Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w22 Mwezi wa 12 uku. 22-27
  • Saidia Wengine Wavumilie Magumu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Saidia Wengine Wavumilie Magumu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • SAIDIA WENGINE WAKATI KUNATOKEA MAGONJWA FULANI
  • SAIDIA WENGINE WAKATI MUSIBA UNATOKEA
  • SAIDIA NDUGU NA DADA WAVUMILIE WAKATI WANATESWA JUU YA IMANI YAO
  • Inawezekana Kuwa na Amani Hata Wakati ya Magumu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Wazee​—Muendelee Kuiga Mutume Paulo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Je, Unajitayarisha kwa Ajili ya Misiba?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Namna Kutaniko Inapangwa
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
w22 Mwezi wa 12 uku. 22-27

HABARI YA KUJIFUNZA YA 52

Saidia Wengine Wavumilie Magumu

“Usiime mema wale wenye unapaswa kutendea mema kama uko na uwezo wa kusaidia.”​—MEZ. 3:27.

WIMBO 103 Yehova Ametupatia Wachungaji

KIFUPI YA HABARIa

1. Mara mingi Yehova anatumiaka nani juu ya kujibia sala za watumishi wake?

UNAJUA kama Yehova anaweza kukutumia juu ya kujibia sala ya mutu fulani? Yehova anaweza kufanya vile ikuwe uko muzee, mutumishi wa huduma, painia, ao muhubiri wa kutaniko, kijana ao umezeeka, ndugu ao dada. Wakati mutu fulani mwenye anamupenda Yehova anamuomba amusaidie, mara mingi Yehova anatumiaka wazee ao watumishi wengine waaminifu juu wakuwe “chanzo cha faraja nyingi” kwa ule mutu. (Kol. 4:11) Ni pendeleo kabisa kumutumikia Yehova na kusaidia ndugu zetu mu ile njia! Tunaweza kufariji ndugu na dada zetu wakati kunatokea magonjwa fulani, musiba, ao wakati wanateswa juu ya imani yao.

SAIDIA WENGINE WAKATI KUNATOKEA MAGONJWA FULANI

2. Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kusaidia wengine wakati kunatokea magonjwa fulani?

2 Inaweza kuwa nguvu kusaidia wengine wakati kunatokea magonjwa fulani ya kuambukiza. Kwa mufano, tunaweza kupenda kutembelea marafiki wetu, lakini tunaona kama kufanya vile kutaweka uzima wetu mu hatari. Tunaweza kupenda kualika wale wenye wako na magumu ya kupata makuta juu tukule pamoya nao chakula, lakini ile pia haiwezekane. Tunaweza kupenda kusaidia wengine, lakini inaweza kuwa nguvu kama watu wa familia yetu ni wagonjwa. Hata vile, tunapenda kusaidia ndugu na dada zetu, na Yehova anafurahi wakati anaona tunafanya mambo yenye tunaweza ili kuwasaidia. (Mez. 3:27; 19:17) Tunaweza kufanya nini ili kuwasaidia?

3. Mufano wa wazee wa mu kutaniko ya Desi unatufundisha nini? (Yeremia 23:4)

3 Mambo yenye wazee wanaweza kufanya. Kama uko muzee, ujikaze kujua muzuri kondoo. (Soma Yeremia 23:4.) Desi, dada mwenye tulitaya mu habari yenye kutangulia, anasema hivi: “Zamani, wazee wa mu kikundi yangu ya mahubiri walikuwa nahubiri pamoya na miye na pamoya na wengine, na walikuwa najiunga na siye mu mambo ya kujifurahisha.”b Ile ilifanya ikuwe mwepesi kwa wale wazee kumusaidia Desi wakati ya ugonjwa wa Coronavirus na wakati watu fulani wa familia yake walikufa na ule ugonjwa.

4. Juu ya nini ilikuwa mwepesi kwa wazee kusaidia Desi, na ile inaweza kufundisha nini wazee?

4 Desi anasema hivi: “Juu tayari wazee walikuwa marafiki wangu, ilikuwa mwepesi kwangu kuwaambia namna nilikuwa najisikia na mambo yenye ilikuwa nanihangaisha.” Wazee wanajifunza somo gani? Muchunge wale wenye kuwa chini ya uongozi wenu mbele magumu itokee. Mukuwe marafiki wao. Kama ugonjwa fulani unawazuia kuonana nao, muzungumuze nao kupitia njia zingine. Desi anasema tena hivi: “Kuko siku yenye wazee mbalimbali waliniita na kuniandikia ujumbe. Maandiko yenye walinisomea ilinigusa sana, hata kama ni maandiko yenye najuaka muzuri.”

5. Wazee wanaweza kufanya nini juu wajue mambo yenye ndugu na dada wako nayo lazima na wanaweza kufanya nini ili kuwasaidia?

5 Kuuliza maulizo kwa busara ndugu na dada ni njia moya yenye inaweza kukusaidia kujua mambo yenye wako nayo lazima. (Mez. 20:5) Kwa mufano, wako na chakula, dawa, na mambo ingine ya lazima? Wanaweza kupoteza kazi ao hata kukosa makuta ya kulipia nyumba? Inaomba kuwasaidia ili wajue mambo ya kufanya juu wapate musaada wa serikali? Desi alisaidiwa kimwili na ndugu na dada zake. Lakini, musaada wa kihisia na wa kiroho wenye wazee walimupatia njo ulimusaidia sana avumilie magumu yake. Anasema hivi: “Wazee walisali na miye. Hata kama sikumbuke kabisa mambo yenye walisema mu ile sala, ninakumbuka namna nilijisikiaka. Ilikuwa sawa vile Yehova iko naniambia, ‘Hauko peke yako.’”​—Isa. 41:10, 13.

Picha: 1. Ndugu iko naongoza mikutano ku Jumba ya Ufalme. Anatumia tablete juu ya kuona ndugu moya mugonjwa mwenye iko nafuata mukutano kupitia vidéoconférence. 2. Ule ndugu mwenye kuzeeka mwenye iko nafuata mikutano kupitia vidéoconférence anainua mukono ili kutoa maelezo. Iko napumua oksijene yenye kuwa mu chupa.

Ndugu mwenye kuongoza sehemu moya ya mukutano anafurahi kusikia maelezo yenye kutia moyo ya ndugu na dada wengi wenye kuwa ku Jumba ya Ufalme. Anafurahi pia kumusikia ndugu mwenye kugonjwa mwenye iko natoa maelezo kupitia vidéoconférence (Ona fungu ya 6)

6. Tunaweza kufanya nini mu kutaniko ili kusaidia wengine? (Ona picha.)

6 Mambo yenye wengine wanaweza kufanya. Tuko na haki ya kutazamia kama wazee wanapaswa kuhangaikia ndugu na dada mu kutaniko. Lakini, Yehova anatuomba siye wote tutie moyo na kusaidia wengine. (Gal. 6:10) Hata kama tunafanyia mugonjwa jambo fulani ya kidogo, ile inaweza kumutia moyo sana. Kwa mufano, mutoto anaweza kutuma karte ao kuchora kitu fulani ili kutia moyo ndugu fulani. Kijana anaweza kuenda kuuzia dada fulani vitu ao kumufanyia jambo fulani. Wengine mu kutaniko wanaweza kupikia mugonjwa chakula na kumupelekea kwake. Kwa kweli, wakati ugonjwa fulani unaenea, kila mutu mu kutaniko anakuwaka na lazima ya kutiwa moyo. Tunaweza kubakia kwa dakika fulani kisha mikutano juu ya kuzungumuza na ndugu na dada, ikuwe mikutano inafanywa ku Jumba ya Ufalme ao kupitia vidéoconférence. Wazee pia wako na lazima ya kutiwa moyo. Wazee fulani wanatumikaka sana kwa ajili ya ndugu na dada wakati kunatokea magonjwa fulani ya kuambukiza, na Mashahidi fulani wamewaandikia maneno ya kuwashukuru. Inafurahisha sana wakati ‘tunaendelea kutiana moyo na kujengana’!​—1 Te. 5:11.

SAIDIA WENGINE WAKATI MUSIBA UNATOKEA

7. Musiba unaweza kuwa na matokeo gani?

7 Musiba unaweza kuvuruga maisha ya mutu mu segonde. Mutu anaweza kupoteza vitu vyake, nyumba yake, ao hata kufiwa na wapendwa. Ndugu na dada zetu wanaweza pia kufikiwa na mambo ya vile. Tunaweza kufanya nini ili kuwasaidia?

8. Wazee na vichwa vya familia wanapaswa kufanya nini mbele musiba utokee?

8 Mambo yenye wazee wanaweza kufanya. Wazee, musaidie ndugu na dada wajitayarishe mbele musiba utokee. Musaidie kila mutu mu kutaniko ajue mambo yenye anaweza kufanya juu akuwe salama na namna anaweza kuwajulisha habari fulani. Margaret, mwenye tulitaya mu habari yenye kutangulia, anasema hivi: “Mu mahitaji ya kutaniko, wazee walituonya kama moto unaweza tena kutokea mu eneo yetu. Walituambia kama, ikiwa wenye mamlaka wanasema tutoke ao kama hali inakuwa mubaya sana, tunapaswa kutoka palepale.” Maagizo yenye wazee walitolea kutaniko ilifika kwa wakati kabisa, juu kisha tu majuma tano, moto ulitokea. Vichwa vya familia, muzungumuzie mu ibada ya familia mambo yenye kila mutu anapaswa kufanya. Ikiwa weye na watoto wako munajitayarisha, ile itawasaidia kutulia wakati musiba unatokea.

9. Ni mipango gani yenye wazee wanapaswa kufanya mbele na kisha musiba?

9 Kama uko mwangalizi wa kikundi ya mahubiri, usichunge tu musiba utokee njo uanze kutafuta namba za telefone za ndugu na dada wa mu kikundi yako. Ufanye liste ya ndugu na dada wa mu kikundi yako ya mahubiri na ukuwe nachunguza kama ku ile liste kuko namba zao za sasa. Kama unafanya vile, itakuwa mwepesi kuwaita juu ya kujua mahitaji yao wakati musiba unatokea. Kisha kujua mahitaji ya ndugu na dada, ujulishe bila kukawia muratibu wa baraza ya wazee, naye ataita mwangalizi wa muzunguko. Wakati wale ndugu wanatumika pamoya, wanaweza kutoa musaada wenye unafaa kabisa. Wakati moto ulizimika, mwangalizi wa muzunguko mwenye alikuwa natembelea kutaniko mwenye Margaret alikuwa, alifanya saa 36 bila kulala usingizi, alikuwa napanga kazi yenye wazee walikuwa nafanya ya kuita na kuhangaikia ndugu na dada 450 hivi wenye walilazimika kuacha nyumba zao. (2 Ko. 11:27) Kwa hiyo, kila mutu mwenye alikuwa na lazima ya fasi ya kuishi, aliipata.

10. Juu ya nini wazee wanaonaka kazi ya uchungaji kuwa ya maana? (Yohana 21:15)

10 Wazee wako na daraka ya kutia moyo ndugu na dada na kuwafariji. (1 Pe. 5:2) Wakati musiba unatokea, wazee wanapaswa kwanza kuhakikisha kama kila ndugu na dada iko salama, iko na chakula, nguo, na fasi ya kuishi. Lakini, hata kisha miezi mingi, ndugu na dada wenye waliokoka musiba wanaweza kuwa na lazima ya kutiwa moyo na kufarijiwa kupitia maandiko. (Soma Yohana 21:15.) Harold, ndugu mwenye kutumika mu Halmashauri ya Tawi, na mwenye amekutana na ndugu na dada wengi wenye walifikiwa na misiba, anasema hivi: “Inakamataka wakati juu mutu ajisikie tena muzuri. Mutu anaweza tena kuanza kujisikia muzuri, lakini anaweza kukumbuka namna alifiwa na mupendwa, vitu vyenye alipoteza, ao namna maisha yake ilikuwa mu hatari. Wakati anakumbuka ile mambo yote, anaweza tena kuwa na huzuni. Ile haiko kukosa imani, lakini ni jambo ya kawaida kwa mwanadamu.”

11. Wazee wanapaswa kusaidia familia ziendelee kufanya nini?

11 Wazee wanatii shauri ya Biblia ya ‘kulia pamoja na wale wenye kulia.’ (Ro. 12:15) Wazee wanapaswa kuhakikishia wale wenye walifikiwa na musiba kama Yehova angali anawapenda na kama ndugu na dada zao wangali pia wanawapenda. Wazee wanapaswa kusaidia familia ziendelee kufanya mambo ya kiroho, sawa vile kusali, kujifunza, kukusanyika, na kuhubiri. Wazee wanapaswa pia kutia moyo wazazi wasaidie watoto wao wakaze akili juu ya mambo yenye musiba hauwezi kuharibisha. Wazazi, mukumbushe watoto wenu kama Yehova ataendelea kuwa rafiki yao na kama kila siku iko pale juu ya kuwasaidia. Na muwafasirie kama wako mu familia ya mu dunia yote ya ndugu na dada wenye wako tayari kuwasaidia.​—1 Pe. 2:17.

