Yehova atafanya jina yake itukuzwe milele
Maulizo Ya Wasomaji Wetu
Namna gani habari “Jina Lako Litakaswe” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 6, 2020 ilibadilisha mambo yenye tuliamini kuhusu jina ya Yehova na Mamlaka Yake Makubwa Zaidi?
▪ Mu ile habari, tulijifunzaka kama kuko jambo moya ya maana sana yenye inahusu wanadamu wote na malaika. Ile jambo ni kutakaswa kwa jina kubwa ya Yehova na inahusu Mamlaka Makubwa Zaidi, ni kusema, njia ya Yehova ya kutawala njo ya muzuri zaidi. Ile inahusiana na kutakaswa kwa jina yake. Vilevile, ushikamanifu wa wanadamu unahusiana pia na kutakaswa kwa jina ya Yehova.
Sasa, juu ya nini tunakazia kama ile jambo ya maana zaidi inahusiana na jina ya Yehova na kutakaswa kwa ile jina? Tuzungumuzie sababu tatu.
Tangu uasi mu bustani ya Edeni, Shetani anaendelea kusema uongo juu ya jina ya Mungu
Kwanza, Shetani alishambulia jina ya Yehova, ao sifa yake mu bustani ya Edeni. Wakati Shetani alimuuliza Eva ulizo alipenda kuonyesha kama Yehova haiko mukarimu na kama maagizo yenye aliwapatiaka yeye na Adamu haikukuwa ya haki. Kisha, Shetani alipinga moja kwa moja maneno yenye Yehova alisemaka na kusema kama ni muongo. Kwa kufanya vile, alisema uongo juu ya jina ya Yehova. Alifikia kuwa “Ibilisi,” maana yake “muchongezi.” (Yoh. 8:44) Juu Eva aliamini uongo wa Shetani, hakumutii Mungu na alipinga Mamlaka Yake Makubwa Zaidi. (Mwa. 3:1-6) Mupaka leo, Shetani anaendelea kusema uongo juu ya jina ya Mungu kwa kueneza uongo juu ya utu wake. Wale wenye wanaamini ule uongo, inawezekana kabisa wakose kumutii Yehova. Njo maana, watu wa Mungu wanaona kama kusema uongo juu ya jina takatifu ya Yehova ni ukosefu wa haki wa mubaya sana. Na njo sababu kubwa sana yenye inafanya kukuwe mateso na uovu ku dunia.
Pili, juu wanadamu na malaika wote wapate faida, Yehova atatakasa jina yake, ataisafisha kabisa kutokana na mambo yote ya uongo yenye ilisemewa. Ile njo jambo kubwa sana na ya maana yenye Yehova anapenda kufanya. Njo maana anasema hivi: “Hakika nitatakasa jina langu kubwa.” (Eze. 36:23) Na Yesu pia alionyesha jambo yenye inapaswa kuwa ya maana sana mu sala za watumishi waaminifu wote wa Yehova, wakati alisema hivi: “Jina lako litakaswe.” (Mt. 6:9) Biblia inakazia tena na tena ulazima wa kutukuza jina ya Yehova. Tuzungumuzie tu mifano fulani: “Mumupatie Yehova utukufu wenye jina lake linastahili.” (1 Ny. 16:29; Zb. 96:8) “Muimbie jina lake lenye utukufu sifa.” (Zb. 66:2) “Nitatukuza jina lako milele.” (Zb. 86:12) Siku moya, Yehova alisema yeye peke kutoka mbinguni; ilikuwa siku yenye Yesu alikuwa mu hekalu mu Yerusalemu, wakati alisemaka hivi: “Baba, tukuza jina lako.” Na Yehova alimujibia hivi: “Nimelitukuza na nitalitukuza tena.”—Yoh. 12:28.a
Tatu, kusudi ya Yehova itaendelea tu kuwa na uhusiano na jina yake, ao sifa yake. Waza kidogo: Mambo itakuwa namna gani kisha jaribu ya mwisho yenye itatokea ku mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo? Je, malaika na wanadamu wote wataendelea kugawanyika kuhusiana na ile jambo ya maana, ni kusema, kutakaswa kwa jina ya Yehova? Ile wakati wanadamu hawatakuwa tena na lazima ya kuonyesha ushikamanifu wao. Watakuwa wakamilifu na watakuwa walishachunguzwa kwa ukamili. Watapata uzima wa milele. Tena, hakutakuwa lazima ya kutafuta ushuhuda ili kuonyesha kama njia ya Yehova ya kutawala njo ya muzuri zaidi. Ile wakati malaika wote mbinguni na wanadamu wataunganishwa na watakubali utawala wa Yehova. Sasa, tuseme nini kuhusu jina ya Yehova?
Ile wakati, kila mutu atajua kweli kuhusu Yehova na jina yake itatakaswa kwa ukamili. Lakini, malaika na wanadamu wote waaminifu wataendelea kuona ile jina kuwa njo jambo ya maana sana. Juu ya nini? Juu wataona mambo ya ajabu yenye Yehova ataendelea kufanya. Waza kidogo: Kwa unyenyekevu, Yesu atamurudishia Yehova utawala wote, ile wakati Mungu ‘atakuwa vitu vyote kwa kila mutu.’ (1 Ko. 15:28) Kisha pale, ku dunia wanadamu wote watafurahia “uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” (Ro. 8:21) Na Yehova atatimiza kusudi yake ya kuunganisha wanadamu na malaika ili wakuwe familia moya.—Efe. 1:10.
Wanadamu na malaika wote watafanya nini kisha ile mambo? Bila shaka, tutapenda sana kuendelea kusifu jina ya Yehova. Mwandikaji wa zaburi Daudi aliongozwa na roho ili kuandika hivi: “Yehova Mungu asifiwe . . . Jina lake lenye utukufu lisifiwe milele.” (Zb. 72:18, 19) Milele na milele, tutaendelea kupata sababu za mupya na zenye kufurahisha za kumusifu.
Jina ya Yehova inafananisha mambo yote kumuhusu. Wakati tunafikiria kuhusu jina ya Yehova, tunakumbuka kama iko na upendo. (1 Yo. 4:8) Tutaendelea kukumbuka kama juu Yehova alitupenda, njo maana alituumba na kututolea zabihu ya bei ya ukombozi. Na tutaendelea kukumbuka kama njia yake ya kutawala ni ya upendo na ya haki. Tutaendelea kujionea upendo wa Yehova milele. Milele na milele, tutachochewa kumukaribia Baba yetu na kuimba nyimbo za kusifu jina yake tukufu.—Zb. 73:28.