HABARI YA KUJIFUNZA YA 29
WIMBO 87 Tunatiana Moyo ku Mikutano
Namna ya Kutoa Mashauri
“Nitakupatia shauri jicho langu likikuangalia.”—ZB. 32:8.
WAZO KUBWA
Namna ya kupatia bengine mashauri yenye itabasaidia.
1. Nani anapaswa kushauria bengine, na juu ya nini?
UNAJISIKIAKA namna gani wakati inaomba ushaurie mutu. Batu fulani banapendaka kupatiana mashauri. Bengine banajizuiaka na habajisikiake muzuri wakati biko napana shauri. Ikuwe tunapendaka kupatiana mashauri ao hapana, siye bote tunalazimika kushauriana. Juu ya nini? Juu ile inaonyesha kama tunapendana. Na Yesu alisema kama juu tukuwe banafunzi yake tunapaswa kupendana. (Yoh. 13:35) Tena Biblia inaonyesha kama wakati tunashauria mutu urafiki wetu na ule mutu unakuwa nguvu zaidi.—Mez. 27:9.
2. Bazee banapaswa kujua kufanya nini, na juu ya nini? (Ona pia kisanduku “Mashauri ku Mukutano wa Katikati ya Juma.”)
2 Bazee ya kutaniko banapaswa kujua namna ya kutoa mashauri ya muzuri yenye itasaidia. Juu ya nini? Juu Yehova na Yesu banaweka bale banaume ili bachunge kutaniko. (1 Pe. 5:2, 3) Bazee banalinda kutaniko wakati banatupatia mashauri yenye inategemea Biblia mu hotuba zenye banatoa. Pia, banapatia kila mumoya wetu mashauri yenye inapatana na hali yake, na banasaidia benye balishamuacha Yehova barudie mu kutaniko. Namna gani bazee, na siye bote tunaweza kutoa mashauri ya muzuri?
3. (a) Nini njo itatusaidia kuwa bashauri bazuri? (Isaya 9:6; ona pia kisanduku “Umuige Yesu Wakati Unatoa Mashauri.”) (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari?
3 Kujifunza mifano ya batu benye kuwa mu Biblia kunaweza kutusaidia kuwa bashauri bazuri, zaidi sana mufano wa Yesu. Yesu anaitwa “Mushauri wa Ajabu.” (Soma Isaya 9:6.) Mu hii habari tutaona mambo ya kufanya wakati banatulomba shauri, na mambo ya kufanya wakati tunapaswa kushauria mutu mwenye hakutulomba shauri. Tutaona pia kama ni jambo ya maana kuchagua wakati wa muzuri juu ya kushauria mutu na kumushauria mu njia ya muzuri.
WAKATI BANAKULOMBA SHAURI
4-5. Wakati mutu anatulomba shauri, tunapaswa kwanza kujiuliza nini? Toa mufano.
4 Wakati mutu anakulomba shauri ile inakufurahisha juu inaonyesha kama anakutumainia. Na unaweza kupenda kumujibia palepale. Lakini mbele ya kumushauria inaomba uwaze kwanza, na ujiulize hivi: ‘Ninajua muzuri hii mambo juu niweze kumupatia shauri ya muzuri?’ Wakati fulani ni muzuri usimupatie shauri lakini umuongoze kwa mutu mwingine mwenye anajua muzuri ile mambo, mwenye anaweza kumupatia shauri ya muzuri.
5 Kwa mufano, tuseme rafiki yako iko na magonjwa ya nguvu. Anakuambia kama kuko namna mbalimbali za kutunza ile magonjwa, na anakuuliza ni ya wapi njo unawaza itamusaidia zaidi. Hata kama kunaweza kuwa namna ya kutunza yenye unafurahia, weye hauko munganga na haujue namna ya kutunza. Mu hali ya vile, njia ya muzuri ya kusaidia rafiki yako ni kumusaidia kutafuta munganga mwenye anajua kutunza ile magonjwa mwenye anaweza kumushauria.
6. Juu ya nini inaweza kuwa muzuri kungoya kidogo mbele ya kushauria mutu?
6 Hata kama tunaona kama tunastahili kupatia mutu shauri, inaweza kuwa muzuri tuchunge kidogo mbele ya kumujibia. Juu ya nini? Juu Mezali 15:28 inasema kama ‘mwenye haki anafikiri sana mbele ya kujibu.’ Njo maana hata kama tunawaza kama tunajua jibu ni muzuri tukamate kwanza wakati wa kufanya utafiti, kusali, na kufikiri sana juu ya ile jambo. Ile itatusaidia tukuwe hakika kama jibu yetu inapatana na mawazo ya Yehova.
7. Mufano wa nabii Natani unatufundisha nini?
7 Tuzungumuzie mufano wa nabii Natani. Daudi aliambia nabii Natani kama anapenda kumujengea Yehova hekalu. Natani alimushauria mara moya afanye vile. Lakini Natani alipaswa kwanza kukamata wakati ya kumuuliza Yehova juu ya ile jambo. Juu ya nini? Juu Yehova hakupenda Daudi njo ajenge ile hekalu. (1 Ny. 17:1-4) Kama vile hii habari inaonyesha, wakati banatulomba shauri ni muzuri tutende kwa hekima. Tusikuwe ‘wepesi wa kusema.’—Yak. 1:19.
8. Juu ya nini tunapaswa kufikiria sana shauri yenye tunataka kupatia mutu?
8 Sababu ingine ya kuwa waangalifu wakati mutu anatulomba shauri ni hii: Kama tunapatia mutu shauri yenye inakuwa na matokeo ya mubaya, na siye tuko na kosa mu ile mambo. Njo maana ni jambo ya maana kufikiri sana mbele ya kutoa shauri.
WAKATI HABAKULOMBE SHAURI
9. Bazee banapaswa kuhakikisha kwanza nini mbele batoe shauri? (Wagalatia 6:1)
9 Mara kwa mara bazee banapaswa kukamata hatua ya kushauria ndugu ao dada mwenye amefanya “hatua fulani ya mubaya.” (Soma Wagalatia 6:1.) Ule ndugu ao dada anaweza kuwa iko nakamata maamuzi yenye haiko ya muzuri yenye inaweza kumuongoza ku zambi nzito. Kusudi ya bazee ni kusaidia ule mutu aendelee kumutumikia Yehova na aishi milele. (Yak. 5:19, 20) Lakini juu shauri yabo isaidie, bazee banapaswa kwanza kuwa hakika kama ule ndugu ao dada alikamata kabisa hatua ya mubaya. Banapaswa kukumbuka kama haiko juu mutu alikamata uamuzi wenye kuwa tofauti ya yabo njo alifanya jambo yenye haimufurahishe Yehova. (Ro. 14:1-4) Sasa ikiwa bazee banatambua kama ule mutu alikamata kabisa hatua ya mubaya, namna gani banaweza kumushauria?
10-12. Muzee anapaswa kufanya nini wakati anashauria mutu mwenye hakulomba shauri? Toa mufano. (Ona pia picha.)
10 Haiko mwepesi kwa bazee kushauria mutu mwenye hakulomba shauri. Juu ya nini? Mutume Paulo alisema kama mutu anaweza kukamata hatua ya mubaya bila hata yeye kujua. Njo maana kama muzee anamupatia ule mutu shauri pengine hataelewa juu ya nini banamushauria. Kwa hiyo bazee banaweza kufanya kwanza mambo fulani ili kutayarisha mutu juu aitike mashauri.
11 Kupatia shauri mutu mwenye hakuilomba ni sawa vile kupanda mbegu mu bulongo ya nguvu. Mbele mutu aanze kupanda, analimaka kwanza bulongo. Ile inafanya bulongo ikuwe teketeke. Kisha anapanda mbegu. Na ku mwisho anamwanga mayi juu ya kusaidia mbegu ikomale. Ni vile njo muzee anafanya mbele ya kupatia mutu shauri yenye hakulomba. Anatayarisha kwanza ule mutu juu akuwe tayari kukubali ile shauri. Kwa mufano anatafuta wakati ya muzuri ya kuzungumuza na ule ndugu ao dada. Anamuambia kama anamuhangaikia na kama alipenda bazungumuzie jambo fulani. Inakuwaka mwepesi kusikia mashauri ya mutu mwenye anajulikana kuwa mutu muzuri mwenye anahangaikiaka bengine.
12 Wakati wa mazungumuzo, muzee anaweza kuendelea kuregeza bulongo mu njia ya mufano kwa kuonyesha kama siye bote tunafanyaka makosa na tunakuwaka na lazima ya mashauri. (Ro. 3:23) Kwa sauti ya kutulia na heshima sana anatumia Maandiko juu ya kusaidia mutu aelewe kama alikamata hatua ya mubaya. Wakati mutu anaelewa kama alifanya kosa, muzee “anapanda mbegu.” Anafanya vile kwa kumuambia mutu waziwazi mambo yenye anapaswa kufanya juu atengeneze mambo. Ku mwisho muzee “anamwangia mayi,” ni kusema anamupongeza juu ya mambo ya muzuri yenye iko nafanya na anasali pamoya naye.—Yak. 5:15.
Juu ya kupatia mutu shauri yenye hakulomba, inaomba kuwa na upendo na ufundi (Ona fungu ya 10-12)
13. Bazee banaweza kufanya nini juu ya kuhakikisha kama mutu anaelewa mashauri?
13 Saa moya unaweza kuambia mutu mambo fulani, lakini yeye anaelewa bingine. Bazee banapaswa kufanya nini juu bahakikishe kama mutu alielewa byenye balisema? Kwa upole banaweza kuuliza mutu maulizo juu bahakikishe kama anaelewa muzuri mashauri na anaelewa namna ya kuitumikisha. (Muh. 12:11) Majibu yenye mutu atapana njo itasaidia muzee ajue kama ule mutu alielewa mashauri.
TOA SHAURI WAKATI WA MUZURI NA MU NJIA YA MUZURI
14. Juu ya nini hatupaswe kushauria mutu wakati tulishakasirika? Fasiria.
14 Siye bote hatukamilike, njo maana tunaweza kusema ao kufanya mambo yenye inaumiza bengine. (Kol. 3:13) Hata Biblia inaonyesha kama wakati fulani mutu anaweza kufanya ao kusema mambo yenye inatukasirisha. (Efe. 4:26) Hata vile, hatupaswe kushauria mutu wakati tulishakasirika. Juu ya nini? Juu “kasirani ya mwanadamu haitokeze haki ya Mungu.” (Yak. 1:20) Kama tunashauria mutu wakati tuko na kasirani, tunaweza kufanya mambo iharibike zaidi kuliko kuitengeneza. Ile haimaanishe kama hatuwezi kuambia mutu kama alitukasirisha. Lakini, ni muzuri tutulie kwanza mbele tuongee naye.
15. Mufano wa Elihu unatufundisha nini? (Ona pia picha.)
15 Tuone mufano wenye Elihu, mushauri muzuri wa Yobu, alituachia. Kwa siku mingi, alisikiliza wakati Yobu alikuwa najitetea juu ya mashitaka ya barafiki yake. Elihu alimusikilia Yobu huruma. Lakini wakati Yobu alikuwa najaribu kujitetea, alisema mambo fulani yenye haikukuwa ya kweli juu ya Yehova. Ile ilimukasirisha sana Elihu. Lakini Elihu alichunga mupaka wakati yake ya kusema ifike, na alimushauria Yobu kwa upole na kwa heshima sana. (Yob. 32:2; 33:1-7) Mufano wa Elihu unatufundisha hii jambo ya maana sana: Shauri ya muzuri ni yenye inatolewa kwa upendo na kwa heshima mu wakati ya muzuri na kwa njia ya muzuri.—Muh. 3:1, 7.
Hata kama Elihu alikasirika ku mwanzo, wakati alitoa shauri alisema kwa upole na heshima sana (Ona fungu ya 15)
TUENDELEE KUSHAURI NA KUKUBALI MASHAURI
16. Zaburi 32:8 inatufundisha nini?
16 Andiko ya musingi ya hii habari inasema kama ‘Yehova anatupatia shauri jicho lake likituangalia.’ (Soma Zaburi 32:8.) Ile inaonyesha kama Yehova anaendelea kutusaidia. Anatupatia mashauri lakini anatusaidia pia kuitumikisha. Yehova ni mufano muzuri sana kwa siye bote. Wakati ni lazima tupatie bengine mashauri, tuendelee kubatia moyo na kubasaidia bakamate maamuzi ya muzuri.
17. Tunaweza kulinganisha bazee na nini wakati banatupatia mashauri? Fasiria. (Isaya 32:1, 2)
17 Mu hii kipindi ya mwisho, tuko na lazima ya kushauriana. (2 Ti. 3:1) Bazee biko sawa “mito midogo ya maji katika inchi yenye haina maji” juu banatoa mashauri yenye kutegemea Biblia yenye ndugu na dada biko nayo lazima. (Soma Isaya 32:1, 2.) Barafiki benye banajua mambo yenye tunapenda kusikia lakini banatupatia mashauri yenye tuko nayo lazima, biko sawa “matunda ya mutofaa ya zahabu kwenye vyombo vya feza vyenye kupambwa.” (Mez. 25:11) Basi siye bote tuendelee kujifunza namna ya kutoa mashauri ya muzuri na kuitika mashauri ya muzuri yenye banatupatia.
WIMBO 109 Tupendane Sana Kutoka Ndani ya Moyo