HABARI YA KUJIFUNZA YA 34
WIMBO 3 Nguvu Yangu, Tumaini Yangu, Ninakutegemea
Itika Musamaha wa Yehova
“Ulisamehe kosa la zambi zangu.”—Zb. 32:5.
WAZO KUBWA
Juu ya nini tunapaswa kuitika musamaha wa Yehova na namna Biblia inatuhakikishia kama Yehova anasamehe watenda-zambi wenye wanatubu.
1-2. Tunajisikia namna gani wakati tunatambua kama Yehova ametusamehe? (Ona pia picha ku.)
MUFALME Daudi alifanya makosa makubwa mu maisha yake. Na ile ilifanya zamiri yake imuhukumu sana. (Zb. 40:12; 51:3; utangulizi) Lakini alitubu kwa moyo wote na Yehova alimusamehe. (2 Sa. 12:13) Njo maana Daudi alijua namna mutu anajisikiaka muzuri sana wakati Yehova anamusamehe.—Zb. 32:1.
2 Sawa Daudi na siye tunaweza kujisikia muzuri sana wakati Yehova anatuonyesha rehema. Inagusa moyo sana kujua kama Yehova iko tayari kusamehe zambi zetu, hata zambi nzito, kama tunatubu kwa moyo wote, tunazungumuza na bazee, na tunajikaza juu tusirudilie tena ile zambi! (Mez. 28:13; Mdo. 26:20; 1 Yo. 1:9) Inatia moyo sana kujua kama Yehova anasamehe kabisa-kabisa, na wakati anasamehe inakuwa sawa vile hatuyafanyaka zambi!—Eze. 33:16.
Mufalme Daudi aliandika zaburi za mingi zenye zinazungumuzia musamaha wa Yehova (Ona fungu ya 1-2)
3-4. Dada moya alijisikia namna gani kisha kubatizwa, tutazungumuzia nini mu hii habari?
3 Saa moya inakuwaka nguvu kwako kuitika kama Yehova alishakusamehe? Ni vile Jennifer mwenye alikomalia mu familia ya Mashahidi alijisikia. Wakati alikuwa kijana alianza kufanya mambo ya mubaya mu uficho. Kisha miaka, alimurudilia Yehova na akafikia kubatizwa. Anasema hivi: “Mu maisha yangu ya zamani nilipenda sana makuta, nilikuwa nafanya uasherati, nilikuwa nakunywa sana, na nilikuwa mutu wa bisirani. Nilijua kama kisha kutubu na kuomba Yehova musamaha, Yehova alinisamehe kupitia zabihu ya Kristo. Lakini, ilikuwa nguvu kuhakikishia moyo wangu kama Yehova alishanisamehe.”
4 Na weye inakuwaka nguvu kwako kuitika kama Yehova alishasamehe makosa yako ya zamani? Yehova anapenda tuitike musamaha wake na tujisikie muzuri sawa vile Daudi alijisikia. Mu hii habari tutaona juu ya nini tunapaswa kuitika musamaha wa Yehova, na nini njo itatusaidia tuikubali.
JUU YA NINI TUITIKE MUSAMAHA WA YEHOVA?
5. Shetani anapenda tuwaze nini? Toa mufano.
5 Wakati tunaitika musamaha wa Yehova, tunaepuka kuangukia mu mutego wa Shetani. Kumbuka kama Shetani atafanya yake yote juu tuache kumutumikia Yehova. Atajaribu kutufanya tuamini kama zambi zetu ni za buzito sana mupaka Yehova hawezi kuzisamehe. Fikiria mufano wa mwanaume mwenye alifanya uasherati mu kutaniko ya Korinto kisha akaondolewa mu kutaniko. (1 Ko. 5:1, 5, 13) Wakati ule mwanaume alitubu, Shetani alipenda bandugu mu kutaniko basimusamehe na basimukaribishe. Vilevile Shetani alipenda ule mwanaume awaze kama Yehova hawezi kumusamehe. Ile ingemufanya akuwe na “huzuni yenye kupita kiasi” na aache kumutumikia Yehova. Shetani hayabadilika, angali natumikisha zilezile njia juu ya kutuchochea tuache kumutumikia Yehova. Lakini “hatukose kujua mipango yake ya werevu.”—2 Ko. 2:5-11.
6. Nini njo itatusaidia tuache kujihukumu?
6 Wakati tunakubali musamaha wa Yehova, tunaacha kujihukumu na tunajisikia muzuri. Wakati tunafanya zambi tunakuwaka najihukumu. (Zb. 51:17) Na haiko mubaya kujihukumu juu ile inaweza kutuchochea tufanye mabadiliko na tuanze kufanya mambo ya muzuri. (2 Ko. 7:10, 11) Lakini kama tunaendelea kujihukumu kwa wakati murefu, hata kisha kutubu, tunaweza kuvunjika moyo na kuacha kumutumikia Yehova. Kama tunaamini kabisa kuwa Yehova alishatusamehe, tutaacha kujihukumu na tutaendelea kumutumikia Yehova na zamiri ya muzuri na kwa furaha. Ni vile Yehova anapenda tumutumikie. (Kol. 1:10, 11; 2 Ti. 1:3) Sasa, tutafanya nini juu ya kuhakikishia moyo wetu kama Yehova alishatusamehe?
NINI NJO ITATUSAIDIA TUITIKE MUSAMAHA WA YEHOVA?
7-8. Yehova aliambia Musa kama yeye ni Mungu wa namna gani, na ile inatuhakikishia nini? (Kutoka 34:6, 7)
7 Fikiria mambo yenye Yehova anasema juu yake yeye mwenyewe. Kwa mufano, fikiria mambo yenye Yehova aliambia Musa ku Mulima Sinai.a (Soma Kutoka 34:6, 7.) Kuko mambo mingi yenye Yehova angeambia Musa kuhusu sifa zake na njia zake. Lakini Yehova aliona kama ni jambo ya maana aseme kama yeye ni “Mungu mwenye rehema na huruma.” Waza hata weye, Mungu wa vile atakosa kusamehe mutumishi wake mwenye anatubu kwa moyo wote? Haiwezekane, juu kukosa kusamehe mutu mwenye anatubu ni kukosa huruma na kuwa na roho mubaya. Yehova hawezi kuwa vile hata siku moya.
8 Yehova hawezi kusema bongo, anasemaka tu kweli. Haiwezekane aseme kama ni Mungu mwenye rehema kisha akose kuonyesha rehema. (Zb. 31:5) Kwa hiyo, tunaweza kuamini mambo yenye anasema. Kama ni nguvu kwako kuacha kujihukumu juu ya zambi zako za zamani, ujiulize hivi: ‘Ninaamini kabisa kama Yehova ni Mungu mwenye rehema na huruma na hawezi kukosa kusamehe mutenda-zambi yeyote mwenye anatubu? Kama ninaamini vile, juu ya nini basi nisikubali kama alishanisamehe?’
9. Kusamehe maana yake nini? (Zaburi 32:5)
9 Fikiria mambo yenye Biblia inasema juu ya musamaha wa Yehova. Kwa mufano, fikiria mambo yenye Daudi alisema. (Soma Zaburi 32:5.) Alisema hivi: “Ulisamehe kosa la zambi zangu.” Neno ya Kiebrania yenye kutafsiriwa “kusamehe” inaweza kumaanisha “kunyangula,” ao “kupeleka mbali.” Wakati Yehova alisamehe Daudi ni sawa vile alinyangula muzigo wa zambi wenye Daudi alikuwa nabeba na kuupeleka mbali. Ile ilifanya Daudi ajisikie muzuri na asijihukumu tena. (Zb. 32:2-4) Wakati tulishatubu kwa moyo wote hatupaswe kuendelea kubeba muzigo wa zambi wenye Yehova alishanyangula na kupeleka mbali sana na siye. Tukifanya vile na siye tutajisikia muzuri sawa Daudi.
10-11. Maneno “tayari kusamehe” inatufundisha nini juu ya musamaha wa Yehova? (Zaburi 86:5)
10 Soma Zaburi 86:5. Mu hii andiko Daudi anasema kama Yehova iko “tayari kusamehe.” Kuhusu ile maneno kitabu fulani kinasema hivi juu ya Yehova: “[Yeye] ni mwenye ‘kusamehe,’ ni vile tu ‘njo anakuwaka.’” Juu ya nini Yehova anakuwaka mwenye kusamehe? Sehemu yenye kufuata ya andiko inatusaidia kuelewa. Inasema hivi: “Uko na upendo mwingi mushikamanifu kwa ajili ya wale wote wenye wanakuitia.” Sawa vile tuliona mu habari yenye kutangulia, upendo mushikamanifu unafanya Yehova ashikamane kabisa na baabudu yake baaminifu na hawezi kubaacha hata siku moya. Juu Yehova iko na upendo mushikamanifu, “atasamehe kwa kupenda” batenda-zambi bote benye kutubu. (Isa. 55:7, maelezo ya chini) Kama ni nguvu kwako kuitika musamaha wa Yehova, ujiulize hivi: ‘Ninaamini kama Yehova ni mwenye kusamehe, ni kusema iko tayari kusamehe kila mutu mwenye anatubu na kumulilia amuonyeshe rehema? Kama ninaamini vile, juu ya nini basi nisikubali kama alinisamehe wakati nilimulilia anionyeshe rehema?’
11 Pia, Yehova anaelewa kama tuko batenda-zambi. Kujua ile kunatufariji sana. (Zb. 139:1, 2) Zaburi ingine yenye Daudi aliandika inaonyesha ile jambo. Ile zaburi inaweza pia kutusaidia tuitike musamaha wa Yehova.
USISAABU MAMBO YENYE YEHOVA ANAKUMBUKA
12-13. Sawa vile Zaburi 103:14 inaonyesha, Yehova anakumbuka nini juu yetu, na ile inamuchochea kufanya nini?
12 Soma Zaburi 103:14. Daudi anasema kama Yehova “anakumbuka kwamba tuko mavumbi.” Kwa kutumia ile maneno Daudi anaonyesha sababu moya yenye inafanya Yehova akuwe tayari kusamehe baabudu yake benye banatubu. Ile sababu ni hii: Anajua muzuri kama tuko batenda-zambi. Juu ya kuelewa muzuri, tuchunguze maneno ya Daudi.
13 Daudi anasema kama Yehova “anajua muzuri namna tumeumbwa.” Yehova alituumba “kutoka katika mavumbi ya udongo” na anajua muzuri mambo yenye banadamu biko nayo lazima. Kwa mufano, banapaswa kula, kulala, na kupumua. (Mwa. 2:7) Lakini juu Adamu na Eva balifanya zambi, maneno “tuko mavumbi” inaweza pia kumaanisha kama tuko zaifu juu tuliriti zambi, na ile inafanya tukuwe na muelekeo wa kufanya mambo ya mubaya. Mu Zaburi 103:14 Daudi haseme tu kama Yehova anajua kama tuko batenda-zambi, anasema pia kama Yehova “anakumbuka” kama tuko mavumbi. Wakati Daudi alisema kama Yehova anakumbuka kama tuko mavumbi, alipenda kumaanisha kama Yehova anatutendea kwa huruma juu anajua kama tuko batenda-zambi. Mu kifupi, tunaweza kusema kama Daudi alimaanisha hivi: Yehova anaelewa kama tutakosea wakati fulani. Na wakati tunakosea iko tayari kutuonyesha rehema na kutusamehe kama tunatubu.—Zb. 78:38, 39.
14. (a) Daudi anasema nini juu ya kuonyesha namna Yehova anatusamehe? (Zb. 103:12) (b) Mufano wa Daudi unaonyesha namna gani kama Yehova anasamehe kabisa-kabisa? (Ona kisanduku “Namna Yehova Anasamehe na Kusaabu.”)
14 Zaburi ya 103 inatufundisha nini ingine juu ya namna Yehova anatusamehe? (Soma Zaburi 103:12.) Daudi anasema kama wakati Yehova anasamehe anatia zambi zetu mbali sana, “kama vile mahali jua linatokea [Mashariki] kuko mbali sana na mahali jua linashukia [Mangaribi].” Mashariki inakuwaka mbali sana na mangaribi, hakuna siku zitakutana. Ile inaonyesha nini juu ya zambi zenye Yehova anasamehe? Juu ya ile andiko, kitabu kimoya kinasema kama Mungu anatiaka zambi zetu mbali sana mupaka harufu ya zile zambi inapotea kabisa-kabisa. Waza kidogo, harufu inaweza kutukumbusha jambo fulani. Lakini wakati Yehova anatusamehe ni sawa vile hakuna hata harufu yenye inabakia yenye inaweza kumukumbusha ile zambi na kumufanya atupatie malipizi juu ile zambi.—Eze. 18:21, 22; Mdo. 3:19.
15. Tunaweza kufanya nini kama tunaendelea kujihukumu juu ya zambi zetu za zamani?
15 Maneno ya Daudi yenye kuwa mu Zaburi 103 inatusaidia kuitika musamaha wa Yehova. Kama tunaendelea kujihukumu juu ya zambi zetu za zamani, tujiulize hivi: ‘Ninasaabu mambo yenye Yehova anakumbuka, ni kusema ninasaabu kama Yehova anakumbuka kama niko mutenda-zambi na kama atasamehe batenda-zambi benye kutubu sawa miye? Niko nakumbuka mambo yenye Yehova anaamua kusaabu, ni kusema niko nakumbuka zambi zenye alishanisamehe zenye hawezi tena kunipatia malipizi juu yazo?’ Yehova haendelee kufikiria makosa yetu ya zamani, na siye hatupaswe kuendelea kuifikiria. (Zb. 130:3) Wakati tunaitika musamaha wa Yehova tunaacha kujihukumu na tunaendelea kumutumikia.
16. Juu ya nini ni hatari kuendelea kujihukumu juu ya zambi zetu za zamani? (Ona pia picha.)
16 Mutu mwenye anaendelea kujihukumu juu ya zambi zake za zamani, iko sawa mutu mwenye iko natembeza gari lakini iko naendelea tu kuangalia mu kioo ya kuangalia bya nyuma. Ni muzuri kuangalia mu ile kioo saa moya-moya, juu ile inaweza kufanya aepuke hatari yenye inaweza kutokea nyuma. Lakini ili kutembeza muzuri, mutu anapaswa kuangalia barabara yenye iko mbele yake. Vilevile haiko mubaya kukumbuka saa moya-moya makosa yetu ya zamani, juu ile inaweza kutusaidia tujifunze kupitia ile makosa na tujikaze juu tusiirudilie tena. Lakini kama tunaendelea kufikiria sana makosa yetu ya zamani, ile itafanya tuendelee kujihukumu na tusimutumikie Yehova muzuri. Kwa hiyo, ni muzuri tukazie akili barabara yenye iko mbele yetu. Tuko mu barabara yenye inaongoza mu ulimwengu mupya wenye Mungu ametuahidi. Na mu ule ulimwengu, mambo ya mubaya “hayatakumbukwa.”—Isa. 65:17; Mez. 4:25.
Sawa vile shofere anapaswa kuangalia sana mbele yake kuliko kuangalia mu kioo ya kuonyesha bya nyuma, tunapaswa kukazia akili baraka zenye tutapata mu siku zenye ziko nakuya kuliko kuendelea kufikiria makosa yetu ya zamani (Ona fungu ya 16)
ENDELEA KUHAKIKISHIA MOYO WAKO
17. Juu ya nini tunapaswa kuendelea kuhakikishia moyo wetu kama Yehova anatupenda na iko tayari kutusamehe?
17 Tunapaswa kuendelea kuhakikishia moyo wetu kama Yehova anatupenda na iko tayari kutusamehe. (1 Yo. 3:19, maelezo ya chini) Juu ya nini tujihakikishie vile? Juu Shetani ataendelea kufanya yake yote ili kutufanya tuamini kama Yehova hatupendi na hawezi kutusamehe. Kusudi yake ni moya: kutufanya tuache kumutumikia Yehova. Na hatachoka juu anajua kama anabakia na wakati kidogo sana. (Ufu. 12:12) Tusimuache atudanganye!
18. Unaweza kufanya nini juu ya kuhakikishia moyo wako kama Yehova anakupenda na iko tayari kusamehe?
18 Juu ukuwe hakika kama Yehova anakupenda, tumikisha mambo yenye tulijifunza mu habari yenye ilitangulia. Juu uhakikishie moyo wako kama Yehova alishakusamehe, fikiria mambo yenye Yehova anasema juu yake mwenyewe. Fikiria mambo yenye Biblia inasema juu ya musamaha wake. Kumbuka kama Yehova anajua kama uko mutenda-zambi na atakutendea kwa rehema. Usisaabu kama Yehova anajua kama uko mutenda-zambi na atakutendea kwa rehema. Na ukumbuke kama wakati anasamehe, anasamehe kabisa-kabisa. Ukifanya vile, utakuwa hakika kama Yehova ni Mungu mwenye rehema na utasema hivi sawa Daudi: “Asante Yehova kwa kusamehe ‘kosa la zambi zangu’!”—Zb. 32:5.
WIMBO 1 Sifa za Yehova
a Ona habari “Mkaribie Mungu—Yehova Alipofunua Sifa Zake,” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 5, 2009.