Juu ya Nini Vita Inaendelea?
Biblia inafasiria mambo yenye inafanyaka kukuwe mavita na juu ya nini inaendelea kuwa.
ZAMBI
Mungu aliumba bazazi yetu ya kwanza, Adamu na Eva, kwa mufano wake. (Mwanzo 1:27) Ile inamaanisha kama balipaswa kuwa na sifa sawa za Mungu, kutia ndani, amani na upendo. (1 Wakorinto 14:33; 1 Yohana 4:8) Lakini, Adamu na Eva habakumutii Mungu na balifanya zambi. Ile ilifanya siye bote turiti zambi na kifo. (Waroma 5:12) Juu tuliriti zambi, ile njo inatusukumaka kuwaza na kutenda bya mubaya.—Mwanzo 6:5; Marko 7:21, 22.
GUVERNEMA
Mungu hakutuumba juu tujitawale. Biblia inasema hivi: “Mwanadamu mwenye kutembea hana hata uwezo wa kuongoza hatua yake.” (Yeremia 10:23) Njo maana, guvernema za banadamu haziwezi kabisa kumaliza vita.
SHETANI NA MASHETANI WAKE
Biblia inaonyesha kama “ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.” (1 Yohana 5:19) Ule “muovu” anaitwa Shetani Ibilisi, na ni muuaji. (Yohana 8:44) Yeye na mashetani wake njo banasukumaka batu kupigana.—Ufunuo 12:9, 12.
Guvernema haziwezi kumaliza mambo yenye inafanyaka kukuwe vita, lakini Mungu yeye anaweza.