HABARI YA KUJIFUNZA YA 18
WIMBO 65 Fanya Maendeleo!
Ndugu Vijana—Muige Marko na Timoteo
“Chukua Marko ukuje pamoja naye, kwa maana ni mwenye faida kwangu katika utumishi.”—2 TI. 4:11.
WAZO KUBWA
Namna mufano wa Marko na Timoteo unaweza kusaidia ndugu vijana wakomalishe sifa zenye zitawasaidia watumikie zaidi bandugu na badada.
1-2. Ni nini ingezuia Marko na Timoteo watumikie zaidi bengine?
NDUGU vijana, munapenda kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova na kusaidia kutaniko? Tunajua munapenda kufanya vile. Inagusa moyo sana kuona vile vijana wengi wanapenda kutumikia bengine! (Zb. 110:3) Lakini pengine kuko mambo yenye iko nakuzuia. Uko naogopa kupanua utumishi wako juu haujue watakuomba utumikie wapi, ao uko najiuliza maisha yako itakuwa namna gani. Ulishakakatala mugao fulani juu uliona kama hautaweza? Kama ni vile, ujue kama vijana wengine walijisikiaka vile.
2 Marko na Timoteo balipata pia magumu ya vile. Habakujua maisha yabo itakuwa namna gani na inawezekana baliogopa kama habataweza kutimiza mugao wao. Lakini habakuacha ile mambo ibazuie kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova. Inawezekana Marko alikuwa naishi mu nyumba ya muzuri pamoya na mama yake wakati mutume Paulo na Barnaba balimuomba abasindikize mu safari yao ya kwanza ya umisionere. (Mdo. 12:12, 13, 25) Marko aliacha fasi kwenye anazoea juu apanue utumishi wake. Kwanza alihamia Antiokia. Kisha alisindikiza Paulo na Barnaba fasi zingine za mbali. (Mdo. 13:1-5) Inawezekana Timoteo naye alikuwa naishi na bazazi yake wakati Paulo alimuomba amusindikize mu kazi ya kuhubiri. Juu Timoteo alikuwa kijana na hakukuwa na uzoefu, pengine aliwaza kama hataweza. (Linganisha 1 Wakorinto 16:10, 11 na 1 Timoteo 4:12.) Lakini alikubali mualiko wa Paulo na alipata baraka mingi.—Mdo. 16:3-5.
3. (a) Tunajua namna gani kama Paulo alifurahia sana Marko na Timoteo? (2 Timoteo 4:6, 9, 11) (Ona pia picha.) (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari?
3 Marko na Timoteo balifikia kuwa na uzoefu na balijifunza kutumikia madaraka ya mingi wakati balikuwa vijana. Paulo alibafurahia sana njo maana alipenda bakuwe pembeni yake wakati alitambua kama alikuwa karibu kufa. (Soma 2 Timoteo 4:6, 9, 11.) Marko na Timoteo balikuwa na sifa gani zenye zilifanya Paulo abapende sana? Ndugu vijana wanaweza kubaiga namna gani? Na namna gani Mashauri yenye upendo ya Paulo inaweza kusaidia vijana?
Marko na Timoteo balitumikia madaraka ya mingi wakati balikuwa vijana na ile ilifanya Paulo abapende sana (Ona fungu ya 3)b
KAMA MARKO UKUWE TAYARI KUTUMIKIA BENGINE
4-5. Marko alionyesha namna gani kama alikuwa tayari kutumikia bengine?
4 Kutumikia bengine inaweza kumaanisha kujikaza sana kusaidia bengine, na kuendelea kufanya vile hata wakati ni nguvu. Ni vile Marko alifanya. Alituachia mufano muzuri. Wakati Paulo alikatala kuenda naye mu safari ya pili ya umisionere, inawezekana Marko aliumia na alivunjika moyo. (Mdo. 15:37, 38) Lakini hakuacha ile imuzuie kutumikia bandugu na badada zake.
5 Marko alikubali mugao wa kutumika pamoya na binamu yake Barnaba. Kisha miaka 11, Marko alikuwa kati ya batu benye balitegemeza Paulo wakati alifungwa kwa mara ya kwanza katika Roma. (Flm. 23, 24) Paulo alifurahia sana namna Marko alimutegemeza, njo maana alimuita “chanzo cha faraja nyingi.”—Kol. 4:10, 11.
6. Kutumika pamoya na Wakristo wenye kukomala kiroho kulisaidia Marko namna gani? (Ona maelezo ya chini.)
6 Kutumika pamoya na Bakristo benye kukomala kiroho kulisaidia sana Marko. Kisha kupitisha wakati fulani pamoya na Paulo katika Roma, Marko alienda Babiloni kutumika na Petro. Balifikia kuwa barafiki sana mupaka Petro akamuita “Marko, mwana wangu.” (1 Pe. 5:13) Wakati balikuwa natumika pamoya, inawezekana Petro alikuwa nafasiria Marko mambo ya mingi juu ya maisha na utumishi wa Yesu. Na Marko alifikia kuandika zile habari mu Injili ya Marko.a
7. Namna gani ndugu Seung-Woo aliiga mufano wa Marko? (Ona pia picha.)
7 Marko aliendelea kumutumikia Yehova kwa bidii na aliendelea kuwa karibu ya bandugu benye kukomala kiroho. Namna gani unaweza kumuiga Marko? Kama hauyapata pendeleo fulani yenye ungependa kutumikia, ukuwe muvumilivu na uendelee kutafuta nafasi za kutumikia Yehova na kutaniko. Ona mufano wa Seung-Woo, mwenye ni muzee wa kutaniko. Wakati alikuwa kijana, alijilinganisha na ndugu wengine vijana. Wamoya walipata mapendeleo fulani mbele yake. Seung-Woo aliona kama banamuonea na aliambia bazee juu ya ile jambo. Muzee moya alimushauria aendelee kujikaza kutumikia bengine hata kama wakati fulani bengine habataona matendo yake ya muzuri. Ile mashauri ilichochea Seung-Woo ajitolee juu ya kusaidia bandugu na badada benye kuzeeka na benye balikuwa na lazima ya musaada juu ya kufika ku mikutano. Wakati Seung-Woo anakumbuka ile mambo, anasema hivi: “Nilifikia kuelewa maana ya kutumikia bengine. Nilijionea furaha ya kusaidia bengine.”
Vijana wanapata faida gani wakati wanapitisha wakati na bandugu benye kukomala kiroho? (Ona fungu ya 7)
KAMA TIMOTEO UHANGAIKIE BENGINE KWA UPENDO
8. Juu ya nini Paulo alimuchagula Timoteo juu asafiri pamoya naye? (Wafilipi 2:19-22)
8 Paulo alikuwa na lazima ya mutu mwenye alikuwa hodari juu amusindikize wakati alirudia mu miji kwenye alipata upinzani. Kwanza alichagula Sila, Mukristo mwenye kukomala kiroho. (Mdo. 15:22, 40) Kisha alichagula Timoteo ajiunge naye. Juu ya nini Paulo alichagula Timoteo? Sababu moya ni juu bandugu balikuwa nasema mambo ya muzuri juu ya Timoteo. (Mdo. 16:1, 2) Pia, Timoteo alihangaikia sana batu.—Soma Wafilipi 2:19-22.
9. Namna gani Timoteo alionyesha kama alihangaikia kabisa batu?
9 Tangu wakati Timoteo alianza kutumika na Paulo, alionyesha kama alihangaikia sana bengine kuliko vile alijihangaikia. Njo maana, Paulo alimuacha Beroya juu atie moyo wanafunzi wapya. (Mdo. 17:13, 14) Ile wakati, inawezekana Timoteo alijifunza mambo mingi kupitia mufano wa Sila, mwenye naye alibakia Beroya. Kisha, Paulo alituma Timoteo yeye peke mu Tesalonike juu atie nguvu Wakristo wa mu ule muji. (1 Te. 3:2, maelezo ya chini) Kwa miaka 15 hivi yenye ilifuata, Timoteo alijifunza ‘kulia pamoja na wale wenye kulia.’ Alikuwa najitia pa nafasi ya benye balikuwa nateseka. (Ro. 12:15; 2 Ti. 1:4) Namna gani vijana Wakristo wanaweza kumuiga Timoteo?
10. Namna gani ndugu Woo Jae alijifunza kuhangaikia bengine?
10 Ndugu Woo Jae alijifunza kuhangaikia sana bengine. Wakati alikuwa kijana, ilikuwa nguvu kwake kuzungumuza na bandugu na badada benye kuzeeka. Alikuwa tu nabasalimia ku Jumba ya Ufalme na anajiendea. Muzee moya alimushauria aanze mazungumuzo kwa kuambia baamini benzake juu ya nini anabafurahiaka. Ule muzee alimushauria pia afikirie mambo yenye batu bengine banaweza kufurahia. Woo Jae alitumikisha ile mashauri. Leo, Woo Jae ni muzee, anasema hivi: “Ni mwepesi sasa kwangu kuzungumuza na batu ba miaka yote. Ninajisikia muzuri juu ninaelewa muzuri mahangaiko ya bengine. Ile imenisaidia sana nijue namna ya kusaidia baamini benzangu.”
11. Namna gani ndugu vijana wanaweza kujifunza kuhangaikia bengine mu kutaniko? (Ona pia picha.)
11 Ndugu vijana, munaweza pia kujifunza namna ya kuhangaikia bengine mu kutaniko. Wakati uko ku mikutano, zungumuza na batu yote ikuwe vijana ao bazee. Ubaulize habari yabo, na ubasikilize. Kisha utajua mambo yenye unaweza kufanya juu ubasaidie. Pengine utavumbula kama bibi na bwana fulani benye kuzeeka, biko na lazima ya musaada juu ya kutumikisha JW Library®. Ao pengine utavumbula kama habana mutu wa kuhubiri nabo. Unaweza kubasaidia kutumikisha muzuri telefone ao tablete yabo, ao unaweza kuhubiri nabo. Kama unakamata hatua ya kusaidia bengine, utakuwa mufano muzuri mu kutaniko.
Ndugu vijana wanaweza kufanya mambo ya mingi juu ya kusaidia kutaniko (Ona fungu ya 11)
MASHAURI YA PAULO INAWEZA KUKUSAIDIA
12. Mashauri yenye Paulo alipatia Timoteo inaweza kusaidia namna gani vijana?
12 Paulo alipatia Timoteo mashauri ya kumusaidia mu maisha na ya kumusaidia atimize muzuri utumishi wake. (1 Ti. 1:18; 2 Ti. 4:5) Ndugu vijana, ile mashauri inaweza kubasaidia na nyiye. Namna gani? Soma mabarua mbili yenye Paulo aliandikia Timoteo, uisome sawa vile ni weye njo Paulo aliandikia, tafuta kuona ni mashauri gani unaweza kutumikisha mu maisha yako. Tuone mifano fulani.
13. Nini njo inaweza kutusaidia tushikamane zaidi na Yehova?
13 “Ujizoeze ukiwa na kusudi la ushikamanifu kwa Mungu.” (1 Ti. 4:7b) Ushikamanifu kwa Mungu maana yake nini? Ni wakati mutu iko muaminifu kwa Yehova na anafanya mambo ya kumufurahisha. Juu hatuzaliwake na ile sifa, tunapaswa kuikomalisha. Tutafanya vile namna gani? Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “ujizoeze” ilikuwa natumiwa juu ya kuzungumuzia mazoezi ya nguvu sana yenye wakimbiaji walikuwa nafanya juu ya kujitayarisha kwa ajili ya mashindano. Wale wakimbiaji walipaswa kujizuia kufanya mambo fulani na kukazia akili muradi wao. Siye pia tunapaswa kujikaza kuepuka mambo ya kutukengeusha akili na kuzoea kufanya mambo yenye itatusaidia tumukaribie Yehova zaidi.
14. Tunapaswa kuwa na muradi gani wakati tuko nasoma Biblia? Toa mufano.
14 Wakati uko nasoma Biblia, kumbuka kama muradi wako ni kumukaribia Yehova. Kwa mufano, habari yenye kuzungumuzia namna Yesu alikutana na kijana fulani mwenye alikuwa mutawala na tajiri, inaweza kukufundisha nini? (Mk. 10:17-22) Ule kijana aliamini kama Yesu alikuwa Masiya lakini hakukuwa na imani ya nguvu juu ya kumufuata. Hata vile, Yesu ‘alimupenda.’ Inagusa moyo kabisa kuona namna Yesu alizungumuza na ule kijana. Ni wazi kama Yesu alipenda kumusaidia akamate uamuzi wa muzuri. Namna Yesu alitendea ule kijana ilionyesha kama Yehova naye alipenda sana ule kijana. (Yoh. 14:9) Wakati uko nafikiria ile habari, fikiria pia hali yako na ujiulize hivi: ‘Ninapaswa kufanya nini juu nimukaribie Yehova zaidi na nitumikie bengine zaidi?’
15. Juu ya nini ndugu kijana anapaswa kuwa mufano muzuri? Toa mufano. (1 Timoteo 4:12, 13)
15 “Ukuwe mufano kwa waaminifu.” (Soma 1 Timoteo 4:12, 13.) Paulo alitia moyo Timoteo akomalishe uwezo wa kusoma na kufundisha, lakini pia akomalishe sifa mbalimbali sawa vile upendo, imani, na mwenendo safi. Juu ya nini? Juu matendo inasemaka kupita maneno. Tuseme banakupatia hotuba yenye inazungumuzia namna ya kuongeza bidii mu mahubiri. Utajisikia huru kutoa ile hotuba kama weye peke unakuwaka na bidii mu mahubiri. Mufano wako utapatia maneno yako buzito.—1 Ti. 3:13.
16. (a) Ni mu mambo gani tano vijana Wakristo wanaweza kuwa mufano? (b) Namna gani kijana anaweza kuwa mufano muzuri “katika kusema”?
16 Sawa vile 1 Timoteo 4:12 inaonyesha, Paulo alizungumuzia mambo tano yenye ndugu kijana anaweza kufanya juu akuwe mufano muzuri. Hauone kama ni muzuri ujitilie muradi wa kujifunza ile mambo yote tano? Kwa mufano, tuseme unapenda kuwa mufano muzuri “katika kusema.” Fikiria ni mu njia gani mbalimbali unaweza kutumia maneno yako juu ya kujenga bengine. Kama ungali naishi na bazazi yako, unaweza kuwa nabashukuru juu ya mambo yote yenye biko nakufanyia. Kisha mikutano, unaweza kuambia mutu fulani mwenye alikuwa na kipindi mambo yenye ulifurahia mu kipindi yake. Unaweza pia kujikaza kutoa maelezo mu maneno yako mwenyewe. Ikiwa unajikaza kuwa mufano katika kusema, utaonyesha kama uko nafanya maendeleo ya kiroho.—1 Ti. 4:15.
17. Nini njo inaweza kusaidia ndugu kijana afikie miradi yake ya kiroho? (2 Timoteo 2:22)
17 “Kimbia tamaa za ujana.” (Soma 2 Timoteo 2:22.) Paulo alishauria Timoteo apiganishe tamaa zenye zingeharibu uhusiano wake pamoya na Yehova na kumuzuia kutimiza miradi yake ya kiroho. Na weye unaweza kutambua kama mambo fulani yenye pengine haiko ya mubaya iko nakukamata wakati mingi mupaka unakosa wakati ya kufanya mambo ya kiroho. Kwa mufano, mambo ya kujifurahisha, Enternete, ao michezo ya video inakukamataka wakati mingi? Unaweza kukamata wakati fulani na kuanza kuitumikisha mu mambo ya kiroho? Pengine unaweza kujitolea juu ya kusaidia kutunza Jumba ya Ufalme ao kuhubiri ku prezantware. Kama unajitolea juu ya kufanya mambo ya vile, inawezekana utapata barafiki ba mupya benye batakusaidia ujitilie miradi ya kiroho na uifikie.
KUTUMIKIA BENGINE KUNALETA BARAKA
18. Juu ya nini tunaweza kusema kama Marko na Timoteo balikuwa na maisha yenye furaha?
18 Marko na Timoteo balijitoa sana juu ya kutumikia bengine, na balikuwa na maisha ya furaha. (Mdo. 20:35) Marko alisafiri mu maeneo ya mingi mu dunia juu ya kutumikia baamini benzake. Aliandika pia habari yenye kugusa moyo juu ya maisha na utumishi wa Yesu. Timoteo alisaidia Paulo kuanzisha makutaniko na kutia moyo ndugu na dada. Kwa kweli, Yehova alifurahia sana roho ya kujitoa ya Marko na Timoteo.
19. Juu ya nini ndugu vijana wanapaswa kukazia akili mashauri yenye Paulo alipatia Timoteo, na bakifanya vile batapata faida gani?
19 Barua zenye Paulo aliandikia rafiki yake kijana Timoteo zinaonyesha wazi kama Paulo alimupenda sana. Zile barua zenye ziliongozwa na roho zinaonyesha pia kama Yehova anabapenda sana nyiye ndugu vijana. Anapenda mukuwe na maisha ya muzuri. Basi mukazie akili mashauri ya Paulo, na mufanye yenu yote juu ya kutumikia bengine. Kama munafanya vile, mutakuwa na maisha ya furaha leo na ‘mutashika sana uzima wa kwelikweli’ wakati wenye kuya.—1 Ti. 6:18, 19.
WIMBO 80 Uonje na Uone Vile Yehova Ni Mwema
b NAFASIRIO YA PICHA: Marko alisaidia Paulo na Barnaba mu safari yao ya umisionere. Kwa kupenda, Timoteo anatembelea kutaniko juu ya kutia nguvu bandugu na badada na kubatia moyo.