Mambo ya Mubaya Yenye Inatokeaka Wakati ya Vita
Vita inakuwaka na matokeo ya mubaya sana ku bale benye kuishi kwenye iko. Mu dunia yote, maaskari na batu bengine benye balishakaishi kwenye kuko vita banajua vile inakuwaka mubaya sana.
MAASKARI
“Wakati yenye unaona vile batu biko nakufa ao kulumia mubaya sana, haujisikiake tu kuwa salama.”—Gary, Uingereza.
“Balinipiga masasi ku mugongo na ku sura, na niliona vile baliua batu mingi, kutia ndani, batoto na bazee. Vita inafanyaka mutu asihangaikie tena mateso wala kufa.”—Wilmar, Kolombia.
“Saa banapiga mutu masasi na uko naona, hauwezi kusahau ile. Picha ya ule mutu mwenye alikuwa nateseka inakurudiliaka tena na tena mu akili. Hauwezi kabisa kusahau byenye bilipitikanaka ile siku.”—Zafirah, Amerika.
BATU BENGINE
“Nilijisikia sawa vile sitakuwaka tena na furaha. Niliogopa kufa, lakini niliogopea zaidi sana batu ya familia yangu na barafiki yangu.”—Oleksandra, Ikrene.
“Tuliogopa sana kupigwa masasi juu tulipaswa kusimama ku mustari juu ya kupata chakula kuanzia saa munane ya busiku (2h:00) mupaka saa tano ya busiku (23h:00), na tulijua kama masasi ingetuangukia saa yoyote juu vita ilikuwa tu karibu na kwenye tulikuwa.”—Daler, Tajikistan.
“Vita iliniacha bila bazazi. Ilinifanya nikuwe yatima bila mutu wa kunifariji wala wa kunihangaikia.”—Marie, Rwanda.
Hata kama batu benye tunatokea kuzungumuzia baliteseka juu ya vita, kwa sasa bamepata faraja. Na biko hakika kama hivi karibuni mambo yote yenye inahusu vita itafikia mwisho. Kupitia Biblia, hii gazeti ya Munara wa Mulinzi itatusaidia kuelewa namna ile inawezekana.