Maulizo ya Wasomaji Wetu
Tunapaswa kuelewa namna gani Zaburi 12:7?
Mu Zaburi 12:1-4, Daudi anaonyesha kama “watu waaminifu hawako tena kati ya wana wa binadamu.” Na kisha mu Zaburi 12:5-7, anasema hivi.
“‘Kwa sababu wale wenye kuteswa wanakandamizwa,
Kwa sababu ya kilio cha maumivu cha maskini,
Nitasimama ili kutenda,” ni vile Yehova anasema.
‘Nitawaokoa kutoka kwa wale wenye kuwatendea kwa zarau.’
Maneno ya Yehova yako safi;
Yako kama feza yenye ilisafishwa katika tanuru ya udongo, yenye ilisafishwa mara saba (7).
Utawalinda, Ee Yehova;
Utamulinda kila mumoja wao milele kutokana na kizazi hiki.”
Mustari wa 5 unaonyesha mambo yenye Mungu anasema juu ya wale wenye kuteswa. Anasema kama atawaokoa.
Mustari wa 6 unaongeza hivi: “Maneno ya Yehova yako safi kama feza yenye ilisafishwa.” Ile maneno inaonyesha mawazo yetu kuhusu maneno ya Yehova.
Mu tafsiri fulani za Biblia, Zaburi 12:7 inatafsiriwa hivi: “Utailinda.” Juu mustari wenye kutangulia unazungumuzia “maneno ya Yehova” watu fulani wanaamini kama Zaburi 12:7 inazungumuzia maneno ya Yehova. Tunajua kama Mungu amelinda Biblia hata kama wapinzani wamejikaza sana ili kuikataza na kuiharibu.—Isa. 40:8; 1 Pe. 1:25.
Lakini pia, Yehova analinda “wenye kuteswa” na wale wenye “wanakandamizwa” wenye kuzungumuziwa mu mutari wa 5, na ataendelea kuwasaidia na kuwaokoa.”—Yob 36:15; Zb. 6:4; 31:1, 2; 54:7; 145:20.
Sasa mu ule mustari wa 7, ni nini njo Yehova analinda, watu ao maneno yake?
Wakati tunachunguza ile zaburi kwa uangalifu inaonekana wazi kama ni watu njo Yehova analinda.
Ku mwanzo wa Zaburi 12, Daudi anazungumuzia watumishi waaminifu wa Yehova wenye watu waovu wamedanganya. Mu mustari wa 3 Yehova anasema kama atapatia malipizi wale wenye kutumia mubaya ulimu wao. Ile zaburi inatuhakikishia kama Mungu atatenda kwa ajili ya watu wake kwa sababu maneno yake ni safi.
Kwa hiyo, mustari wa 7 unamaanisha kama Yehova atalinda wale wenye kuteswa na kugandamizwa na waovu.
Sasa juu ya nini tafsiri fulani za Biblia zinatafsiri mustari wa 7 hivi: “Utailinda”? Ile namna ya kutafsiri inategemea kopi fulani zenye kutumainika za Maandiko ya Kiebrania. Lakini mu Septante ya Kigiriki hii neno njo inatumiwa: “Atatulinda.” Kwa hiyo, ile andiko inazungumuzia waaminifu wenye kuteswa na kukandamizwa. Watalindwa “kutokana na kizazi hiki,” ni kusema kutokana na wanaume wenye kuendeleza upotovu. (Zb. 12:7, 8) Mu tafsiri ya Maandiko ya Kiebrania katika Kiaramu, ile andiko inasema hivi: “Weye, Ee Bwana, utalinda wenye haki, utawalinda kutokana na kizazi kibaya milele.” Ile ni ushuhuda ingine yenye kuonyesha kama Zaburi 12:7 haizungumuzie maneno ya Mungu.
Kwa hiyo, ile andiko inapatia tumaini, “watu waaminifu” kama Mungu atatenda kwa ajili yao.