Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 10 uku. 2-5
  • 1925​—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 1925​—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAMBO YENYE BALIKUWA NACHUNGA HAIKUFIKA
  • VITUO VYA RADIO VINAONGEZEKA
  • MAFASIRIO YA MUPYA
  • KUTOA USHAHIDI JUU YA YEHOVA
  • KURUDILIA BENYE KUPENDEZWA
  • KUANGALIA MBELE
  • 1924​—⁠Kumepita Miaka Mia Moya Sasa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • 1922—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Njia Mbalimbali Zilizotumiwa Ili Kuhubiri—Kutumia Kila Njia Ili Kuhubiria Watu
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 10 uku. 2-5
Bandugu na dada ba mingi biko inje biko nakatamata picha ku mukusanyiko wa 1925 mu muji wa Indianapolis, Indiana.

Mukusanyiko wa eneo mu muji wa Indianapolis, Indiana, 1925

1925​—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa

MUNARA WA MULINZI wa tarehe 1 Mwezi wa 1, 1925 ilisema hivi: “Bakristo bamengoya kwa hamu hii mwaka.” Lakini, ile habari iliongezea hivi: “Bakristo habapaswe kuhangaikia sana mambo yenye inaweza kutokea hii mwaka mupaka bashindwe kufanya kazi yenye Bwana anapenda bafanye.” Banafunzi ya Biblia balikuwa nangoya nini itokee mu mwaka wa 1925? Na namna gani baliendelea kufanya kazi ya Bwana kwa bidii hata kama mambo yenye balikuwa natumainia itafika haikufika?

MAMBO YENYE BALIKUWA NACHUNGA HAIKUFIKA

Mu 1925 Banafunzi ya Biblia bamingi balikuwa nawaza kama ile mwaka dunia itageuka na kuwa tena Paradiso. Juu ya nini baliwaza vile? Ndugu Albert Schroeder, mwenye alifikia kutumika mu Baraza Yenye Kuongoza, anafasiria hivi: “Banafunzi ya Biblia baliwaza kama ile mwaka mabaki ya Bakristo batiwa-mafuta bangeenda mbinguni juu ya kutawala mu Ufalme, na banaume baaminiifu ba zamani sawa vile Abrahamu, Daudi na bengine, bangefufuliwa juu ya kutawala ku dunia.” Wakati ile mambo haikufika, bandugu na badada fulani balivunjika moyo.—Mez. 13:12.

Hata kama mambo yenye balikuwa nangoya haikufika, Banafunzi mingi ya Biblia baliendelea kuhubiri kwa bidii na balielewa kama kazi ya kuhubiri njo ilikuwa ya maana zaidi. Kwa mufano, tuone namna balitumia radio juu ya kuhubiria batu mingi.

VITUO VYA RADIO VINAONGEZEKA

Juu mu 1924 batu mingi balisikiliza radio WBBR, mu 1925 Banafunzi ya Biblia balijenga ingine kituo ya radio, sasa balijenga karibu na Chicago, mu Illinois. Jina ya ile radio ilikuwa WORD. Ralph Leffler, mwenye alisaidia kujenga ile kituo ya radio, alisema hivi: “Mangaribi mu kipindi ya baridi, batu mingi ba mbali balikuwa nasikiliza radio WORD.” Kwa mufano, familia moya yenye ilikuwa naishi ku kilometre zaidi ya 5000 mu muji wa Pilot, mu Alaska, ilisikiliza programe moya kati ya programe za kwanza-kwanza za radio WORD. Kisha kusikiliza ile programe, ile familia iliandikia benye balikuwa natumika ku ile radio barua ili kubashukuru juu ya ile programe ya kiroho yenye kutia moyo.

Left: Antene za radio WORD mu Batavia, Illinois

Right: Ralph Leffler iko natumika ku kituo ya radio

Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 12 ,1925, ilisema hivi kuhusu ile radio: “WORD ni kati ya radio za mu Amerika zenye ziko nafika mbali sana. Iko nafika mu Amerika yote na hata mu sehemu ya mbali sana ya Alaska. Batu mingi benye habayasikiaka kweli banapenda kujua mambo mingi zaidi juu biko nasikiliza hii radio.”

George Naish

Ileile wakati, Banafunzi ya Biblia balipenda kutumikisha sana radio juu ya kuhubiri habari njema mu Kanada. Mu 1924 kituo ya radio yenye kuitwa CHUC ilijengwa Saskatoon mu muji wa Saskatchewan. Ilikuwa kati ya radio za kwanza-kwanza mu Kanada zenye zilikuwa nazungumuzia mambo ya Biblia. Mu 1925 balipaswa kuhamishia ile kituo fasi ya munene zaidi. Kwa hiyo tengenezo iliuza jengo moya ya zamani mu Saskatoon, ikaitengeneza na kisha ikahamisha ile kituo ya radio mu ile jengo.

Ile radio ilisaidia batu mingi benye balikuwa naishi mu miji ya kidogo-kidogo na mu bijiji bya mbali bya Saskatchewan basikie habari njema kwa mara ya kwanza. Kwa mufano, mu muji fulani wa mbali, mwanamuke moya aliandika juu ya kulomba bichapo kisha kusikiliza ile radio. Ndugu George Naish anakumbuka hivi: “Ombi yake ilionekana kuwa ya haraka sana, mupaka bila kukawia tukamutumia buku zote za kitabu Études des Écritures.” Ule mwanamuke alianza kutangaza habari njema ya Ufalme mupaka mu maeneo ya mbali.

MAFASIRIO YA MUPYA

Mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 3, 1925, mulikuwa habari moya ya pekee yenye kichwa “Kuzaliwa kwa Taifa.” Juu ya nini ile habari ilikuwa ya maana sana? Ile wakati Banafunzi ya Biblia balijua kama Shetani iko na tengenezo yake yenye inafanyizwa na pepo wachafu mbinguni, na ku dunia mashirika ya kidini, kibiashara, na kipolitike. Lakini, kupitia ile habari, “mutumwa muaminifu na mwenye busara” alisaidia bandugu baelewe kama Yehova naye iko na tengenezo yake yenye iko tofauti kabisa, na inapingana na tengenezo ya Shetani. (Mt. 24:45) Zaidi ya ile, mutumwa alifasiria kama Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mu mwaka wa 1914 na kama mu ile mwaka, kisha vita yenye ilitokea mbinguni, Shetani na mashetani wake balifukuzwa mbinguni na sasa biko ku dunia.—Ufu. 12:​7-9.

Ilikuwa nguvu kwa Bakristo fulani kuitika ile mafasirio ya mupya. Njo maana mu ile habari mulikuwa hii shauri: “Tunapendekeza kama kila mutu mwenye hakubaliane na hii mafasirio ya mupya, akuwe muvumilivu, aendelee kumutumainia Yehova, na kumutumikia kwa uaminifu.”

Tom Eyre, painia kutoka Uingereza, alieleza namna Banafunzi mingi ya Biblia balijisikia kisha kusoma ile habari: “Bandugu balifurahia ile mafasirio ya Ufunuo 12. Wakati tulielewa kama Ufalme ulishaanza kutawala mbinguni, ile ilituchochea tutangazie bengine habari njema. Ilituchochea tuongeze bidii yetu mu kazi ya Yehova, na ilitusaidia tuelewe kama Yehova atafanyia batu yake mambo ya ajabu wakati wenye kuya.”

KUTOA USHAHIDI JUU YA YEHOVA

Leo, Mashahidi wa Yehova wanajua muzuri maneno ya Isaya 43:10: “‘Muko mashahidi wangu,’ ni vile Yehova anasema, ‘Ndiyo, mutumishi wangu mwenye nimechagua.’” Mbele ya 1925, ile andiko haikutumiwa sana mu bichapo yetu. Lakini mambo ilibadilika, juu mu 1925, magazeti 11 ya Munara wa Mulinzi ilizungumuzia Isaya 43:10 na 12!

Ku mwisho wa Mwezi wa 8, 1925, Banafunzi ya Biblia balifanya mukusanyiko wa eneo mu muji wa Indianapolis, katika Indiana. Ku programe ya mukusanyiko kulikuwa ujumbe wa kukaribisha watu, na mu ule ujumbe Joseph F. Rutherford alisema hivi: “Tumekuya ku huu mukusanyiko juu ya kupata . . . nguvu kutoka kwa Bwana juu tuweze kurudia mu shamba na nguvu ya mupya ya kuwa mashahidi wake.” Siku zote munane za ile mukusanyiko, benye balikuwa pale balitiwa moyo batumikishe kila nafasi juu ya kutoa ushahidi juu ya Yehova.

