HABARI YA KUJIFUNZA YA 28
WIMBO 88 Unijulishe Njia Zako
Namna ya Kutafuta Mashauri
“Hekima ni ya wale wenye kutafuta shauri.”—MEZ. 13:10.
WAZO KUBWA
Mambo ya kufanya juu mashauri yenye tunapata itusaidie.
1. Tunaweza kufanya nini juu tukamate maamuzi ya muzuri? (Mezali 13:10; 15:22)
SIYE bote tunapendaka kukamata maamuzi ya muzuri. Neno ya Mungu inatuambia kama, juu tuweze kufanya vile inaomba tutafute mashauri ya muzuri.—Soma Mezali 13:10; 15:22.
2. Yehova anaahidi kutufanyia nini?
2 Mutu mwenye anaweza kutupatia mashauri ya muzuri zaidi ni Baba yetu Yehova. Njo maana tunapaswa kumulomba atupatie hekima. Anaahidi kama atatusaidia. Anasema hivi: “Nitakupatia shauri jicho langu likikuangalia.” (Zb. 32:8) Hii maneno inaonyesha kama Yehova anaahidi kutupatia mashauri yenye tuko nayo lazima na anaahidi kutusaidia kuitumikisha.
3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?
3 Mu hii habari, tutatafuta majibu ya Biblia ku hii maulizo ine: (1) Ninapaswa kuwa na sifa gani juu mashauri ya Biblia inisaidie? (2) Nani njo anaweza kunipatia mashauri ya muzuri? (3) Nitaonyesha namna gani kama ninapenda kabisa kupewa mashauri? (4) Juu ya nini ninapaswa kuepuka kulomba bengine banikamatie maamuzi?
NINAPASWA KUWA NA SIFA GANI?
4. Tunapaswa kuwa na sifa gani juu mashauri itusaidie?
4 Tunapaswa kuwa na unyenyekevu na kiasi juu mashauri ya muzuri itusaidie. Tunapaswa kukumbuka kama tuko na lazima ya mashauri ya bengine juu tukamate maamuzi ya hekima, zaidi sana wakati tunajikuta mu hali yenye hatuyajikutaka. Na tunapaswa kuitika kama hatujue mambo yote. Kama hatuna unyenyekevu na kiasi, ni nguvu Yehova atusaidie. Na mashauri yenye tunapata wakati tunasoma Neno ya Mungu inaweza kuwa sawa mayi yenye inamwangika ku mugongo ya bata. (Mik. 6:8; 1 Pe. 5:5) Lakini kama tuko na unyenyekevu na kiasi, tutakuwa tayari kusikiliza mashauri ya Biblia.
5. Daudi alifanya mambo gani ya ajabu yenye ingefanya akuwe na kiburi?
5 Tufikirie mufano wa Daudi. Alifanya mambo mingi ya ajabu lakini ile haikumuletea kiburi. Kwa mufano miaka mingi mbele hata akuwe mufalme, alijulikana juu alikuwa najua kupiga muziki muzuri sana. Na hata balimuita aende kupigia mufalme muziki. (1 Sa. 16:18, 19) Yehova alimuchagua akuwe mufalme pa nafasi ya Sauli na alimupatia roho yake takatifu. (1 Sa. 16:11-13) Batu balimusifu sana juu aliua baadui bamingi, aliua hata Goliati mwenye alikuwa na nguvu mingi. (1 Sa. 17:37, 50; 18:7) Daudi alifanya mambo ya mingi ya ajabu. Angekuwa na kiburi angewaza kama hana tena lazima ya mashauri ya bengine. Lakini Daudi hakukuwa vile.
6. Tunajua namna gani kama Daudi alikuwa nasikiliza mashauri ya bengine? (Ona pia picha)
6 Hata wakati Daudi alikuwa mufalme, aliendelea kuwa karibu na batu benye balikuwa namushauria. (1 Ny. 27:32-34) Ile haitushangaze, juu hata mbele akuwe mufalme alisikiliza mashauri ikuwe inatoka kwa mwanaume ao kwa mwanamuke. Kwa mufano, alisikiliza shauri ya Abigaili. Abigaili alikuwa bibi ya Nabali. Nabali alikuwa muchoyo na hakukuwa na shukrani. Lakini juu Daudi alikuwa munyenyekevu alitumikisha mashauri yenye Abigaili alimupatia, na ile ilimuepusha kufanya kosa kubwa.—1 Sa. 25:2, 3, 21-25, 32-34.
Kwa unyenyekevu Daudi anakubali na anatumikisha shauri yenye Abigaili alimupatia (Ona fungu ya 6)
7. Mufano wa Daudi unatufundisha nini? (Muhubiri 4:13) (Ona pia picha.)
7 Mufano wa Daudi unatufundisha mambo ya maana. Na siye tunaweza kuwa na uwezo fulani ao mamlaka fulani. Hata vile hatupaswe kuwaza kama tunajua kila kitu na hatuna lazima ya mashauri ya bengine. Tunajifunza pia kama tunapaswa kuwa tayari kusikiliza mashauri ya muzuri hata itoke kwa nani. (Soma Muhubiri 4:13.) Tukifanya vile, tunaweza kuepuka kufanya makosa mazito, yenye inaweza kutuletea siye na batu bengine magumu.
Tunapaswa kuwa tayari kusikiliza mashauri ya muzuri ikuwe inatoka kwa nani (Ona fungu ya 7)c
NANI ANAWEZA KUNIPATIA MASHAURI YA MUZURI?
8. Juu ya nini Yonatani alistahili kumupatia Daudi shauri?
8 Mufano wa Daudi unatufundisha jambo ingine ya maana. Alitafuta mashauri kwa batu benye balikuwa na urafiki muzuri pamoya na Yehova lakini pia benye balielewa muzuri hali yenye alikuwa ndani. Kwa mufano, wakati Daudi alipenda kujua kama inawezekana bafanye tena amani na Mufalme Sauli, alisikiliza shauri ya Yonatani mwana wa Sauli. Juu ya nini Yonatani njo angeweza kumupatia shauri ya muzuri? Ni juu Yonatani alikuwa na urafiki muzuri pamoya na Yehova, lakini pia alimujua muzuri Sauli. (1 Sa. 20:9-13) Ile inatufundisha nini?
9. Ni nani njo tunaweza kuuliza kama tuko na lazima ya mashauri? Toa mufano. (Mezali 13:20)
9 Wakati tuko na lazima ya mashauri, ni muzuri tuulize mutu mwenye iko na urafiki muzuri pamoya na Yehova lakini pia mwenye anajua muzuri hali yenye tuko ndani.a (Soma Mezali 13:20.) Kwa mufano, tuseme ndugu kijana iko natafuta dada mwenye anaweza kuwa bibi muzuri kwake. Unawaza nani njo anaweza kumupatia mashauri ya muzuri? Rafiki yake mwenye hayaoa anaweza kumupatia mashauri ya muzuri kama ile mashauri inategemea kanuni za Biblia. Lakini inawezekana ule ndugu kijana atapata mashauri ya muzuri zaidi kama anauliza bibi na bwana benye banamujua muzuri na benye bametumikia Yehova pamoya kwa wakati fulani. Banaweza kumuonyesha namna ya kutumikisha mashauri ya Biblia na banaweza kumuambia pia mambo yenye bamejifunza mu maisha yabo ya ndoa.
10. Tutazungumuzia sasa nini?
10 Tumezungumuzia sifa mbili zenye tunapaswa kuwa nazo juu mashauri itusaidie na tumeona ni nani anaweza kabisa kutupatia mashauri ya muzuri. Tuone sasa juu ya nini tunapaswa kuonyesha kama tunapenda kabisa kupewa mashauri, na juu ya nini hatupaswe kuomba bengine batukamatie maamuzi.
NINI ITAONYESHA KAMA NAPENDA KABISA KUPEWA MASHAURI?
11-12. (a) Tunapaswa kuepuka nini? (b) Mufalme Rehoboamu alifanya nini wakati alipaswa kukamata uamuzi wa maana?
11 Wakati fulani mutu anaweza kulomba mashauri, lakini anaweza kuwa tayari alishaamua jambo yenye atafanya. Mutu wa vile haiko kabisa natafuta mashauri, anapenda tu kujua ikiwa bengine banakubaliana na maamuzi yake. Mutu wa vile anaweza kujifunza kupitia mambo yenye ilimufikia mufalme Rehoboamu.
12 Rehoboamu njo alikuwa mufalme kisha Sulemani. Wakati Rehoboamu alianza kutawala, batu balikuwa na mali mingi. Lakini baliona kama Sulemani alikuwa nabatumikisha sana, njo maana balienda kumuona Rehoboamu na kumulomba abapunguzie muzigo. Rehoboamu alibalomba bamuachie wakati wa kuwaza mbele akamate uamuzi. Kwanza aliomba mashauri kwa banaume benye kukomala benye balitumikaka pamoya na Sulemani. (1 Fa. 12:2-7) Lakini inawezekana alikuwa tayari alishaamua mambo yenye atafanya, na alikuwa nawaza kama banaume benye kukomala batakubaliana na mawazo yake. Njo maana wakati benzake biyana balimupatia mashauri yenye ilipatana na mambo yenye alikuwa napenda, alikatala mashauri ya bazee na akaitika ya benzake. (1 Fa. 12:8-14) Rehoboamu alijibia batu maneno ileile yenye benzake biyana balimuambia. Matokeo ilikuwa nini? Taifa iligawanyika, na kuanzia pale mambo haikumuendea muzuri Rehoboamu.—1 Fa. 12:16-19.
13. Tunaweza kujua namna gani ikiwa tunapenda kabisa kupewa mashauri?
13 Mufano wa Rehoboamu unatufundisha nini? Hatupaswe kulomba mutu mashauri wakati tayari tulishaamua bya kufanya, tunapaswa kuwa tayari kusikiliza mashauri ya ule mutu. Tutajua namna gani kama tuko tayari kupewa mashauri? Tujiulize hivi: ‘Ninalombaka shauri na mara moya ninaikatala juu haipatane na mambo yenye ninapenda?’
14. Wakati banatupatia shauri, tunapaswa kukumbuka nini? Toa mufano. (Ona pia picha.)
14 Tufikirie hii mufano. Ndugu anapata kazi. Mbele aitike ile kazi, analomba mashauri kwa muzee fulani. Ule ndugu anaambia ule muzee vile ile kazi itamulomba akuwe mbali na familia yake kwa wakati murefu. Ule muzee anamukumbusha kama kupatana na kanuni za Biblia, daraka yake ya kwanza ni kushugulikia mahitaji ya kiroho ya familia yake. (Efe. 6:4; 1 Ti. 5:8) Wazia kama ule ndugu anakatala mashauri ya ule muzee na anaendelea kulomba mashauri kwa bandugu bengine, mupaka wakati anapata ndugu mwenye anamushauria kama anaweza kuitika ile kazi. Unawaza nini, ule ndugu iko natafuta kabisa shauri ao alishaamua jambo ya kufanya na iko natafuta tu mutu mwenye atakubaliana na maamuzi yake? Tunapaswa kukumbuka kama moyo wetu ni mudanganyifu. (Yer. 17:9) Wakati fulani shauri ya muzuri yenye tuko nayo kabisa lazima, ni ile yenye hatupendi.
Je tuko natafuta kabisa shauri ao tuko natafuta njo mutu mwenye anakubaliana na siye? (Ona fungu ya 14)
NAPASWA KULOMBA BENGINE BANIKAMATIE MAAMUZI?
15. Tunapaswa kuepuka kufanya nini, na juu ya nini?
15 Sawa vile tumeona, mutu mwenye hekima anatafuta mashauri mu Neno ya Mungu na analomba mashauri kwa Bakristo benye kukomala kiroho mbele ya kukamata maamuzi. Lakini, kila mumoya wetu iko na daraka ya kujikamatia maamuzi. (Gal. 6:4, 5) Njo maana tunapaswa kuwa baangalifu. Hatupaswe kuacha bengine batukamatie maamuzi. Batu fulani banalombaka waziwazi bengine babakamatie maamuzi. Kwa mufano, banaulizaka hivi mutu mwenye iko na uzoefu: “Kama ingekuwa weye, ungefanya nini?” Na bengine, kuliko kufikiri sana, banafuataka tu byenye bengine balifanya.
16. Ni hali gani ilikuwa mu kutaniko ya Korinto kuhusu nyama yenye ilitolewa kwa sanamu, na ni nani njo alipaswa kuamua ikiwa mutu atakula ile nyama? (1 Wakorinto 8:7; 10:25, 26)
16 Fikiria hii jambo yenye ilitokea mu karne ya kwanza mu kutaniko ya Korinto. Mu ile kutaniko Bakristo balipaswa kuamua ikiwa banaweza kula nyama yenye ilikuwa ilishatolewa ku masanamu. Paulo aliandikia bale Bakristo hivi: “Tunajua kwamba sanamu haiko kitu katika ulimwengu na kwamba hakuna Mungu isipokuwa mumoja.” (1 Ko. 8:4) Kwa hiyo, Bakristo fulani baliona kama haikukuwa mubaya kula nyama yenye ilitolewa kwa sanamu na kisha inauzishwa mu soko. Bengine baliamua kama habatakula ile nyama juu bakifanya vile zamiri yabo itabasumbua. (Soma 1 Wakorinto 8:7; 10:25, 26.) Ile ilikuwa uamuzi wenye kila mutu alipaswa kujikamatia. Paulo wakushauria Bakorinto bakamate uamuzi pa nafasi ya bengine ao bafuate tu uamuzi wa bengine bila kufikiri. Kila mutu alipaswa ‘kutoa hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.’—Ro. 14:10-12.
17. Mambo inaweza kuwa namna gani kama tunafuata tu maamuzi ya bengine bila kujiamulia siye peke? Toa mufano. (Ona pia picha.)
17 Namna gani hali ya vile inaweza kutufikia leo. Tuone kwa mufano uamuzi wenye kila Mukristo anapaswa kukamata juu ya sehemu za kidogo-kidogo za damu.b Kila Mukristo anapaswa kujiamulia ikiwa atazikubali ao hapana. Inaweza kuwa nguvu kwetu kuelewa mambo yenye inahusu damu. Lakini uamuzi kuhusu mambo ya vile ni muzigo wenye kila Mukristo anapaswa kujibebea. (Ro. 14:4) Kama tunafuataka tu uamuzi wenye bengine balikamata bila kujiamulia siye benyewe, tunaweza kuwa bazaifu na hatutakuwa na hekima ya kukamata maamuzi ya muzuri. Kama tunapenda kuwa na hekima, tunapaswa kujikaza kujikamatia maamuzi yenye inategemea Biblia. (Ebr. 5:14) Sasa ni wakati gani njo tunaweza kulomba shauri kwa Mukristo mwenye kukomala kiroho? Tunapaswa kulomba mashauri kama tulishatafuta habari lakini tungali tu na lazima ya musaada juu ya kuelewa namna ya kutumikisha kanuni za Biblia mu hali yetu.
Ni kisha tu kutafuta habari njo tunaweza kulomba mashauri (Ona fungu ya 17)
ENDELEA KUTAFUTA MASHAURI
18. Yehova alishatufanyia nini?
18 Yehova anatutumainia sana. Njo maana alitupatia uhuru wa kujikamatia maamuzi. Anatupatia Biblia na anatupatia barafiki benye biko na hekima benye banaweza kutusaidia kujua namna ya kutumikisha kanuni za Biblia. Ile inaonyesha kama Yehova, Baba yetu mwenye upendo anatuhangaikia sana. (Mez. 3:21-23) Sasa na siye tutafanya nini juu ya kumushukuru?
19. Namna gani tunaweza kuendelea kumufurahisha Yehova?
19 Bazazi banakuwaka na furaha sana wakati mutoto wabo anakomala na anakuwa mutumishi wa Yehova mwenye hekima na mwenye anasaidiaka bengine. Yehova naye anafurahi wakati tunaendelea kukomala kiroho, tunaendelea kutafuta mashauri, na kukamata maamuzi yenye inamuletea sifa.
WIMBO 127 Ninapaswa Kuwa Mutu wa Namna Gani?
a Mu mambo fulani Bakristo banaweza kulomba mashauri kwa batu benye habamutumikie Yehova. Kwa mufano mambo ya makuta, mambo ya afya, ao mambo ingine.
b Juu ya kujua habari za mingi kuhusu hii habari, ona nukta ya 5 na sehemu “Habari Zingine” mu somo ya 39 ya kitabu Furahia Maisha Milele!
c MAFASIRIO YA PICHA: Muzee mumoya anashauria muzee mwenzake juu ya namna alizungumuza mu mukutano wenye ulipita.