Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mrt habari 112
  • Vita Itaisha Wakati Gani?​—Biblia Inasema Nini?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vita Itaisha Wakati Gani?​—Biblia Inasema Nini?
  • Habari Zingine
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Vita ku dunia
  • Vita yenye itamalizaka mavita yote
  • 2023: Mwaka wa Mahangaiko​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zingine
  • Mwaka Moya Inaenea Tangu Vita Ianze mu Ikrene​—Ni Tumaini Gani Yenye Biblia Inatoa?
    Habari Zingine
  • Vita Imemaliza Makuta Mingi Sana—Iko Na Matokeo Gani Ingine?
    Habari Zingine
  • Namna Vita Inatuleteaka Siye Bote Matokeo ya Mubaya
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2025
Ona Habari Zaidi
Habari Zingine
mrt habari 112
Picha mbalimbali: Picha yenye kuonyesha maeneo mbalimbali kwenye kuko vita. 1. Mabombe mu eneo fulani ya Gaza. 2. Yerusalemu kisha kushambuliwa na mabombe.

Kushoto: Yasser Qudaih/Anadolu via Getty Images; kuume: RONALDO SCHEMIDT/AFP via Getty Images

MUENDELEE KUKESHA!

Vita Itaisha Wakati Gani?​—Biblia Inasema Nini?

Le 13 ya Mwezi wa 4, 2024, Secrétaire Général wa Umoja wa Mataifa alisema hivi juu ya vita kati ya Iran na Israeli: “Hii njo wakati ya kupunguza vita na kusaidia batu baishi mu usalama. Tena hii njo wakati ya kujikaza kabisa kujizuia.”

Ile vita ni moya tu kati ya mavita yenye iko napiganiwa mu dunia.

“Leo, mu dunia, hesabu ya mavita inaongezeka sana kuliko wakati ingine tangu Vita ya Pili ya Ulimwengu, na inagusa batu miliare mbili. Ile ni sehemu moya juu ya ine (1/4) ya batu benye biko mu dunia.”​—United Nations Security Council, le 26 Mwezi wa 1, 2023.

Maeneo kwenye kuko vita ya nguvu sana ni inchi na miji sawa vile Israeli, Gaza, Siria, Azerbaijan, Ukraine, Sudan, Ethiopie, Niger, Myanmar, na Haiti.a

Vita itaisha wakati gani? Batawala ba hii dunia banaweza kuleta amani? Biblia inasema nini?

Vita ku dunia

Mavita yenye iko nafanyika leo mu dunia inaonyesha kama hivi karibuni vita yote itaisha. Hii mavita iko natimiza mambo yenye Biblia ilisemaka juu ya kipindi yenye tuko naishi. Biblia inaita hii kipindi “umalizio wa mupangilio wa mambo.”​—Matayo 24:3.

  • “Mutasikia juu ya vita na habari za vita. . . . Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme.”​—Matayo 24:6, 7.

Soma habari “Ni Nini Ishara ya ‘Siku za Mwisho’?” juu ujue namna vita yenye tuko naona leo iko natimiza mambo yenye Biblia ilisemaka.

Vita yenye itamalizaka mavita yote

Biblia inatabiri kama mavita itaisha. Namna gani? Haiko batu njo bataimaliza, itamalizika njo ku Armagedoni, “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufunuo 16:14, 16) Kisha ile vita, Mungu atatimiza ahadi yake ya kufanya batu baishi milele kwa amani.​—Zaburi 37:10, 11, 29.

Juu ya kujua habari mingi kuhusu vita ya Mungu yenye itamalizaka mavita yote, soma habari “Armagedoni Ni Nini?”

a ACLED Conflict Index, “Ranking violent conflict levels across the world,” January 2024

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine