Namna Vita Inatuleteaka Siye Bote Matokeo ya Mubaya
“Tangu Vita ya Pili ya Ulimwengu, vita inaendelea kuongezeka mu dunia. Kati ya batu miliare munane benye kuwa mu dunia, batu miliare mbili biko naishi kwenye kuko vita.”
Amina J. Mohammed, wa Chini ya Mwandishi Mukubwa wa Umoja wa Mataifa, Tarehe 26 Mwezi wa 1, 2023.
Vita inaweza kuanza kwa kushitukia ku mafasi kwenye pengine hatukutazamia kama itaanza. Hata bale benye kuwa mbali na fasi kwenye kuko vita banaweza kupatwa na matokeo ya ile vita, juu leo mainchi iko na uhusiano mu njia moya ao ingine. Na hata kama ile vita inaisha, batu banaweza tu kuendelea kuteseka juu ya matokeo ya ayo. Fikiria mifano fulani:
Kukosa chakula. Kulingana na Shirika ya Chakula ya Ulimwenguni (PAM) “sababu kubwa yenye inafanya kukuwe njala ya mingi ni vita. Batu mingi benye banakosaka chakula ni bale benye biko naishi kwenye kuko vita.”
Matatizo ya kimwili na ya kiakili. Kusikia kama vita inaweza kutokea mu eneo fulani, inafanyaka batu bahangaike sana na bakuwe na wasiwasi. Batu benye kuishi kwenye kuko vita banaweza kulumia kimwili ao tena banaweza kuwa na matatizo ya akili. Na jambo ya kuhuzunisha ni kama, mara mingi bale batu habapatake matunzo yenye biko nayo lazima mu ile wakati.
Kuacha manyumba. Shirika ya Umoja wa Mataifa Yenye Kuhangaikia Wakimbizi (UNHCR) ilisema kama mu Mwezi wa 9, 2023, zaidi ya batu milioni 114 mu dunia yote, bamelazimika kuacha manyumba yabo. Sababu kubwa yenye inaleta ile hali ni vita.
Matatizo ya makuta. Vita inaletaka matatizo ya makuta, sawa vile bitu kupanda bei sana. Batu banatesekaka juu makuta yenye ilipaswa kutumikishwa mu mambo ya matunzo na ya masomo, guvernema inaitumiaka juu ya kutegemeza vita. Na kisha vita, inalombaka makuta mingi juu ya kujenga tena majengo yenye ilibomoka.
Dunia kuharibika. Batu banatesekaka sana wakati bitu byenye binabasaidiaka kuishi binaharibishiwa kimakusudi. Kuchafuka kwa mayi, hewa, na budongo, inaweza kuleta magonjwa mu siku zenye ziko nakuya. Na hata kisha vita, mabombe yenye ilibakia mu budongo inaweza kulumiza ao kuua batu saa inalipuka.
Kusema kweli, vita inaharibishaka bitu na inalombaka makuta mingi sana.