Siku ya Posho tarehe 29 Mwezi wa 8, Ndugu Rutherford alitoa hotuba yenye kichwa “Kuchochewa Kutenda.” Mu ile hotuba, alikazia kama ni jambo ya maana kutoa Ushahidi. Alisema hivi: “Yehova anaambia batu yake. . . : ‘Muko mashahidi wangu . . . mimi ni Mungu.’ Kisha Yehova anatolea batu yake hii amri kwa kutumia maneno yenye nguvu: ‘Musimamishe alama kwa ajili ya vikundi vya watu.’ Batu benye banaweza kutoa ushahidi juu ya Yehova ku dunia ni bale tu benye banaongozwa na roho yake juu ni batu yake.”—Isa. 43:12; 62:10.

Trakte yenye kuwa na azimio ya “Ujumbe wa Tumaini.”

Trakte Ujumbe wa Tumaini

Kisha hotuba yake, Ndugu Rutherford alisoma azimio yenye iliitwa “Ujumbe wa Tumaini.” Batu yote benye balikuwa ku mukusanyiko balikubaliana na ule ujumbe wenye ulionyesha kama ni Ufalme wa Mungu tu njo unatoa tumaini ya kweli ya kuleta “amani, maisha ya muzuri, afya ya muzuri, uzima, uhuru, na furaha ya milele.” Ile azimio ilifikia kutafsiriwa mu luga mbalimbali na ikachapishwa juu ikuwe trakte ili itumikishwe mu mahubiri. Banafunzi ya Biblia baligabulia batu kopi milioni 40 hivi.

Miaka fulani ilipita mbele Banafunzi ya Biblia babadilishe jina yabo na baanze kuitwa Mashahidi wa Yehova. Lakini balianza kuelewa kabisa kama ni jambo ya maana kutoa ushahidi juu ya Yehova.

KURUDILIA BENYE KUPENDEZWA

Hesabu ya Banafunzi ba Biblia iliendelea kuongezeka mu dunia yote. Kwa hiyo balitiwa moyo barudilie batu benye balipendezwa na habari njema. Kisha kampanye ya kugabulia batu ile trakte yenye kichwa Ujumbe wa Tumaini, Bulletina ilisema hivi: “Murudilie batu benye muliachia trakte Ujumbe wa Tumaini.”

Bulletin ya Mwezi wa 1, 1925 ilikuwa na hii ripoti ya Mwanafunzi wa Biblia fulani kutoka Plano, mu Texas: “Tunashangala kuona namna wakati tunarudia mu maeneo yenye tulishahubiria, tunapata matokeo ya muzuri zaidi kupita yenye tunapata wakati tunahubiria mu maeneo ya mupya. Muji fulani ya kidogo mu eneo yetu ilisharudiliwa mara tano mu miaka kumi yenye imepita. . . . Juzi-juzi, dada Hendrix na mama yangu balirudia tena mu ile muji na baliachia batu bichapo mingi kupita zamani.”

Na mu inchi ya Panama, painia moya aliandika hivi: “Batu mingi benye balikatala kunisikiliza wakati nilibatembelea kwa mara ya kwanza, baliitika kunisikiliza wakati nilibarudilia mara ya pili ao ya tatu. Hii mwaka mu mahubiri nimepitisha wakati mingi na niko narudilia batu benye nilishakahubiria, na bamoya kati yabo balipendezwa.”

KUANGALIA MBELE

Mu barua ya kila mwaka yenye Ndugu Rutherford aliandikia bahubiri bote, alizungumuzia kazi ya ile mwaka na kazi yenye ilikuwa mbele yabo. Alisema hivi: “Mu hii mwaka ya 1925 mumekuwa na pendeleo ya kufariji batu mingi benye balikuwa na huzuni. Hii kazi imetuletea furaha sana. . . . Mu mwaka yenye iko nakuya, mutakuwa na nafasi za mingi za kutoa ushahidi juu ya Mungu na Ufalme wake na kuonyesha kama muko kabisa baabudu yake. . . . Tuendelee basi kutumikisha sauti zetu juu ya kumusifu Mungu wetu na Mufalme wetu.”

Ku mwisho wa mwaka wa 1925, bandugu balikuwa nafanya mipango ya kunenepesha Beteli ya Brooklyn. Mu mwaka wa 1926 bandugu bangeanza kazi kubwa ya ujenzi yenye tengenezo ilikuwaka haiyafanya.

Bandugu biko najenga jengo ya mupya, biko nafanya kazi za mwanzo-mwanzo.

Ujenzi uko nafanywa mu Adams Street, Brooklyn, New York, 1926

a Leo inaitwa Buku ya Mukutano—Utumishi na Maisha ya Mukristo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine