiasi.’ (2 Ko. 2:7) Pengine mara mingi angesikia haya na kuvunjika moyo. Paulo alitia moyo kutaniko hivi: “Munapaswa kumusamehe kwa fazili na kumufariji.” Wale wenye walirudishwa wako na lazima tuwahakikishie kama Yehova na waamini wenzao wanawapenda sana. Kila mara, wakati wazee wanapongeza na kusaidia wenye walirudishwa ile inaweza kuwasaidia wasivunjike moyo.

Musali pamoja nao. “Sala ya kumulilia Mungu ya mwenye haki iko na nguvu nyingi.” (Yak. 5:16) Larissa, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Niliambia wazee kuhusu mashaka na woga wenye nilikuwa nao. Walisali kwa ajili yangu. Kisha, nilifikia kuelewa kama wazee hawakunikasirikia, walipenda tu kunisaidia nirudishe tena uhusiano wangu pamoja na Yehova.” Theo anasema: “Sala zenye wazee walitoa zilinihakikishia kama Yehova ananipenda sana na anaona mambo ya muzuri yenye ninafanya, hapana tu ya mubaya.”

Mukuwe marafiki wao. Wenye walisharudishwa wako na lazima ya marafiki mu kutaniko. Justin, muzee mumoja, anasema hivi: “Tumia kila nafasi yenye inajitokeza ili kuhubiri pamoja na wale wenye walisharudishwa. Na jambo ya maana zaidi ni kuwatembelea kwao. Na pia ni jambo ya maana sana kuwa marafiki pamoja nao!” Muzee mwingine mwenye kuitwa Henry, anasema hivi: “Kama ndugu na dada mu kutaniko wanaona namna wazee wanafanya urafiki pamoja na wale wenye wamerudishwa, ile itawasaidia nao pia wafanye vile.”

Muwasaidie kujifunza. Rafiki mwenye ni mukomavu kiroho anaweza kusaidia mwenye alirudishwa akuwe na programu ya muzuri ya funzo. Darko, muzee moja, anasema hivi: “Napendaka kuwaambia mambo yenye kutia moyo yenye nilipata mu funzo yangu ya kipekee na kuwaonyesha namna napendaka sana kujifunza Biblia. Pia, najifunzaka nao habari fulani yenye kutia moyo.” Clayton, muzee mwingine, anasema hivi: “Nawatiaka moyo watafute habari fulani ya Biblia kuhusu mutu mwenye alipambana na hali yenye kufanana na yao na waone mambo yenye wanaweza kujifunza.”

Mukuwe wachungaji wazuri. Wale wenye walirudishwa waliona namna wazee walikuwa wanatimiza daraka yao ya waamuzi. Lakini sasa wako na lazima ya kuona wazee mu daraka yao ya wachungaji. (Yer. 23:4) Mukuwe tayari kuwasikiliza na kuwapongeza. Muzungumuze nao kila mara. Ona mambo yenye muzee moja mwenye kuitwa Marcus anafanyaka wakati anatembelea ndugu na dada mu kazi ya uchungaji. Anasema hivi: “Tunazungumuzaka na mutu mwenye amerudishwa kuhusu andiko fulani, tunamupongeza na tunamuhakikishia kama tunafurahi kuona vile alijikaza kumurudilia Yehova, na Yehova pia anafurahi. Na ku mwisho tunapangaka tarehe ya kumuona tena siku ingine.”

a Majina mu hii habari imebadilishwa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine