Batu habawezi kumaliza vita
Namna Vita Itamalizika
Biblia inaonyesha kama Mungu ‘atamaliza vita katika dunia yote.’ (Zaburi 46:9) Hapana batu.
MUNGU ATATOSHA GUVERNEMA ZOTE
Mungu atatosha guvernema zote ku vita yenye Biblia inaita Armagedoni.a (Ufunuo 16:16) Mu ile wakati, “wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu” watakusanywa pamoya ku “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufunuo 16:14) Armagedoni njo vita ya Mungu yenye itamaliza vita zote.
Mungu atatosha guvernema za banadamu na kutia guvernema ao Ufalme wake, wenye kuwa mbinguni na wenye hauwezi kuharibiwa. (Danieli 2:44) Mungu alimuchagula, Yesu Kristo, Mwana wake juu ya kuwa Mufalme wa ile guvernema. (Isaya 9:6, 7; Matayo 28:18) Ile guvernema njo Ufalmeb yenye Yesu alifundishaka bafuasi yake basali juu ya ayo. (Matayo 6:9, 10) Batu yote batatawaliwa na guvernema yenye Yesu njo atakuwa Mutawala.
Tofauti na batawala banadamu, Yesu yeye hatatumia mamlaka yake juu ya faida yake mwenyewe. Juu ni mwenye haki na hana ubaguzi, hakuna mutu mwenye atazarauliwa juu ya rangi yake ya ngozi, inchi, ao kabila yake. (Isaya 11:3, 4) Na batu habatapigania tena haki zao. Juu ya nini? Juu Yesu atahangaikia maisha ya kila mutu. “Ataokoa maskini mwenye kulilia musaada, pia mutu wa hali ya chini na mutu yeyote mwenye hana musaidizi. . . . Atawaokoa katika ukandamizaji na katika jeuri.”—Zaburi 72:12-14.
Ufalme wa Mungu utatosha ku dunia silaha zote zenye kuua batu. (Mika 4:3) Utatosha pia batu babaya benye habapendi kuacha kupigana na benye kuumiza bengine. (Zaburi 37:9, 10) Kila mwanaume, mwanamuke, na mutoto atajisikia salama hata akuwe wapi ku dunia.—Ezekieli 34:28.
Wakati Ufalme wa Mungu utaanza kutawala dunia, batu bote batakuwa na maisha ya muzuri zaidi. Ile Ufalme itamaliza magumu yenye inafanyaka batu bapigane, sawa vile umaskini, njala, na kukosa nyumba. Kila mutu atakuwa na chakula mingi yenye kujenga mwili na atafurahia fasi ya muzuri ya kuishi.—Zaburi 72:16; Isaya 65:21-23.
Ufalme wa Mungu utatosha mambo yote ya mubaya yenye vita ilishaletea batu. Ile inatia ndani bidonda, mahangaiko ya kiakili, na ya kihisia, mambo yenye inatesaka batu wakati ya vita. Hata bale benye balikufa batafufuliwa juu ya kuishi tena ku dunia. (Isaya 25:8; 26:19; 35:5, 6) Mafamilia itakutana tena, na mambo ya mubaya ya vita haitakumbukwa tena, itakuwa njo “mambo ya zamani [yenye] yamepita kabisa.”—Ufunuo 21:4.
MUNGU ATOTOSHA ZAMBI
Wakati Ufalme wa Mungu utatawala dunia, batu bote bataabudu Mungu wa kweli, Yehovac, “Mungu wa upendo na amani.” (2 Wakorinto 13:11) Batu batajifunza namna ya kuishi pamoya kwa amani. (Isaya 2:3, 4; 11:9) Bote benye banamutii Mungu habatateseka tena juu ya zambi.—Waroma 8:20, 21.
MUNGU ATATOSHA SHETANI NA MASHETANI WAKE
Ufalme wa Mungu utaharibu bale benye biko nachochea batu kupigana, ni kusema, Shetani na mashetani wake. (Ufunuo 20:1-3, 10) Juu habatachochea tena batu kufanya vile, “amani itakuwa nyingi.”—Zaburi 72:7.
Ukuwe hakika kama ahadi (malako) ya Mungu ya kumaliza vita itatimia kabisa. Juu iko na uwezo na anapenda kumaliza vita.
Mungu iko na hekima na nguvu ya kumaliza vita. (Yobu 9:4) Hakuna kitu yenye anaweza kushinda kutimiza.—Yobu 42:2.
Mungu anachukia kuona batu banateseka. (Isaya 63:9) Tena “anachukia mutu yeyote mwenye kupenda jeuri.”—Zaburi 11:5.
Mungu anatimizika tu byenye anasema; hawezi kusema bongo.—Isaya 55:10, 11; Tito 1:2.
Mungu ataleta amani ya kweli na ya milele wakati wenye kuya.
Mungu atamaliza vita
a Soma habari “Armagedoni Ni Nini?” ku jw.org.
b Angalia video Ufalme wa Mungu Ni Nini? ku jw.org.
c Yehova njo jina ya pekee ya Mungu.—Zaburi 83:18.