Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp25 na. 1 uku. 3
  • Mambo ya Mubaya Yenye Inatokeaka Wakati ya Vita

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo ya Mubaya Yenye Inatokeaka Wakati ya Vita
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAASKARI
  • BATU BENGINE
  • Namna ya Kuwa na Amani Hata Kama Kuko Vita
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2025
  • Mwaka Moya Inaenea Tangu Vita Ianze mu Ikrene​—Ni Tumaini Gani Yenye Biblia Inatoa?
    Habari Zingine
  • Vita Imemaliza Makuta Mingi Sana—Iko Na Matokeo Gani Ingine?
    Habari Zingine
  • Namna Vita Inatuleteaka Siye Bote Matokeo ya Mubaya
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2025
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2025
wp25 na. 1 uku. 3
Picha: 1. Ku picha kuko sehemu ya yulu ya sura ya askari fulani. 2. Ku picha kuko sehemu ya yulu ya sura ya mwanamuke moya mwenye kuzeeka.

Mambo ya Mubaya Yenye Inatokeaka Wakati ya Vita

Vita inakuwaka na matokeo ya mubaya sana ku bale benye kuishi kwenye iko. Mu dunia yote, maaskari na batu bengine benye balishakaishi kwenye kuko vita banajua vile inakuwaka mubaya sana.

MAASKARI

“Wakati yenye unaona vile batu biko nakufa ao kulumia mubaya sana, haujisikiake tu kuwa salama.”—Gary, Uingereza.

“Balinipiga masasi ku mugongo na ku sura, na niliona vile baliua batu mingi, kutia ndani, batoto na bazee. Vita inafanyaka mutu asihangaikie tena mateso wala kufa.”—Wilmar, Kolombia.

“Saa banapiga mutu masasi na uko naona, hauwezi kusahau ile. Picha ya ule mutu mwenye alikuwa nateseka inakurudiliaka tena na tena mu akili. Hauwezi kabisa kusahau byenye bilipitikanaka ile siku.”—Zafirah, Amerika.

BATU BENGINE

“Nilijisikia sawa vile sitakuwaka tena na furaha. Niliogopa kufa, lakini niliogopea zaidi sana batu ya familia yangu na barafiki yangu.”—Oleksandra, Ikrene.

“Tuliogopa sana kupigwa masasi juu tulipaswa kusimama ku mustari juu ya kupata chakula kuanzia saa munane ya busiku (2h:00) mupaka saa tano ya busiku (23h:00), na tulijua kama masasi ingetuangukia saa yoyote juu vita ilikuwa tu karibu na kwenye tulikuwa.”—Daler, Tajikistan.

“Vita iliniacha bila bazazi. Ilinifanya nikuwe yatima bila mutu wa kunifariji wala wa kunihangaikia.”—Marie, Rwanda.

Hata kama batu benye tunatokea kuzungumuzia baliteseka juu ya vita, kwa sasa bamepata faraja. Na biko hakika kama hivi karibuni mambo yote yenye inahusu vita itafikia mwisho. Kupitia Biblia, hii gazeti ya Munara wa Mulinzi itatusaidia kuelewa namna ile inawezekana.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine