Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 9 uku. 31
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Habari Zenye Kuwa Katika Wimbo wa Sulemani
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • Yehova Anamupatia Nguvu Mutu Mwenye Kuchoka
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Mambo Yenye Tunajifunza Kupitia Ndege wa Mbinguni
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • “Hakuna Hata Mumoja Wenu Mwenye Atapotea”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 9 uku. 31

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Mwenye aliandika Mezali 30:​18, 19 alisema kama “njia ya mwanaume pamoja na kijana mwanamuke” ilikuwa ya ‘kupita uelewaji.’ Alimaanisha nini?

Ile maneno imevuruga batu mingi, hata batu benye elimu. Ile andiko yote inasema hivi mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya: “Kuko mambo tatu (3) yenye kunipita uelewaji, [ao, “yenye kuwa ya ajabu sana,” maelezo ya chini], na mambo ine (4) yenye sielewe: Njia ya tai katika mbingu, njia ya nyoka juu ya mwamba, njia ya mashua katika bahari kubwa, na njia ya mwanaume pamoja na kijana mwanamuke.” —Mez. 30:​18, 19.

Zamani tuliwaza kama maneno “njia ya mwanaume pamoja na kijana mwanamuke” ilikuwa nazungumuzia jambo ya mubaya. Juu ya nini tuliwaza vile? Juu mistari ingine ya mu Mezali 30 inazungumuzia mambo ya mubaya yenye haisemake “inaenea.” (Mez. 30:​15, 16) Mustari wa 20 unazungumuzia “mwanamuke muzinifu” mwenye anasema kama hakufanya jambo yoyote ya mubaya. Kwa hiyo tuliwaza kama sawa vile tai inapitaka mu anga, nyoka inapitaka ku lijiwe, na mashua inapitaka mu bahari bila kuacha alama yoyote fasi kwenye ilipita, mwanaume anaweza kufanya jambo fulani bila mutu yeyote kujua byenye alifanya. Njo maana tuliwaza kama maneno “njia ya mwanaume pamoja na kijana mwanamuke” inazungumuzia jambo ya mubaya, ni kusema, kijana mwanaume mujanja mwenye anatongoza kijana mwanamuke na nia mubaya bila ule mwanamuke kutambua.

Lakini kuko sababu zenye zinatuchochea kuona kama ile andiko haizungumuzie jambo ya mubaya. Mwenye aliandika maneno ya ile andiko alikuwa tu nazungumuzia mambo ya ajabu yenye inamushangazaka.

Maandishi ya zamani ya Kiebrania inaonyesha pia kama ile andiko inazungumuzia jambo ya muzuri. Kitabu fulani inaonyesha kama neno ya Kiebrania yenye inatumiwa ili kutafsiri “kunipita uelewaji “ mu Mezali 30:18 “inazungumuzia jambo yenye . . . mutu anaona kuwa haiko ya kawaida, ya ajabu, na hata ya kushangaza.”

Crawford H. Toy, mwalimu ku Masomo ya Juu ya Harvard mu Amerika, anasema pia kama ile andiko ya Biblia haizungumuzie jambo ya mubaya. Anasema hivi: “Muandikaji anapenda tu kuonyesha namna mambo yenye anataya ni ya ajabu.”

Kwa hiyo, tunaweza kusema kama maneno yenye iko mu Mezali 30:​18, 19 inazungumuzia mambo ya ajabu kabisa, na hata yenye hatuwezi kuelewa. Kama tu muandikaji wa Biblia mwenye aliandika ile maneno, tunashangala kuona namna tai inaruka mu hewa, namna nyoka yenye haina migulu inapita haraka ku majiwe, namna mashua ya buzito inatembea yulu ya bahari, na namna kijana mwanaume na kijana mwanamuke banaweza kupendana na kuishi pamoya kwa furaha.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine