Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w24 Mwezi wa 10 uku. 2-5
  • 1924​—⁠Kumepita Miaka Mia Moya Sasa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 1924​—⁠Kumepita Miaka Mia Moya Sasa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • WANAJENGA KITUO YA RADIO
  • BALIONYESHA WAZIWAZI MAKOSA YA WAKUBWA WA DINI
  • WANAFUNZI WA BIBLIA WALIHUBIRI KWA UHODARI MU INCHI ZINGINE
  • KUFANYA KAZI MINGI ZAIDI
  • 1925​—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • 1922—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • 1919—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Njia Mbalimbali Zilizotumiwa Ili Kuhubiri—Kutumia Kila Njia Ili Kuhubiria Watu
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
w24 Mwezi wa 10 uku. 2-5

1924​—⁠Kumepita Miaka Mia Moya Sasa

BULLETIN ya Mwezi wa 1, 1924 ilisema hivi: “Mwanzo wa mwaka ni wakati wa muzuri kwa kila mutumishi wa Bwana mwenye kujitoa kwake . . . kutafuta nafasi ya kufanya mambo mingi mu kazi yake.”a Wakati mwaka iliendelea Wanafunzi wa Biblia walitumikisha ile shauri mu njia mbili: Kwanza walitenda kwa uhodari, na pili walihubiri bila woga.

WANAJENGA KITUO YA RADIO

Kwa zaidi ya mwaka moya bandugu ku Beteli balikuwa natumika sana juu ya kujenga kituo ya radio WBBR mu kisiwa ya Staten, New York City. Kisha kukata miti mu kiwanja, balijenga nyumba kubwa kwa ajili ya batu benye bangetumika pale na balijenga nyumba ingine ya kutumikia ndani. Wakati balimaliza ile kazi, balianza kutia pamoya vitu vyenye balikuwa navyo lazima juu radio ianze kutumika. Lakini balikutana na magumu ya mingi.

Bandugu baliona kama ilikuwa nguvu sana kusimamisha antene ya radio. Ile antene ya urefu wa metre 91 ilipaswa kusimama katikati ya miti mbili, na kila muti ulikuwa na urefu wa metre 61. Balipima kuisimamisha mara ya kwanza lakini balishindwa. Balimutegemea Yehova na ku mwisho baliweza kuisimamisha. Ndugu Calvin Prosser, mwenye alitumika ku ile kituo alisema hivi: “Kama tungeweza kusimamisha ile antene wakati tulipima kwa mara ya kwanza, tungeweza kujisifu na kusema ‘angalia mambo yenye tunafanya!’” Ndugu walimutolea Yehova sifa juu ya mambo yote yenye waliweza kufanya. Lakini magumu ilikuwa ingali.

Tuko tunasimamisha antene ku kituo ya WBBR

Ile wakati teknolojia ya mambo ya radio ilikuwa ingali ya mupya, na ilikuwa nguvu kupata vitu vya kutumikisha juu radio ianze kutumika. Lakini ndugu walipata vitu vyenye vilikuwa vilishatumikishwa vyenye mutu fulani wa mu ile eneo alikuwa ametengeneza. Kuliko kuuza mikro balitumikisha mikro ya telefone. Usiku moya ya mu Mwezi 2, bandugu baliamua kupima vile vyombo. Balikuwa na lazima ya programu yenye batapitisha ku radio, kwa hiyo baliamua kuimba nyimbo za Ufalme. Ernest Lowe alikumbuka kwa kicheko mambo yenye ilitokea wakati bandugu balikuwa naimba. Muamuzi Rutherfordb aliita; alikuwa Brooklyn, ku kilometre 25 hivi, kutoka pale. Alisikia ku radio yake namna bandugu balikuwa naimba.

Ndugu Rutherford alibaambia hivi: “Muache ile makelele, sauti zenu ziko nasikilika sawa za mapusi.” Bandugu balisikia haya na bakakata mara moya radio. Lakini balikuwa hakika kama balikuwa tayari kupitisha programu yao ya kwanza ku radio.

Tarehe 24 Mwezi wa 2, 1924, wakati balitumikisha ile radio kwa mara ya kwanza, Ndugu Rutherford alisema kama ile radio itatumiwa “ili kufanya kazi yenye Kristo Mufalme ametupatia.” Alisema kama kusudi ya ile radio ilikuwa “kusaidia batu baelewe Biblia, na baelewe kama tuko naishi mu kipindi ya maana sana.”

Kushotoo: Ndugu Rutherford mu studio ya kwanza

Kuume: Vyombo vya kusaidia kupitisha habari ku radio

Programu ya kwanza ya radio ilipita muzuri sana. Miaka 33 yenye ilifuata kituo ya radio WBBR ilitumiwa juu ya kupitisha programu mbalimbali za batu ya Yehova.

BALIONYESHA WAZIWAZI MAKOSA YA WAKUBWA WA DINI

Mu Mwezi wa 7, 1924, Wanafunzi wa Biblia walifanya mukusanyiko mu Columbus, Ohio. Batu kutoka mu dunia yote balisikiliza hotuba mu Kiarabu, Kiingereza, Kifaransa, Kijerumani, Kigiriki, Kihongria, Kiitaliano, Kilituania, Kirusi, mu luga za Kiskandinavia, na pia mu luga ya Polonye na Ukrene. Sehemu fulani za ile mukusanyiko zilipitishwa ku radio na mipango ilifanywa juu gazeti Ohio State Journal itoe ripoti ya kila siku ya ile mukusanyiko.

Mukusanyiko wa 1924 Columbus, Ohio

Siku ya Ine tarehe 24, Mwezi wa 7 batu zaidi ya 5000 benye balikuwa ku mukusanyiko balienda mu mahubiri. Balipatia batu vitabu 30000 na balianzisha maelfu ya mafunzo ya Biblia. Munara wa Mulinzi uliita ile siku, “siku ya furaha zaidi ya mukusanyiko.”

Sehemu ingine ya maana zaidi ya mukusanyiko ilikuwa Siku ya Tano, tarehe 25, Mwezi wa 7, wakati ndugu Rutherford alisoma dokima fulani yenye ilionyesha waziwazi makosa ya viongozi wa dini. Ile dokima ilishitaki viongozi wa mambo ya politike, wakubwa wa dini, na wakubwa mu mambo ya biashara kwa kusema kama “walikuwa nazuia watu wasijifunze juu ya Ufalme wa Mungu, wenye Mungu atatumia juu ya kubariki wanadamu.” Zaidi ya ile aliwashitaki pia kama walikosea “kwa kuunga mukono Muungano wa Mataifa na juu walisema kama ulikuwa ‘njia ya Mungu ya kutawala.’” Wanafunzi wa Biblia walipaswa kuwa hodari ili kutangazia watu ile ujumbe.

Munara wa Mulinzi ulisema hivi juu ya matokeo ya ule mukusanyiko: “Kikundi kidogo ya batumishi ya Bwana benye balikuwa ku mukusanyiko wa Columbus balirudia na imani yenye nguvu . . . , hakuna mamlaka ao upinzani wowote wenye ungeweza kuwaogopesha.” Ndugu Leo Claus, mwenye alikuwa ku ule mukusanyiko alikumbuka hivi: “Tulitoka ku ule mukusanyiko na tuko na hamu sana ya kupatia batu ya mu eneo yetu ile dokima.”

Kopie ya trakte Makasisi Washtakiwa

Mu Mwezi wa 10, Wanafunzi wa Biblia walianza kupatia watu mamilioni ya kopi ya trakte Makasisi Washtakiwa (Ecclesiastics Indicted), yenye ilikuwa na ujumbe wenye ndugu Rutherford alisoma juu ya kuonyesha makosa ya wakubwa wa dini. Mu muji mudogo wa Cleveland, Oklahoma, Frank Johnson alimaliza kupatia watu trakte dakika 20 mbele ya wakati wenye wahubiri wenzake walipaswa kumukamata. Hangesimama fasi ya wazi ili kungoya wahubiri wenzake juu wanaume wa mu ule muji wenye walikasirika kwa sababu ya mahubiri yake walikuwa wanamutafuta. Ndugu Johnson aliamua kujificha mu kanisa yenye ilikuwa karibu na pale. Wakati aliingia mu ile kanisa hakukuta mutu, kwa hiyo alitia kopi ya trakte Makasisi Washtakiwa mu Biblia ya muhubiri na ku kila kiti. Na akatoka mu ile kanisa mbio sana. Alikuwa angali na wakati, kwa hiyo alifanya vilevile mu kanisa zingine mbili.

Kisha Frank akarudia mbio fasi yenye wahubiri wenzake walipaswa kumukamata. Alijificha nyuma ya fasi ya kuuzishia carburant, juu wale wanaume wenye walikuwa namutafuta wasimuone. Wale wanaume walipita mu gari lakini hawakumuona. Na kisha tu pale wahubiri wenzake wenye walikuwa nahubiri karibu na pale, walifika kumukamata na wakaondoka.

Mumoya kati ya wale wahubiri alisema hivi: “Wakati tulikuwa natoka mu muji tulipita ku zile kanisa tatu. Ku kila kanisa kulikuwa watu 50 hivi wenye walikuwa nasimama inje. Wamoya walikuwa nasoma ile trakte na wengine walikuwa naionyesha muhubiri. Tuliponyoka kabisa! Na tulimushukuru Yehova juu alitusaidia kutolea watu ile ujumbe bila kukamatwa.”

WANAFUNZI WA BIBLIA WALIHUBIRI KWA UHODARI MU INCHI ZINGINE

Józef Krett

Mu inchi zingine, Wanafunzi wa Biblia waliendelea kuhubiri kwa uhodari. Kaskazini mwa Ufaransa, Józef Krett alihubiria bafanyakazi kutoka Polanye benye balikuwa natumika mu kariere. Alipanga kutoa hotuba yenye kichwa “Ufufuo wa Wafu Uko Karibu.” Wakati ndugu na dada balianza kupatia batu mu ile eneo mialiko, padiri moya wa kule aliambia batu ya mu kanisa yake basiende kusikia ile hotuba. Lakini haiko vile alipenda njo vile mambo ilikuwa. Batu zaidi ya 5000 balikuya kusikiliza ile hotuba, na ule padiri pia alikuya! Ndugu Krett alimuomba ule padiri atetee imani yake, lakini alikatala. Ndugu Krett alitolea batu vichapo vyote vyenye alikuwa navyo juu aliona kama batu benye alitoleo ushahidi balikuwa na hamu kabisa ya Neno ya Mungu.—Amo. 8:11.

Claude Brown

Mu Afrika, Claude Brown alipeleka habari njema mu inchi ya Gold Coast, yenye leo inaitwa Ghana. Vichapo na hotuba zenye alitoa vilisaidia habari njema ienee haraka mu ile inchi. John Blankson, mwenye alikuwa nasomea mambo yenye kuhusu dawa (mambo ya pharmacie) alisikia hotuba moya ya ndugu Brown. Mara moya alielewa kama amepata kweli. John alikumbuka hivi: “Nilifurahia sana kweli yenye nilisikia na niliizungumuzia ku masomo yetu.”

John Blankson

Siku moya, John alienda kutembelea kanisa fulani ya Anglikani ili kuuliza padiri maulizo kuhusu Utatu, juu sasa alijua kama ile fundisho haipatane na Maandiko. Padiri alimufukuza na kumulalamikia hivi: “Hauko Mukristo, uko mutu wa Shetani, toka hapa!”

Wakati alifika ku nyumba, John aliandikia ule padiri barua na kumualika akuye kutetea fundisho ya Utatu mbele ya batu mingi. Ule padiri alimuambia John aende kwa mwalimu mwenye alikuwa nasimamia masomo. Ule mwalimu alimuuliza John ikiwa aliandikia padiri barua.

John alijibu hivi: “ Ndiyo, nilimuandikia.”

Ule mwalimu alimuomba John amuandikie padiri barua ya kuomba musamaha. Kwa hiyo John aliandika hivi:

“Padiri, mwalimu wangu ananiomba nikuandikie barua ya kuomba musamaha, na niko tayari kukuandikia kama tu unakubali kama uko nafundisha mambo ya bongo.”

Mwalimu alishangala sana na akauliza: “Blankson, njo hivi unapenda kuandika?”

“Ndiyo mwalimu, hii tu njo naweza kuandika.”

“Tutakufukuza ku hii masomo. Hauwezi kuendelea kuwa ku hii masomo kama uko nasema mubaya juu ya padiri wa kanisa yenye serikali inakubali.”

John alijibia hivi: “Lakini mwalimu, . . . wakati uko natufundisha na kuko mambo yenye hatuelewe, si tunakuulizaka maulizo?”

“Ndiyo njo vile munafanyaka.”

“Mwalimu ile njo mambo yenye ilitokea. Padiri alikuwa natufundisha Biblia na nikamuuliza maulizo. Kama anashindwa kujibia juu ya nini nimuandikie barua ya kuomba musamaha?”

Blankson hakufukuzwa ku masomo na hakuandika barua ya kuomba musamaha.

KUFANYA KAZI MINGI ZAIDI

Munara wa mulinzi ulisema hivi juu ya kazi ya ile mwaka: “Tunaweza kusema hivi kama Daudi: ‘Utanipatia nguvu kwa ajili ya vita.’ (Zaburi 18:39) Hii mwaka imekuwa na mambo mingi yenye kutia moyo sana juu tumeona mukono wa Bwana . . . Watumishi wake waaminifu . . . wamefurahia sana kutoa ushahidi.”

Ku mwisho-mwisho wa mwaka, bandugu balianza kutumika juu ya kufungula kituo ingine ya radio karibu na Chicago. Ile kituo ya mupya iliitwa WORD yenye kumaanisha NENO, juu bangetumia ile kituo ili kutangaza Neno ya Mungu. Ku ile kituo balitumia vyombo vya hali ya juu ili kusaidia batu mingi zaidi benye kuwa mbali kusikia ujumbe wa Ufalme; hata benye kuwa mu sehemu ya kaskazini ya Kanada.

Mu mwaka wa 1925 kungekuwa mwangaza wa kiroho, ni kusema Wanafunzi wa Biblia wangeelewa muzuri zaidi Ufunuo sura ya 12. Ile mafasirio ingefanya Wanafunzi fulani wa Biblia waache kumutumikia Yehova. Lakini wengi walifurahi kuelewa muzuri zaidi mambo yenye ilitokea mbinguni, na matokeo yenye ile mambo ilikuwa nayo juu ya watumishi wa Mungu ku dunia.

a Leo inaitwa Buku ya Mukutano—Utumishi na Maisha ya Mukristo.

b J. F. Rutherford, mwenye alikuwa nasimamia kazi ya Wanafunzi wa Biblia ile wakati alijulikana kuwa Mwamuzi Rutherford. Mbele akuye ku Beteli, kwa wakati fulani alikuwa mwamuzi ku tribinali fulani ya Missouri.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine