Mungu Anakuhangaikiaka
BIBLIA iko na mashauri ya muzuri sana juu inatoka kwa Mungu. Haiko kitabu ya matunzo, lakini inaweza kutusaidia mu njia mbalimbali tupiganishe hali zenye kuleta mahangaiko, mawazo yenye kuvunja moyo, hali ya kujisikia mubaya, na pia matatizo ya afya ya mwili na ya akili.
Jambo ya maana zaidi, Biblia inatuhakikishia kama Muumbaji wetu Yehova Mungu,a anaelewa muzuri mawazo yetu na namna tunajisikia kuliko mutu mwingine yeyote. Anapenda sana kutusaidia tupiganishe magumu yoyote yenye tunapata. Kwa mufano, fikiria hii maandiko mbili ya Biblia yenye kutia moyo:
“Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo; anaokoa wale wenye kupondwa roho.”—ZABURI 34:18.
“Mimi, Yehova Mungu wako, ninashika mukono wako wa kuume, ni mimi mwenye kukuambia, ‘Usiogope. Nitakusaidia.’”—ISAYA 41:13.
Sasa, namna gani Yehova anatusaidiaka tupiganishe matatizo ya akili? Vile utaona mu habari zenye kufuata, Yehova anaonyesha kama anatuhangaikiaka kabisa mu njia mbalimbali.
a Yehova ni jina ya pekee ya Mungu.—Zaburi 83:18.