Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 9 uku. 14-19
  • Heshimia Bengine

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Heshimia Bengine
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • HESHIMA MAANA YAKE NINI?
  • HESHIMIA BATU YA FAMILIA
  • HESHIMIA NDUGU NA DADA MU KUTANIKO
  • HESHIMIA BATU BENYE HABIKO MASHAHIDI
  • Heshima Imeenda Wapi?
    Amuka!—2024
  • Juu ya Nini Tuheshimie Mamlaka?
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Namna ya Kuonyesha Heshima
    Amuka!—2016
  • Sababu Gani Tunapaswa Kuheshimu Mamlaka?
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 9 uku. 14-19

HABARI YA KUJIFUNZA YA 38

WIMBO 120 Tukuwe Wapole Kama Kristo

Heshimia Bengine

“Kuheshimiwa ni muzuri kuliko feza na zahabu.”—MEZ. 22:1.

WAZO KUBWA

Juu ya nini tunapaswa kuheshimia bengine na namna ya kufanya vile hata wakati haiko mwepesi.

1. Juu ya nini banadamu banasikiaka muzuri wakati bengine banabaheshimia? (Mezali 22:1)

UNASIKIAKA muzuri wakati bengine banakuheshimia? Bila shaka ndiyo. Siye bote tunakuwaka na lazima ya kuheshimiwa. Biblia inasema kama “kuheshimiwa ni muzuri kuliko feza na zahabu”!—Soma Mezali 22:1.

2-3. Juu ya nini wakati fulani haikuwake mwepesi kuheshimia bengine, na tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Wakati fulani haikuwake mwepesi kuheshimia bengine. Juu ya nini? Sababu moya ni juu tunaonaka uzaifu wabo. Tena tunaishi wakati yenye batu mingi habaheshimiane. Lakini siye tunapaswa kuwa tofauti juu Yehova anapenda tuheshimie “watu wa namna zote.”—1 Pe. 2:17.

3 Mu hii habari tutaona maana ya kuheshimia bengine na namna tunaweza kuheshimia (1) batu ya familia, (2) baabudu benzetu, na (3) batu bengine benye habiko Mashahidi. Tutaona zaidi sana namna tunaweza kuonyesha heshima wakati haiko mwepesi kufanya vile.

HESHIMA MAANA YAKE NINI?

4. Heshima maana yake nini?

4 Heshima maana yake nini? Heshima inahusu namna tunaona mutu na namna tunamutendea. Wakati tunaona mutu iko na sifa za muzuri ao amefanya mambo ya muzuri, ao tena wakati iko na mamlaka fulani juu yetu, tunamutendea mu namna yenye inaonyesha kama tunamuheshimia. Ni jambo ya maana tuheshimie bengine kutoka ku moyo.—Mt. 15:8.

5. Nini njo inapaswa kutuchochea kuheshimia bengine?

5 Yehova anapenda tuheshimie bengine. Kwa mufano, anatuomba tuheshimie “mamlaka zenye kuwa kubwa.” (Ro. 13:​1, 7) Lakini mutu anaweza sema hivi: “Niko tayari kuheshimia mutu kama ule mutu anastahili heshima.” Ni muzuri kuwaza vile? Hapana! Juu tuko batumishi ya Yehova tunaelewa kama tunapaswa kuheshimia bengine, haiko juu tu ya matendo yabo, lakini juu tunapenda Yehova na tunapenda kumufurahisha.—Yos. 4:14; 1 Pe. 3:15.

6. Inawezekana kuheshimia mutu mwenye hakuheshimie? Fasiria. (Ona pia picha.)

6 Batu mingi banasemaka: “Heshima kuheshimiana.” Mawazo ya vile inaweza kufanya tujiulize: ‘Inawezekana kabisa kuheshimia mutu mwenye hakuheshimie?’ Ndiyo, inawezekana. Tuone mifano fulani. Mufalme Sauli alizarau mutoto yake Yonatani mbele ya batu. (1 Sa. 20:​30-34) Lakini Yonatani aliendelea kumuheshimia na alimuunga mukono ku vita mupaka mwisho wa maisha yabo. (Kut. 20:12; 2 Sa. 1:23) Kuhani Mukubwa Eli alisema kama Hana analewa. (1 Sa. 1:​12-14) Lakini Hana alimujibia kwa heshima, hata kama mu Israeli yote balijua kama Eli hakukuwa baba muzuri na hakukuwa kuhani mukubwa muzuri. (1 Sa. 1:​15-18; 2:​22-24) Pia, batu ya Atene balitukana mutume Paulo, balimuita “musema-mingi.” (Mdo. 17:18) Hata vile Paulo alizungumuza nabo kwa heshima. (Mdo. 17:22) Ile mifano inaonyesha wazi kama, ikiwa tunamupenda Yehova na tunaogopa kumuhuzunisha, tutajikaza kuheshimia bengine hata wakati haiko mwepesi kufanya vile. Tuone sasa nani njo tunapaswa kuheshimia na juu ya nini.

Yonatani, Sauli, na baaskari Baisraeli biko napigana na mipanga na mikuki, na biko na ngao.

Yonatani aliendelea kutegemeza utawala wa baba yake hata kama baba yake alimuzarau (Ona fungu ya 6)


HESHIMIA BATU YA FAMILIA

7. Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kwetu kuheshimia batu ya familia?

7 Juu ya nini inaweza kuwa nguvu? Tunapitishaka wakati mingi pamoya na batu ya familia yetu, njo maana tunajuaka sifa zao na uzaifu wao. Bamoya banaweza kuwa na magonjwa yenye inafanya ikuwe nguvu kubahangaikia na bengine banaweza kuwa na mahangaiko ya mingi. Bengine banaweza hata kufanya ao kusema mambo yenye inatukwaza. Familia inapaswa kuwa fasi ya amani kwenye mutu anajisikia kuwa salama. Lakini kama batu mu familia habatendeane kwa heshima ile inaweza kuleta muvurugo na ile itafanya mu familia musikuwe umoja. Familia iko sawa vile mwili. Magonjwa fulani inaweza kufanya sehemu fulani za mwili zisitumike pamoya muzuri. Vilevile kama mu familia batu habaheshimiane ile inaweza kufanya basikuwe na umoja. Lakini, vile tu magonjwa ya mingi inaweza kutunziwa, batu ya familia nabo banaweza kujifunza kuheshimiana.

8. Juu ya nini ni jambo ya maana tuheshimie batu ya familia yetu? (1 Timoteo 5:​4, 8)

8 Juu ya nini tuonyeshe heshima? (Soma 1 Timoteo 5:​4, 8.) Mu barua yake ya kwanza kwa Timoteo, Paulo anazungumuzia namna batu ya familia banapaswa kuhangaikiana. Anaonyesha kama tunapaswa kuheshimia batu ya familia yetu kwa kuhangaikia mahitaji yabo. Na sababu kubwa yenye inapaswa kutuchochea kufanya vile ni “ushikamanifu kwa Mungu,” haiko juu tu tunalazimika kufanya vile. Ile inaonyesha kama tunaheshimia batu ya familia yetu juu tunamupenda Yehova na tunaona kama kufanya vile ni sehemu ya ibada yetu. Ni Yehova njo alianzisha familia. (Efe. 3:​14, 15) Kwa hiyo wakati tunaheshimia batu ya familia yetu ni Yehova, mwenye alianzisha familia, njo tunaheshimia. Ile ni sababu kubwa kabisa ya kuheshimia batu ya familia yetu!

9. Namna gani bibi na bwana banaweza kuonyeshana heshima? (Ona pia picha.)

9 Namna ya kuonyesha heshima. Bwana mwenye anaheshimia bibi yake anamuonyeshaka kama ni wa maana wakati biko na batu bengine lakini pia wakati biko abo bawili tu. (Mez. 31:28; 1 Pe. 3:7) Hamupige, hamuzarau, ao kumufanya ajisikie kama haiko wa maana. Ariel,a mwenye anaishi Argentina, anasema hivi: “Bibi yangu iko na ugonjwa fulani wenye unafanyaka wakati fulani aseme mambo ya kuumiza. Wakati ile inatokea, ninajikaza kukumbuka kama byenye anasema habitoke ku moyo. Pia ninakumbukaka 1 Wakorinto 13:​5, yenye inanisaidia nizungumuze naye kwa heshima hapana kwa ukali.” (Mez. 19:11) Bibi anaonyesha kama anaheshimia bwana yake kwa kusema mambo ya muzuri kuhusu bwana yake. (Efe. 5:33) Anaepuka kumuzarau, kumupanga tumajina-jina na kufanya mizaha ya kumushushia heshima; anajua kama kufanya ile mambo inaweza kuharibisha ndoa yake. (Mez. 14:1) Dada fulani wa mu Italia, mwenye bwana yake anakuwaka na mahangaiko sana anasema hivi: “Wakati fulani ninaonaka kama bwana yangu ananenepeshaka sana mambo. Zamani maneno na sura yangu ilikuwa inaonyesha tu kama simuheshimie. Lakini nimeona kama kupitisha wakati na batu benye banazungumuzia bengine kwa heshima kumenisaidia niheshimie zaidi bwana yangu.”

Picha: Bibi na bwana biko natendeana kwa heshima. 1. Bwana iko nazungumuza na bibi yake kwa upole wakati biko napiga chakula mu mafiga. 2. Bibi anatapa bwana yake mbele ya bageni wakati iko nabaletea chakula.

Wakati tunaheshimia batu ya familia yetu, tunaheshimia Yehova Kichwa ya familia (Ona fungu ya 9)


10. Namna gani vijana wanaweza kuonyesha kama wanaheshimia bazazi?

10 Vijana, mutii sheria zenye bazazi yenu banabatilia. (Efe. 6:​1-3) Muongee nabo kwa heshima. (Kut. 21:17) Vile bazazi yenu biko nakomala, batakuwa na lazima mubahangaikie zaidi. Mujikaze kubahangaikia. Tuone mufano wa Maria mwenye baba yake haiko Shahidi wa Yehova. Wakati baba yake aligonjwa, Maria alikuwa namuhangaikia, lakini haikukuwa mwepesi juu baba yake alikuwa namutendea mubaya. Maria anasema hivi: “Niliomba Yehova anisaidie niheshimie baba yangu na nionyeshe ile heshima kwa matendo. Nilijiambia kama, juu ni Yehova njo ananiomba niheshimie baba yangu, ni kusema anaweza kunipatia nguvu ya kufanya vile. Kisha wakati, nilifikia kuelewa kama haiko lazima baba yangu abadilike juu nimutendee kwa heshima.” Wakati tunaheshimia batu ya familia yetu hata kama biko na uzaifu fulani, tunaonyesha kama tunaheshimia Yehova mwenye alianzisha familia.

HESHIMIA NDUGU NA DADA MU KUTANIKO

11. Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kuheshimia bandugu na badada yetu?

11 Juu ya nini inaweza kuwa nguvu? Bandugu na badada banajikaza kutumikisha kanuni za Biblia mu maisha yabo. Lakini, wakati fulani banaweza kututendea mubaya, kutuhukumu bila haki, ao kutuuzi. Kama Mukristo mwenzetu anatupatia “sababu ya kulalamika,” inaweza kuwa nguvu kuendelea kumuheshimia. (Kol. 3:13) Nini njo inaweza kutusaidia tuendelee kumuheshimia?

12. Juu ya nini ni jambo ya maana tuheshimie Bakristo benzetu? (2 Petro 2:​9-12)

12 Juu ya nini tuonyeshe heshima? (Soma 2 Petro 2:​9-12.) Mu barua yake ya pili, Petro anazungumuzia batu fulani mu kutaniko ya karne ya kwanza benye balikuwa nasema bila heshima kuhusu “watukufu,” ni kusema bazee Bakristo. Wakati malaika waaminifu waliona ile walitenda namna gani? “Kwa sababu wanamuheshimia Yehova,” malaika hawakusema hata neno moya ya kutukana bale batu! Ni jambo ya ajabu kabisa! Malaika wakamilifu walikatala kusema mubaya juu ya bale banaume benye kiburi, lakini baliacha Yehova njo abahukumu na abakaripie. (Ro. 14:​10-12; linganisha na Yuda 9.) Mufano wa malaika unatufundisha nini? Unatufundisha kama tunapaswa kuheshimia batu benye banatupinga. Sasa kama tunapaswa kuheshimia batu benye banatupinga, hauone kama tunapaswa kuheshimia hata zaidi Bakristo benzetu? Tunapaswa “kuwa wa kwanza” kubaheshimia. (Ro. 12:10) Kama tunafanya vile tunaonyesha kama tunaheshimia Yehova.

13-14. Namna gani tunaweza kuheshimia ndugu na dada mu kutaniko? Toa mufano. (Ona pia picha.)

13 Namna ya kuonyesha heshima. Bazee, mujikaze kufundisha bengine kwa upendo. (Flm. 8, 9) Kama inaomba mushaurie mutu mujikaze kufanya vile kwa upole, hapana saa mulishakasirika. Dada, munaweza kusaidia bengine mu kutaniko baheshimiane kwa kuepuka kusemana mubaya ao kusingiziana bya bongo. (Tit. 2:​3-5) Siye bote tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia bazee kwa kutii muongozo wabo na kwa kubashukuru juu ya kazi ya nguvu yenye biko nafanya juu ya kuongoza mikutano, kusimamia kazi ya kuhubiri, na kusaidia bale benye balishakamata “hatua fulani ya mubaya.”—Gal. 6:1; 1 Ti. 5:17.

14 Ilikuwa nguvu kwa dada mwenye kuitwa Rocío kuheshimia muzee fulani mwenye alimushauria. Rocío anasema hivi: “Niliona sawa vile ule muzee hakuzungumuza na miye kwa upole. Wakati nilikuwa ku nyumba nilikuwa nasema mubaya juu yake. Hata kama sikuonyesha waziwazi, mu roho yangu niliona sawa vile hakukuwa tu ananihangaikia. Na sikufuata mashauri yake.” Nini njo ilisaidia Rocío? Anasema hivi: “Mu usomaji wangu wa Biblia, nilisoma 1 Watesalonike 5:​12, 13. Ile andiko ilinisaidia nitambue kama sikukuwa naonyesha ule ndugu heshima, na zamiri yangu ilianza kunisumbua. Nilisali kwa Yehova na nikafanya utafiti mu bichapo yetu juu nipate habari yenye ingenisaidia nibadilishe mawazo yangu. Ku mwisho nilielewa kama tatizo haikukuwa ule ndugu, miye njo sikukuwa najishusha. Sasa ninaelewa kama juu mutu aweze kuheshimia bengine anapaswa kuwa munyenyekevu. Ningali najikaza juu niheshimie zaidi bengine na ninajua kama Yehova anafurahi kuona vile niko najikaza.”

Picha: Dada mwenye kuzeeka iko nasoma Biblia na iko nafikiria namna bazee banatumikaka sana mu njia mbalimbali. 1. Muzee iko natoa hotuba ku mukutano. 2. Iko nasaidia ndugu mwenye iko mu kinga ya bilema. 3. Iko natosha teluji inje ya Jumba ya Ufalme.

Siye bote tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia bazee kwa kutii muongozo wabo na kwa kubashukuru juu ya kazi ya nguvu yenye biko nafanya (Ona fungu ya 13-14)


HESHIMIA BATU BENYE HABIKO MASHAHIDI

15. Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kuonyesha heshima batu benye habiko Mashahidi?

15 Juu ya nini inaweza kuwa nguvu? Mu mahubiri tunakutanaka na batu benye habahangaikie Mungu wala Biblia. (Efe. 4:18) Bamoya banakatala kutusikiliza juu ya namna balikomala. Ku kazi unaweza kutumika na batu ba mihali-mihali ao shefu mwenye hata ufanye nini hafurahiake. Ku masomo pengine banafunzi benzako banaoneanaka na mwalimu wako hafurahiake byote byenye unafanyaka. Kisha wakati unaweza kuacha kuheshimia batu ya vile na unaweza kuacha kubatendea muzuri.

16. Juu ya nini ni jambo ya maana kuheshimia batu benye habayaanza kumutumikia Yehova? (1 Petro 2:12; 3:15)

16 Juu ya nini tuonyeshe heshima? Kumbuka kama Yehova anaangalia namna tunatendea bale benye habayaanza kumutumikia. Mutume Petro alikumbusha Bakristo kama mufano wao muzuri unaweza kuchochea watu fulani “wamutukuze Mungu.” Njo maana alibashauria batetee imani yabo “kwa upole na heshima kubwa.” (Soma 1 Petro 2:12; 3:15.) Ikuwe biko nasamba ku tribinali ao biko nazungumuza na mutu mwingine juu ya imani yabo, Bakristo banapaswa kutendea kwa heshima batu benye habaamini, sawa tu vile bangefanya ikiwa Mungu angekuwa mbele yabo. Tukumbuke kama Yehova iko naangalia na iko nasikiliza maneno yenye tunasema na namna tunaisema. Ile ni sababu kubwa ya kutuchochea tuheshimie batu benye habiko Mashahidi!

17. Namna gani tunaweza kuheshimia batu benye habiko Mashahidi?

17 Namna ya kuonyesha heshima. Saa tuko mu mahubiri tunaepuka kufanya ionekane sawa vile bengine habana akili juu habajue mambo mingi kuhusu Biblia. Lakini tunapenda kuona bengine kuwa ba maana kwa Mungu na bazuri zaidi kutupita. (Hag. 2:7; Flp. 2:3) Kama mutu anakutukana juu ya mambo yenye unaamini, ujizuie usimurudishie. Kwa mufano tutaepuka kusema maneno yenye inaweza kufanya ionekane sawa vile siye njo tuko na akili na abo habajue kitu. (1 Pe. 2:23) Kama tunasema jambo yenye hatukupaswa kusema tulombe musamaha palepale. Namna gani unaweza kuonyesha heshima ku kazi? Ujikaze kuwa mufanyakazi mwenye bidii na ujikaze kuona sifa za muzuri za bafanyakazi benzako ao bashefu yako. (Tit. 2:​9, 10) Kama unatumikaka sana mu kazi na unasemaka kweli, batu bakufurahie ao hapana, ya lazima unamufurahisha Mungu.—Kol. 3:​22, 23.

18. Juu ya nini ni jambo ya maana tuendelee kuheshimia bengine?

18 Tuko na sababu za mingi za muzuri za kuheshimia bengine. Tumeona kama wakati tunaheshimia batu ya familia yetu, tunaheshimia Yehova, Kichwa ya familia. Na wakati tunaheshimia ndugu na dada zetu mu kutaniko, ni Yehova Baba yetu wa mbinguni njo tunaheshimia. Na tena, kama tunaheshimia batu benye habiko Mashahidi, pengine siku moya itakuwa mwepesi kwabo kumutukuza ao kumuheshimia Yehova, Mungu wetu Mukubwa. Hata kama banadamu benzetu habatuheshimie, siye tuendelee tu kubaheshimia. Juu ya nini? Juu Yehova atatubariki. Anaahidi hivi: “Wale wenye kuniheshimia nitawaheshimia.”—1 Sa. 2:30.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Namna gani tunaweza kuheshimia batu ya familia yetu?

  • Namna gani tunaweza kuheshimia ndugu na dada zetu mu kutaniko?

  • Namna gani tunaweza kuheshimia batu benye habiko Mashahidi?

WIMBO 129 Tutaendelea Kuvumilia

a Majina fulani imebadilishwa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine