NAMNA YA KUJIFUNZA
Tumikisha Referanse za Katikati
Referanse za katikati za mu Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya zinaonyesha namna Biblia inapatana. Zinakusaidia kupata maandiko yenye kuwa na habari zingine zenye kupatana na mambo yenye uko nasoma. Juu ya kupata referanse, utaona ka herufi ka kidogo pembeni ya neno. Sasa juu upate maandiko yenye inapatana na mambo yenye uko nasoma, mu Biblia yenye kuchapishwa utafute herufi yenye inafanana na kale ka herufi kenye kiko pembeni ya ile neno; uitafute ku liste yenye kuwa katikati ya ukurasa ao pembeni. Ku jw.org ao ku JW Library® gusa kale ka herufi kisha maandiko itaonekana.
Referanse za katikati zinaweza kukupeleka ku maandiko yenye kuzungumuzia mambo yenye kufuata:
Habari ileile: Mu referanse utapata maandiko yenye inazungumuzia ileile habari. Kwa mufano, ona 2 Samweli 24:1 na 1 Mambo ya Nyakati 21:1.
Kwenye maneno ilitoka: Referanse itakuonyesha kwenye maneno yenye uko nasoma ilitoka. Kwa mufano Matayo 4:4 na Kumbukumbu la Torati 8:3.
Utimizo wa unabii: Referanse itakuonyesha maandiko yenye inazungumuzia utimizo wa unabii wenye uko nasoma. Kwa mufano, Matayo 21:5 na Zekaria 9:9.