Bibi na bwana wako naletea chakula na vitu vingine vya lazima mama na mutoto wake mwanaume wenye walikimbilia fasi fulani kwa muda.

Unaweza kujitolea ili kusaidia kisha musiba kutokea mu eneo yenu? (Ona fungu ya 12)e

12. Wengine wanaweza kufanya nini ili kusaidia wakati musiba unatokea? (Ona picha.)

12 Mambo yenye wengine wanaweza kufanya. Kama musiba unatokea karibu na kwenu, omba wazee wakuambie mambo yenye unaweza kufanya ili kusaidia. Pengine unaweza kupatia wale wenye walilazimika kuacha nyumba zao ao wale wenye kusaidia mu kazi za ujenzi fasi kwenye wanaweza kuishi kwa wakati fulani. Unaweza kusaidia wahubiri wenye kuwa na lazima ya musaada kwa kuwapelekea chakula na vitu vingine vya lazima. Hata kama musiba unatokea mbali na kwenu, unaweza tu kusaidia. Utasaidia namna gani? Kwa kusali kwa ajili ya wale wenye walifikiwa na musiba. (2 Ko. 1:8-11) Unaweza kutegemeza kazi ya kutoa misaada kwa kutoa muchango kwa ajili ya kazi ya mu dunia yote. (2 Ko. 8:2-5) Kama uko na uwezo wa kusafiri mupaka fasi kwenye kulitokea musiba, omba wazee wakuambie mambo yenye unaweza kufanya ili kusaidia. Kama unaalikwa ili kusaidia, unaweza kupewa mazoezi fulani juu uweze kusaidia fasi kwenye ni lazima na wakati ni lazima kabisa.

SAIDIA NDUGU NA DADA WAVUMILIE WAKATI WANATESWA JUU YA IMANI YAO

13. Ni magumu gani yenye ndugu na dada zetu wako napambana nayo mu inchi kwenye kazi yetu imekatazwa?

13 Maisha iko nguvu sana mu inchi kwenye kazi yetu imekatazwa. Mu zile inchi, ndugu na dada wako na magumu ya kupata makuta, wako nagonjwa, na kufiwa na wapendwa. Juu kazi yetu imekatazwa, ni nguvu kwa wazee kutembelea ao kuzungumuza na wale wenye wako na lazima ya kutiwa moyo. Njo mambo yenye ilimufikia Andrei, mwenye tulizungumuzia mu habari yenye kutangulia. Alikuwa mu kikundi ya mahubiri na dada moya mwenye alikuwa na magumu ya kupata makuta. Kisha Andrei alifanya aksida ya gari. Kisha ile aksida, iliomba afanyiwe upasuaji mbalimbali, na hangeweza kufanya kazi tena. Hata kama kazi yetu ilikatazwa na hata kama kulikuwa ugonjwa wa Coronavirus, ndugu walifanya yote yenye waliweza ili kumusaidia, na Yehova alikuwa najua mambo yenye ule dada alikuwa nayo lazima.

14. Wakati kazi yetu inakatazwa, wazee wanapaswa kufanya nini?

14 Mambo yenye wazee wanaweza kufanya. Andrei alisali na alifanya yenye angeweza. Yehova alijibia sala yake? Ndiyo, alichochea ndugu na dada zake wenye walikuwa na uwezo wamusaidie. Wamoja walimupeleka wakati alienda kuonana na munganga. Wengine walitoa makuta juu imusaidie. Yehova aliwachochea kufanya mambo yenye waliweza, na alibariki mambo yenye walifanya kwa umoja ili kumusaidia. (Ebr. 13:16) Wazee, wakati kazi yetu inakatazwa, muombe wengine wawasaidie kufanya mambo fulani. (Yer. 36:5, 6) Zaidi ya yote, mumutegemee Yehova. Anaweza kuwapatia nguvu ya kusaidia ndugu na dada zetu.

15. Tunaweza kufanya nini juu tuendelee kuwa na umoja wakati kazi yetu inakatazwa?

15 Mambo yenye wengine wanaweza kufanya. Wakati kazi yetu inakatazwa, tunaweza kukutana tu na ndugu na dada zetu mu vikundi vidogo-vidogo. Kwa hiyo, ni jambo ya maana sana kuishi kwa amani na ndugu na dada zetu. Upigane na Shetani, usipigane na ndugu ao na dada yako. Usikaze akili juu ya makosa ya ndugu ao dada yako, na mumalize haraka hali yoyote ya kukosa kuelewana. (Mez. 19:11; Efe. 4:26) Mukuwe tayari kusaidiana. (Tit. 3:14) Musaada wenye wengine walipatia ule dada mwenye alikuwa na lazima ya musaada ulitia moyo wengine mu kikundi yake ya mahubiri. Ulifanya wakaribiane sana, sawa vile watu wa familia moya.​—Zb. 133:1.

16. Sawa vile Wakolosai 4:3, 18 inaonyesha, tunaweza kufanya nini ili kusaidia ndugu na dada zetu wenye kuteswa juu ya imani yao?

16 Ndugu na dada zetu wengi wako namutumikia Yehova, hata kama serikali inakataza kazi yetu. Wengine wamefungwa juu ya imani yao. Tunaweza kusali kwa ajili yao, kwa ajili ya familia zao, na kwa ajili ya wale wenye kutia uzima wao mu hatari ili kusaidia wale ndugu kiroho, kimwili, na kuwatetea ku tribinali.c (Soma Wakolosai 4:3, 18.) Usisahau kama sala zako zinaweza kusaidia!​—2 Te. 3:1, 2; 1 Ti. 2:1, 2.

Wazazi na watoto wao wawili wakati ya ibada ya familia. Ule kijana anazungumuzia jambo fulani yenye kuwa mu video “Danieli: Mwanaume wa Imani.”

Unaweza kufanya nini ili kutayarisha familia yako sasa kwa ajili ya mateso? (Ona fungu ya 17)

17. Unaweza kufanya nini ili kujitayarisha sasa kwa ajili ya mateso?

17 Weye na familia yako munaweza kujitayarisha sasa kwa ajili ya mateso. (Mdo. 14:22) Usijaribu kuwazia-wazia mambo yote ya mubaya yenye inaweza kukupata. Lakini, ufanye urafiki wako pamoya na Yehova ukuwe nguvu na usaidie watoto wako wafanye vile. Kama wakati fulani unaanza kuhangaika, umuambie Mungu mambo yote yenye kuwa mu moyo wako. (Zb. 62:7, 8) Muzungumuzie mu familia sababu zote zenye zinapaswa kutuchochea tumutumainie Yehova.d Kutayarisha watoto wako kwa ajili ya musiba kunaweza kuwasaidia sana. Vilevile, kutayarisha watoto wako kwa ajili ya mateso, kunaweza pia kuwasaidia sana. Watakuwa na amani na hawataogopa juu wamejifunza kumutumainia Yehova.

18. Ni mambo gani yenye iko natuchunga?

18 Amani ya Mungu inafanya tujisikie salama. (Flp. 4:6, 7) Kupitia ile amani, Yehova anatuliza moyo wetu wakati kunatokea magonjwa, misiba, na mateso. Anatumia wazee wenye wako wanatumika kwa bidii ili kutuchunga. Na anatupatia siye wote pendeleo ya kusaidia wengine. Amani yenye tuko nayo sasa itatusaidia kupambana na magumu ya nguvu zaidi, itatusaidia hata kupambana na “taabu kubwa.” (Mt. 24:21) Wakati ya taabu kubwa, itaomba tukuwe na amani na kusaidia wengine wakuwe nayo. Kisha taabu kubwa, magumu yenye iko natuhangaisha leo, haitakuwa tena. Tutakuwa sasa na jambo yenye Yehova amependa tangu zamani tukuwe nayo, ni kusema, amani kamilifu na ya milele.​—Isa. 26:3, 4.

UNAWEZA KUFANYA NINI ILI KUSAIDIA WENGINE WAKUWE NA AMANI HATA KAMA KUNATOKEA . . .

  • magonjwa fulani?

  • musiba?

  • mateso?

WIMBO 109 Tupendane Sana Kutoka Ndani ya Moyo

a Mara mingi Yehova anatumiaka watumishi wake waaminifu juu ya kusaidia wale wenye kuwa na magumu. Anaweza kukutumia ili utie moyo ndugu na dada zako. Tuone mambo yenye tunaweza kufanya juu ya kusaidia wengine wakati wako na lazima ya musaada.

b Majina fulani imebadilishwa.

c Haiko biro ya tawi ao ndugu wa makao makubwa njo watatuma barua yenye unaandikia ndugu na dada wenye kufungwa.

d Ona habari “Ujitayarishe Leo kwa Ajili ya Mateso” mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 7, 2019.

e MAFASIRIO YA PICHA: Bibi na bwana wanaletea chakula familia yenye ilikimbilia fasi fulani kisha musiba.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine