Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w22 Mwezi wa 10 uku. 2-5
  • 1922—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 1922—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “WAZO YA MUZURI SANA”
  • KUHUBIRIA WATU WENGI ZAIDI KUPITIA RADIO
  • “ADV”
  • KAZI YA MAANA
  • 1919—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • 1924​—⁠Kumepita Miaka Mia Moya Sasa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • 1921—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Watu Wanaofanya Kazi ya Kuhubiri—Wahubiri Wanajitoa kwa Kupenda
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
w22 Mwezi wa 10 uku. 2-5
Jukwaa kwenye mukusanyiko wa 1922. Juu ya jukwaa kuko kitambala yenye kuwa na maneno: “Mutangaze Mufalme na Ufalme wake.” Nyuma ya jukwaa kuko herufi “ADV.”

Picha ya karibu yenye kuonyesha jukwaa na kitambala yenye maandishi juu ya jukwaa

1922—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa

“MUNGU . . . anatupatia ushindi kupitia Bwana wetu Yesu Kristo.” (1 Ko. 15:57) Ile maneno yenye ilichaguliwa kuwa andiko ya mwaka wa 1922, ilihakikishia Wanafunzi wa Biblia kama Yehova atawabariki juu ya uaminifu wao. Mu ule mwaka, Yehova alibariki wale wahubiri wenye bidii. Aliwabariki wakati wao wenyewe walianza kuchapisha na kutia pamoya kurasa za vitabu vyao na kutumia radio juu ya kutangaza kweli za Ufalme. Kisha, mu 1922, ilionekana tena wazi kama Yehova alikuwa nabariki watu wake. Wanafunzi wa Biblia waliweza kukutana pamoya ku mukusanyiko wa maana sana wenye ulifanyika Cedar Point, Ohio, Amerika. Mambo yenye ilifanyika ku ule mukusanyiko ilikuwa na matokeo ya muzuri juu ya tengenezo ya Yehova mupaka leo.

“WAZO YA MUZURI SANA”

Wakati watu wengi sana walianza kuhubiri, ndugu na dada walikuwa na lazima ya vichapo mingi zaidi. Ndugu ku Beteli ya Brooklyn walikuwa nachapisha magazeti. Lakini, walikuwa wangali natumia kompanyi za kuchapisha juu ya kuchapisha vitabu vyenye kuwa na jalada ya nguvu. Kisha, kwa miezi mingi, ile kompanyi haikuweza kuchapisha vitabu mingi vyenye wangeweza kutumia mu kazi ya kuhubiri. Njo maana, Ndugu Rutherford aliuliza Robert Martin, mwenye kusimamia izine, ikiwa anawaza kama wangeweza kuchapisha vitabu wao wenyewe.

Barabara ya izine ya Concord Street katika Brooklyn, New York

Ndugu Martin anakumbuka hivi: “Ilikuwa wazo ya muzuri sana juu ile ilimaanisha kama tulipaswa kufungula izine yetu ya kuchapisha vitabu.” Ndugu walianza kulipia nafasi ku 18 Concord Street mu Brooklyn na walipata vyombo vyote vyenye walikuwa navyo lazima.

Haiko kila mutu njo alifurahi kuona vile ndugu wangeanza kuchapisha vichapo wao wenyewe. Musimamizi wa kompanyi fulani yenye ilikuwa nachapisha vichapo vyetu alitembelea izine yetu ya mupya. Alisema hivi: “Muko na vyombo vya muzuri sana vya kuchapisha vitabu lakini hakuna hata mutu moya mwenye anajua namna ya kuvitumia. Mu miezi sita vyote vitaharibika.”

Ndugu Martin alisema hivi: “Ilionekana sawa vile ule musimamizi alisema kweli.” Kisha aliongezea hivi: “Lakini tulijua kama Yehova atatusaidia na ni vile njo alifanya.” Ndugu Martin alikuwa na sheria. Kisha tu wakati kidogo, ile izine ya mupya ilikuwa nachapisha vitabu 2 000 kwa siku.

Wenye kuchapisha wamesimama karibu na mashini zao za kuchapisha mu izine

KUHUBIRIA WATU WENGI ZAIDI KUPITIA RADIO

Zaidi ya kujichapishia vitabu vyao fulani, watu wa Yehova walianza kutumia njia ya mupya ili kueneza habari njema, ni kusema, radio. Siku ya Yenga kisha midi, tarehe 26, Mwezi wa 2, 1922, Ndugu Rutherford alisema ku radio kwa mara ya kwanza. Alitoa hotuba yenye kichwa: “Mamilioni ya Watu Wenye Wanaishi Sasa Hawatakufa Hata Kidogo” ku radio KOG mu Los Angeles, Californie, Amerika.

Watu karibu 25 000 walisikia ile hotuba. Wamoja walituma barua za kumushukuru Ndugu Rutherford. Barua moya ilikuwa ya Willard Ashford, mwenye alikuwa anaishi Santa Ana, Californie. Alimushukuru Ndugu Rutherford juu ya hotuba yenye “kufurahisha na yenye kupendeza.” Kisha, aliongezea hivi: “Mu nyumba yangu, watu tatu walikuwa wagonjwa na hawangeweza kutoka ku nyumba. Njo maana, hatungeweza kuya kusikiliza hotuba hata kama ingefanywa fasi ya karibu sana.”

Hotuba zingine zilitolewa mu majuma yenye kufuata. Ku mwisho wa 1922, Munara wa Mulinzi ulionyesha kama “watu karibu 300 000 walisikiliza ujumbe kupitia radio.”

Juu Wanafunzi wa Biblia walitiwa moyo na barua na mambo yenye watu walisema kisha kufuata zile hotuba, waliamua kujenga radio mu Staten Island karibu na Beteli ya Brooklyn. Mu miaka yenye ilifuata, Wanafunzi wa Biblia wangeweza kutumia ile radio, WBBR, juu ya kusaidia watu wengi zaidi wasikie ujumbe wa Ufalme.

“ADV”

Tarehe 15, Mwezi wa 6, 1922, Munara wa Mulinzi ulitangaza kama mukusanyiko mukubwa ungefanywa Cedar Point, Ohio, kuanzia tarehe 5 mupaka tarehe 13, Mwezi wa 9, 1922. Wanafunzi wa Biblia walifurahi sana wakati walifika Cedar Point.

Mu hotuba yake ya kwanza, Ndugu Rutherford aliambia wasikilizaji hivi: “Niko hakika kabisa kama Bwana . . . atabariki huu mukusanyiko na ushahidi mukubwa utatolewa, ushahidi wenye hauyatolewaka hapa ku dunia.” Ku ule mukusanyiko, wasemaji walitia sana moyo ndugu na dada kuhubiri habari njema.

Watu wengi ku mukusanyiko wenye ulifanyika Cedar Point, Ohio, mwaka wa 1922

Kisha, Siku ya Tano, tarehe 8, Mwezi wa 9, watu karibu 8 000 walifika ku jumba kwenye mukusanyiko ulipaswa kufanywa, na walichunga kwa hamu kusikiliza hotuba ya Ndugu Rutherford. Waliwaza kama atawafasiria maana ya herufi “ADV,” zenye zilikuwa zimechapwa ku mialiko yao. Wakati waliikala, wengi kati yao waliona kitambala ya murefu juu ya jukwaa. Arthur Claus, mwenye alikuwa amesafiri kutoka Tulsa, Oklahoma, Amerika, juu ya kuya ku mukusanyiko, alipata kiti fasi kwenye angeweza kusikiliza muzuri hotuba. Ile wakati, ilikuwa nguvu sana kusikia sauti juu hakukuwa mikrofone ao vikuza-sauti.

“Tulikuwa nasikiliza kwa uangalifu kila neno”

Juu kusikuwe mutu wa kukatiza hotuba, mwenyekiti wa programu alitangaza kama hakuna mutu mwenye kuchelewa mwenye ataruhusiwa kuingia mu jumba wakati Ndugu Rutherford iko natoa hotuba. Saa tatu na dakika makumi tatu ya asubui (9:30), Ndugu Rutherford alianza hotuba kwa kutaya maneno ya Yesu yenye inapatikana mu Matayo 4:17: “Ufalme wa mbinguni umekaribia.” Wakati alikuwa nazungumuzia namna wanadamu wangesikia habari ya Ufalme, alisema hivi: “Yesu mwenyewe alisema kama wakati ya kuwapo kwake angeongoza kazi kubwa ya kuvuna watu wake, ni kusema, angekusanya wafuasi wake wa kweli na waaminifu.”

Ndugu Claus, mwenye alikuwa naikala mu jumba ya kwanza, anasema hivi: “Tulikuwa nasikiliza kwa uangalifu kila neno.” Lakini kisha wakati kidogo, alijisikia mubaya na alilazimika kutoka mu jumba. Claus alitoka bila kupenda juu alijua kama hangeruhusiwa kurudia ndani wakati ya hotuba ya Rutherford.

Kisha dakika fulani, alianza kujisikia muzuri. Alisema kama wakati alikuwa narudia mu jumba, alisikia watu wako napiga mikono. Ile ilifanya afurahi sana! Aliamua kama atasikiliza sehemu ya mwisho ya ile hotuba ya muzuri sana, hata kama itamuomba kupanda kwenye sehemu ya juu ya jumba. Ndugu Claus, mwenye ile wakati alikuwa na miaka 23, aliweza kupanda kwenye sehemu ya juu ya ile jumba. Madirisha kwenye sehemu ya juu ya ile jumba ilikuwa wazi, na alisema kama wakati aliikaribia, aliweza “kusikia muzuri hotuba.”

Lakini Arthur hakukuwa yeye peke. Marafiki wake fulani walikuwa pia kwenye sehemu ya juu ya ile jumba. Mumoja kati yao, Frank Johnson, alienda haraka karibu naye na kumuuliza, “Uko na kisu ya kidogo?”

Arthur akamujibu, “Ndiyo.”

Frank akamuambia, “Weye njo jibu ku sala zetu. Unaona ile kitambala ya murefu? Iko na maandishi fulani na imepigiliwa na hii misumari. Usikilize kwa uangalifu mambo yenye Muamuzia anasema. Wakati mutasikia anasema, ‘na munapaswa kutangaza, kutangaza,’ palepale mukate hizi kamba ine.”

Kwa hiyo, Arthur, alikamata kisu yake mu mikono na alichunga pamoya na marafiki wake wakati atasikia Ndugu Rutherford anasema ile maneno yenye waliwaambia juu waweze kukata zile kamba. Ndugu Rutherford alifika ku wakati ya maana sana ya hotuba yake. Alikuwa na furaha sana na alichangamuka sana, na pengine alisema hivi kwa sauti kubwa: “Mukuwe mashahidi waaminifu na wa kweli wa Bwana. Muendelee mbele katika vita mupaka wakati Babiloni mukubwa itaharibiwa kabisa. Mutangaze ujumbe fasi yote. Dunia inapaswa kujua kama Yehova njo Mungu na kama Yesu Kristo njo Mufalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. Leo ni siku ya maana sana. Muangalie, Mufalme anatawala! Muko na mugao wa kuambia kila mutu kuhusu ile jambo. Kwa hiyo, mutangaze, mutangaze, mutangaze, Mufalme na Ufalme wake!”

Arthur alieleza kama yeye na ndugu wengine walikata zile kamba na wakashusha polepole ile kitambala yenye maandishi. Kulingana na herufi “ADV,” ku ile kitambala kulikuwa hii maneno: “Mutangaze Mufalme na Ufalme wake.” “ADV” ilikuwa kifupi ya maneno ya Kiingereza ‘advertise’ yenye inamaanisha kutangaza, ao kuhubiri.

KAZI YA MAANA

Mukusanyiko wenye ulifanyika Cedar Point ulisaidia ndugu wakaze akili juu ya kazi ya maana sana ya kuhubiri Ufalme, na wale wenye walikuwa na moyo tayari walifurahia kuhubiri. Kolportere moya (sasa anaitwa painia) wa Oklahoma, Amerika, aliandika hivi: “Tulihubiri mu eneo kwenye watu wengi walikuwa natumika fasi ya kuchimbula makala ao charbon na walikuwa maskini sana.” Alisema kama, mara mingi wakati watu walikuwa nasikia ujumbe wenye kupatikana mu gazeti L’Âge d’Or, “walikuwa nalia.” Alisema, “Tulikuwa na furaha sana juu tuliweza kuwafariji.”

Wale Wanafunzi wa Biblia walijionea kama maneno ya Yesu mu Luka 10:2 ni ya kweli: “Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi wako kidogo.” Kadiri mwaka wa 1922 ulikaribia mwisho, Wanafunzi wa Biblia waliazimia hata zaidi kutangaza ujumbe wa Ufalme fasi yote.

a Wakati fulani, Ndugu Rutherford alikuwa naitwa “Muamuzi” juu kuko wakati alitumikaka sawa vile muamuzi mu Missouri, Amerika.

Kutoa Ushahidi mu Dunia Yote

Tarehe 26, Mwezi wa 2, 1922, Wanafunzi wa Biblia walijikaza “kutoa ushahidi mu dunia yote.” Mu dunia yote, walifanya mikutano ya pekee kwenye watu waliweza kusikia hotuba yenye kichwa “Mamilioni ya Watu Wenye Wanaishi Sasa Hawatakufa Hata Kidogo.”

Ile hotuba ilitafsiriwa mu luga karibu 33, na Munara wa Mulinzi ulionyesha kama karibu kila musemaji mwenye kustahili alitumiwa ili kutoa ile hotuba. Wanafunzi wa Biblia mu Uingereza walifanya mikutano 306, na watu 67 010 walihuzuria. Mu Belgique, Ufaransa, na Uswisi, watu zaidi ya 15 000 wenye kuzungumuza Kifaransa walihuzuria ile mikutano. Wakati Wanafunzi wa Biblia waliona namna watu wengi walihuzuria ile mikutano, walipanga siku za kufuatana za “kutoa ushahidi mu dunia yote,” ni kusema, tarehe 25, Mwezi wa 6, tarehe 29, Mwezi wa 10, na tarehe 10, Mwezi wa 12, 1922.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine