Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp25 na. 1 uku. 10-13
  • Namna Vita Itamalizika

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Vita Itamalizika
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MUNGU ATATOSHA GUVERNEMA ZOTE
  • MUNGU ATOTOSHA ZAMBI
  • MUNGU ATATOSHA SHETANI NA MASHETANI WAKE
  • Namna Mungu Anaona Vita Leo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Juu ya Nini Vita Inaendelea?
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2025
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2025
wp25 na. 1 uku. 10-13
Askari alishaikala yulu ya manyumba yenye ilibomoka na vita na iko nawaza.

Batu habawezi kumaliza vita

Namna Vita Itamalizika

Biblia inaonyesha kama Mungu ‘atamaliza vita katika dunia yote.’ (Zaburi 46:9) Hapana batu.

MUNGU ATATOSHA GUVERNEMA ZOTE

Mungu atatosha guvernema zote ku vita yenye Biblia inaita Armagedoni.a (Ufunuo 16:16) Mu ile wakati, “wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu” watakusanywa pamoya ku “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufunuo 16:14) Armagedoni njo vita ya Mungu yenye itamaliza vita zote.

Mungu atatosha guvernema za banadamu na kutia guvernema ao Ufalme wake, wenye kuwa mbinguni na wenye hauwezi kuharibiwa. (Danieli 2:44) Mungu alimuchagula, Yesu Kristo, Mwana wake juu ya kuwa Mufalme wa ile guvernema. (Isaya 9:6, 7; Matayo 28:18) Ile guvernema njo Ufalmeb yenye Yesu alifundishaka bafuasi yake basali juu ya ayo. (Matayo 6:9, 10) Batu yote batatawaliwa na guvernema yenye Yesu njo atakuwa Mutawala.

Tofauti na batawala banadamu, Yesu yeye hatatumia mamlaka yake juu ya faida yake mwenyewe. Juu ni mwenye haki na hana ubaguzi, hakuna mutu mwenye atazarauliwa juu ya rangi yake ya ngozi, inchi, ao kabila yake. (Isaya 11:3, 4) Na batu habatapigania tena haki zao. Juu ya nini? Juu Yesu atahangaikia maisha ya kila mutu. “Ataokoa maskini mwenye kulilia musaada, pia mutu wa hali ya chini na mutu yeyote mwenye hana musaidizi. . . . Atawaokoa katika ukandamizaji na katika jeuri.”—Zaburi 72:12-14.

Ufalme wa Mungu utatosha ku dunia silaha zote zenye kuua batu. (Mika 4:3) Utatosha pia batu babaya benye habapendi kuacha kupigana na benye kuumiza bengine. (Zaburi 37:9, 10) Kila mwanaume, mwanamuke, na mutoto atajisikia salama hata akuwe wapi ku dunia.—Ezekieli 34:28.

Wakati Ufalme wa Mungu utaanza kutawala dunia, batu bote batakuwa na maisha ya muzuri zaidi. Ile Ufalme itamaliza magumu yenye inafanyaka batu bapigane, sawa vile umaskini, njala, na kukosa nyumba. Kila mutu atakuwa na chakula mingi yenye kujenga mwili na atafurahia fasi ya muzuri ya kuishi.—Zaburi 72:16; Isaya 65:21-23.

Ufalme wa Mungu utatosha mambo yote ya mubaya yenye vita ilishaletea batu. Ile inatia ndani bidonda, mahangaiko ya kiakili, na ya kihisia, mambo yenye inatesaka batu wakati ya vita. Hata bale benye balikufa batafufuliwa juu ya kuishi tena ku dunia. (Isaya 25:8; 26:19; 35:5, 6) Mafamilia itakutana tena, na mambo ya mubaya ya vita haitakumbukwa tena, itakuwa njo “mambo ya zamani [yenye] yamepita kabisa.”—Ufunuo 21:4.

MUNGU ATOTOSHA ZAMBI

Wakati Ufalme wa Mungu utatawala dunia, batu bote bataabudu Mungu wa kweli, Yehovac, “Mungu wa upendo na amani.” (2 Wakorinto 13:11) Batu batajifunza namna ya kuishi pamoya kwa amani. (Isaya 2:3, 4; 11:9) Bote benye banamutii Mungu habatateseka tena juu ya zambi.—Waroma 8:20, 21.

MUNGU ATATOSHA SHETANI NA MASHETANI WAKE

Ufalme wa Mungu utaharibu bale benye biko nachochea batu kupigana, ni kusema, Shetani na mashetani wake. (Ufunuo 20:1-3, 10) Juu habatachochea tena batu kufanya vile, “amani itakuwa nyingi.”—Zaburi 72:7.

Ukuwe hakika kama ahadi (malako) ya Mungu ya kumaliza vita itatimia kabisa. Juu iko na uwezo na anapenda kumaliza vita.

  • Mungu iko na hekima na nguvu ya kumaliza vita. (Yobu 9:4) Hakuna kitu yenye anaweza kushinda kutimiza.—Yobu 42:2.

  • Mungu anachukia kuona batu banateseka. (Isaya 63:9) Tena “anachukia mutu yeyote mwenye kupenda jeuri.”—Zaburi 11:5.

  • Mungu anatimizika tu byenye anasema; hawezi kusema bongo.—Isaya 55:10, 11; Tito 1:2.

Mungu ataleta amani ya kweli na ya milele wakati wenye kuya.

Mu paradiso, familia moya iko nacheka wakati balishaikala yulu ya mulima. Farasi ziko nakula mayani pembeni yabo.

Mungu atamaliza vita

Juu ya nini Mungu ameruhusu vita?

Pengine uko najiuliza, juu ya nini Mungu ameacha vita iendelee mupaka leo? Juu ya kupata jibu ya ile ulizo, angalia video Sababu Gani Mungu Anaacha Mateso? ku jw.org.

a Soma habari “Armagedoni Ni Nini?” ku jw.org.

b Angalia video Ufalme wa Mungu Ni Nini? ku jw.org.

c Yehova njo jina ya pekee ya Mungu.—Zaburi 83:18.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine