HABARI YA KUJIFUNZA YA 42
WIMBO 44 Sala ya Mutu wa Hali ya Chini
Namna ya Kusali kwa Moyo Wote
“Ninakuita kwa moyo wangu wote. Unijibu, Ee Yehova.”—ZB. 119:145.
WAZO KUBWA
Kufikiri juu ya sala zenye ziliandikwa mu Biblia kunaweza kutusaidia kusali kwa moyo wote.
1-2. (a) Ni nini inaweza kutusaidia kufungulia Yehova moyo wetu? (b) Tunajua namna gani kama Yehova anafurahia kusikiliza sala zetu?
WAKATI fulani unaonaka sawa vile uko narudilia maneno ileile mu sala ao sala zako zilishakuwa tu za yuluyulu? Juu tuko na bya mingi bya kufanya, wakati fulani tunafanyaka tu sala za mbiombio. Ao wakati fulani tunaweza kujizuia kufungulia Yehova moyo wetu juu tunajiona kama hatustahili.
2 Biblia inatuhakikishia kama byenye Yehova anaangaliaka haiko maneno ya ajabu-ajabu yenye tunatia mu sala, lakini ni kusali kwa moyo wote. Anasikilizaka “ombi la wapole.” (Zb. 10:17) Anasikilizaka kwa uangalifu mambo yote yenye tunamuambia juu anatuhangaikia kabisa.—Zb. 139:1-3.
3. Tutazungumuzia maulizo gani mu hii habari?
3 Tunaweza kujiuliza hivi: Juu ya nini tunapaswa kujisikia huru kusali kwa Yehova? Tunaweza kufanya nini juu sala zetu zitoke ku moyo? Namna gani kufikiri juu ya sala zenye ziko mu Biblia kunaweza kutusaidia kusali kutoka ku moyo? Na tutafanya nini kama tuko na mahangaiko sana mupaka tunakosa maneno ya kusema juu ya kuelezea Yehova namna tuko najisikia? Tuzungumuzie basi majibu ya ile maulizo.
USIJIZUIE KUSALI KWA YEHOVA
4. Nini njo inaweza kukusaidia usijizuie kusali kwa Yehova? (Zaburi 119:145)
4 Wakati tunaelewa kama Yehova ni rafiki mushikamanifu na anapenda tukuwe na maisha ya muzuri, tunajisikia huru kumuambia mambo yote yenye iko mu moyo wetu. Mwenye aliandika Zaburi 119 alijikaza kumuona Yehova kuwa rafiki mushikamanifu. Alipata magumu mu maisha. Batu babaya balimusemea bongo. (Zb. 119:23, 69, 78) Na wakati fulani alivunjika moyo kwa sababu ya uzaifu wake. (Zb. 119:5) Lakini ile yote haikumuzuia kumufungulia Yehova moyo wake.—Soma Zaburi 119:145.
5. Juu ya nini hatupaswe kujizuia kusali kwa Yehova kama tumefanya makosa? Leta mufano.
5 Yehova anapenda batu yote basali kwake, hata bale benye bamefanya zambi nzito. (Isa. 55:6, 7) Njo maana hatupaswe kujizuia kusali kwa Yehova hata kama tumefanya makosa. Fikiria hii mufano: Tuseme unaenda kutembelea fasi yenye hauyafikaka. Kisha wakati uko kule, unapotea njia. Lakini ukiuliza mutu wa kule, atakuonyesha njia. Utajizuia kuuliza juu unasikia haya vile unapotea? Hapana. Na siye wakati fulani tunaweza kupotea njia ao kufanya zambi. Lakini ile isituzuie kusali kwa Yehova.—Zb. 119:25, 176.
NAMNA YA KUSALI KUTOKA KU MOYO
6-7. Namna gani kufikiri juu ya sifa za Yehova kunaweza kukusaidia usali kutoka ku moyo? Leta mufano. (Ona pia maelezo ya chini.)
6 Wakati tunazungumuza na Yehova na tunamuambia mawazo yetu yote na byote byenye biko ku moyo wetu, tunamukaribia zaidi. Sasa, nini njo inaweza kutusaidia tufungulie Yehova moyo wetu?
7 Fikiri juu ya sifa za Yehova.a Wakati tunafikiri juu ya sifa za Yehova inakuwa mwepesi zaidi kwetu kumufungulia moyo wetu. (Zb. 145:8, 9, 18) Fikiria mufano wa Kristine, mwenye baba yake alikuwa natendea mubaya. Anasema hivi: “Juu baba yangu alikuwa nanitendea mubaya ilikuwa nguvu kwangu kuamini kama Yehova ni Baba mwenye upendo mwenye ninaweza ongea naye. Niliwaza kama makosa yangu itafanya Yehova aniache.” Ni sifa gani ya Yehova njo inamusaidiaka? Anasema hivi: “Upendo mushikamanifu wa Yehova unafanya nijisikie kuwa salama. Ninajua kama hawezi kuniacha. Hata kama ninaanguka, atanisimamisha kwa upendo. Ile inanisaidia nijisikie huru kumufungulia moyo wangu, kumuambia mambo yenye inanifurahisha na mambo yote yenye inanihangaisha.”
8-9. Juu ya nini ni muzuri kufikiria mambo yenye utasema mbele usali? Leta mufano.
8 Fikiria mambo yenye utasema. Mbele ya kusali unaweza kujiuliza maulizo fulani. Kwa mufano: Niko na magumu gani hii wakati? Kuko mutu mwenye ninapaswa kusamehe? Kuko jambo fulani yenye imetokea mu maisha yangu na niko na lazima ya musaada wa Yehova juu nijue namna ya kuipiganisha? (2 Fa. 19:15-19) Tunaweza pia kufuata sala ya mufano yenye Yesu alituachia na kufikiri juu ya mambo yenye tunaweza kuomba Yehova kuhusu jina yake, Ufalme wake, na mapenzi yake.—Mt. 6:9, 10.
9 Wakati dada mwenye jina yake Aliska alijua kama bwana yake hataishi tena siku mingi juu ya kansere ya ubongo, ilikuwa nguvu kwake kusali. Anakumbuka hivi: “Nilikuwa na mahangaiko ya mingi mupaka nilishindwa niseme nini mu sala.” Nini njo ilimusaidia? Anasema hivi: “Nilikuwa nakamata wakati kidogo mbele ya kusali juu ya kuwaza byenye nitasema. Ile ilinisaidia nisikuwe nazungumuzia tu magumu yangu mu sala. Kufanya vile kumenisaidia nitulie wakati niko nasali na nisali juu ya mambo mbalimbali.”
10. Juu ya nini tunapaswa kujikaza kufanya sala za murefu? (Ona pia picha.)
10 Fanya Sala za murefu. Tunaweza kuambia Yehova mambo yenye iko ku moyo wetu hata mu sala za mufupi. Lakini wakati tunafanya sala za murefu tunakuwa na wakati zaidi ya kufungulia Yehova moyo wetu.b Elijah bwana ya Aliska, anasema hivi: “Ninajikazaka kusali mara mingi ku siku. Na kufanya sala za murefu kumenisaidia kumukaribia Yehova. Ninaweza kawia na niko nasali juu Yehova iko na wakati yote ya kunisikiliza.” Pima kufanya hivi: Chagula saa na fasi kwenye unaweza kusali kwa wakati murefu bila kukengeushwa. Ukipenda unaweza hata kusali kwa sauti. Kisha ujikaze kukuwa nafanya vile kila mara.
Chagula fasi na saa yenye unaweza kusali kwa wakati murefu (Ona fungu ya 10)
FIKIRIA SALA ZENYE ZIKO MU BIBLIA
11. Tunapata faida gani wakati tunafikiria sala za batumishi ya Yehova zenye ziko mu Biblia? (Ona pia kisanduku “Hali Yako Inafanana Yabo?”)
11 Unaweza kupata faida kama unafikiri juu ya sala, nyimbo, ao zaburi zenye ziko mu Biblia. Wakati utaona vile batumishi ya Yehova baliambia Yehova mambo yenye ilikuwa kabisa ndani ya moyo wao, ile itakusaidia na weye ufungulie Yehova moyo wako. Unaweza hata kupata maneno ya kumusifu Yehova yenye na weye unaweza kutia mu sala zako. Na inawezekana utapata sala za batumishi ya Yehova benye balikuwa mu hali sawa yako.
12. Tunaweza kujiuliza maulizo gani wakati tuko nafikiria sala fulani yenye iko mu Biblia?
12 Wakati uko nafikiria sala fulani yenye iko mu Biblia, ujiulize hii maulizo: ‘Nani njo alisema hii maneno na alikuwa mu hali gani? Hali yenye alikuwa ndani wakati alisema hii maneno njo yenye na miye niko ndani? Sala yenye alitoa inanifundisha nini?’ Pengine itaomba utafute habari zaidi juu ya kujibia ile maulizo na utapata faida kabisa kama unafanya vile. Tuone mifano fulani.
13. Sala ya Hana inatufundisha nini? (1 Samweli 1:10, 11) (Ona pia picha.)
13 Soma 1 Samweli 1:10, 11. Wakati Hana alitoa hii sala kulikuwa mambo mbili yenye ilikuwa namusumbua. (1) Hakukuwa nazala, na (2) bibi mwingine wa bwana yake alikuwa namutendea mubaya. (1 Sa. 1:4-7) Kama uko na tatizo yenye haipendi kuisha, sala ya Hana inaweza kukufundisha nini? Alisali kwa Yehova kwa wakati murefu na alimutupia muzigo wake kwa kumuambia mambo yote yenye ilikuwa ku moyo wake, na ile ilimutuliza. (1 Sa. 1:12, 18) Na siye tunaweza kutulia wakati ‘tunamutupia Yehova muzigo wetu’ kwa kumuambia magumu yetu na namna ile magumu inafanya tujisikie.—Zb. 55:22.
Hana hakukuwa nazala, na bibi mwingine wa bwana yake alikuwa namutendea mubaya. Lakini hana alimufungulia Yehova moyo wake (Ona fungu ya 13)
14. (a) Mufano wa Hana unatufundisha nini ingine? (b) Namna gani kusoma Biblia na kutafakari kunaweza kutusaidia tukuwe na mambo ya mingi ya kusema mu sala? (Ona maelezo ya chini.)
14 Miaka fulani kisha Samweli kuzaliwa, Hana alimubeba kwa Kuhani Mukubwa Eli. (1 Sa. 1:24-28) Na wakati Hana alikuwa kule, alisali kutoka ku moyo na kumushukuru Yehova juu analinda na kuhangaikia batumishi yake bashikamanifu.c (1 Sa. 2:1, 8, 9) Pengine magumu yenye alikuwa nayo kwake haikuisha, lakini Hana alikazia akili namna Yehova alikuwa amemubariki. Ile inatufundisha nini? Kama tuko na magumu yenye haipendi kuisha, tutaweza kuvumilia kama tunakazia akili namna Yehova alishatubariki na namna iko naendelea kutubariki.
15. Wakati banatutendea bila haki, sala ya nabii Yeremia inaweza kutufundisha nini? (Yeremia 12:1)
15 Soma Yeremia 12:1. Yeremia alihuzunika wakati aliona batu babaya banaonekana kuwa na maisha ya muzuri. Pia alihuzunika kuona vile Baisraeli benzake balimutendea mubaya. (Yer. 20:7, 8) Na siye tunaweza kujisikia vile wakati tunaona batu babaya biko tu naendelea muzuri na maisha yabo, ao wakati tunatendewa mubaya. Ni kweli Yeremia aliambia Yehova kama mambo yenye ilikuwa napitikana ilimukasirisha, lakini hakushakia haki ya Yehova. Wakati aliona vile Yehova alipatia malipizi batu yake benye balikosa kumutii, alikuwa hakika zaidi kama sikuzote Yehova anatendaka tu kwa haki. (Yer. 32:19) Na siye tunaweza kuambia Yehova waziwazi kama jambo fulani inatuhuzunisha, lakini wakati uleule tukuwe hakika kama Yehova atatengeneza mambo kwa wakati wenye kufaa.
16. Kama hali yetu haituruhusu kufanya mambo fulani, sala ya Mulawi inaweza kutufundisha nini? (Zaburi 42:1-4) (Ona pia picha.)
16 Soma Zaburi 42:1-4. Hii wimbo iliandikwa na Mulawi mwenye alikuwa mu uhamisho mwenye hangeweza kukusanyika pamoya na Baisraeli benzake ku hekalu. Maneno yake inaonyesha vile alikuwa najisikia. Na siye tunaweza kujisikia sawa yeye kama hatuwezi kutoka ku nyumba ao tuko mu gereza kwa sababu ya imani yetu. Saa moya tunaweza jisikia muzuri, saa ingine tunajisikia mubaya. Lakini hata tujisikie namna gani, ni muzuri tumuelezee Yehova vile tuko najisikia. Ile itatusaidia tujielewe muzuri na tukumbuke nini njo ya maana zaidi. Kwa mufano, ule Mulawi alitambua kama hali yake ingemupatia nafasi zingine za kumusifu Yehova. (Zb. 42:5) Pia, alifikiria namna Yehova alikuwa namuhangaikia. (Zb. 42:8) Kuambia Yehova mambo yenye iko mu moyo wetu kunaweza kutusaidia tuelewe juu ya nini tuko najisikia vile, tutulie, na tukuwe na nguvu ya kuvumilia.
Mulawi mwenye aliandika Zaburi ya 42 alimufungulia Yehova moyo wake. Wakati tunaambia Yehova vile tuko najisikia ile inatusaidia tuone nini njo ya maana zaidi (Ona fungu ya 16)
17. (a) Sala ya nabii Yona inaweza kutufundisha nini? (Yona 2:1, 2) (b) Namna gani maneno fulani yenye kuwa mu Zaburi inaweza kutusaidia wakati wa magumu? (Ona maelezo ya chini.)
17 Soma Yona 2:1, 2. Nabii Yona alitoa hii sala wakati alikuwa mu tumbo ya samaki. Hata kama Yona hakumutii Yehova, alikuwa hakika kama Yehova atasikiliza sala yake. Mu sala yenye alitoa alitumikisha maneno ya mingi yenye iko mu Zaburi.d Inaonekana alijua maneno yenye ilikuwa mu zile zaburi. Kukumbuka ile maneno na kuifikiria kulimusaidia akuwe hakika kama Yehova atamusaidia. Na siye kama tunajikaza kuweka mu akili maandiko fulani ya Biblia, tutaikumbuka wakati tutakuwa mu magumu na itatufariji wakati tutakuwa nasali kwa Yehova.
ENDELEA KUMUKARIBIA YEHOVA KATIKA SALA
18-19. Waroma 8:26, 27 inatutia moyo namna gani kama tunashindwa kuelezea Yehova vile tuko najisikia? Leta mufano.
18 Soma Waroma 8:26, 27. Wakati fulani tunaweza kuwa na mahangaiko sana mupaka tunashindwa kuelezea Yehova vile tuko najisikia. Lakini ile isituhangaishe sana, juu mu wakati ya vile roho takatifu ya Mungu “inatuombea.” Inafanya vile namna gani? Kupitia roho yake takatifu, Yehova aliandikisha sala za mingi mu Neno yake. Wakati tunashindwa kujieleza, Yehova anaweza kukubali maneno yenye kuwa mu zile sala sawa vile ni maneno yetu yenye tungependa kusema mu sala, na anaweza kuijibia.
19 Kujua ile kulisaidia dada mwenye kuitwa Yelena. Dada Yelena alifungwa kwa sababu ya imani yake. Ile ilimuhangaisha sana mupaka ilikuwa nguvu kwake kusali. Anasema hivi: “Kisha nikakumbuka kama wakati niko na mahangaiko ya mingi na sijue niseme nini mu sala, Yehova ataitika sala za batumishi yake ba zamani zenye ziko mu Biblia . . . sawa vile ni miye njo ninatoa zile sala. . . . Ile ilinitia moyo sana mu ile wakati ya nguvu.”
20. Tunaweza kufanya nini juu ikuwe mwepesi kwetu kusali wakati tuko na mahangaiko?
20 Wakati tuko na mahangaiko inaweza kuwa nguvu kutia akili fasi moya juu ya kusali. Lakini inaweza kuwa mwepesi zaidi kama tunatayarisha akili yetu mbele ya kusali. Tutafanya vile namna gani? Tunaweza kusikiliza usomaji wenye kurekodiwa wa kitabu ya Zaburi. Tunaweza pia kuandika mawazo yetu sawa vile Mufalme Daudi alifanya. (Zb. 18, 34, 142; utangulizi.) Kusema kweli, hakuna sheria juu ya namna tunapaswa kujitayarisha mbele ya kusali. (Zb. 141:2) Kila mutu afanye byenye anaona kama bitamusaidia.
21. Juu ya nini tusali kwa moyo wote?
21 Inatia moyo sana kujua kama Yehova anaelewa vile tuko najisikia mbele hata tuseme kitu. (Zb. 139:4) Lakini anafurahia kusikia namna tunamufungulia moyo wetu na kumuonyesha kama tunamutegemea. Kwa hiyo, usijizuie kusali kwa Baba yako wa mbinguni. Tumikisha maneno yenye iko mu sala zenye ziko mu Biblia. Sali kwa moyo wote. Ambia Yehova mambo yenye inakufurahisha na yenye inakuhangaisha. Na sikuzote, Yehova, Rafiki yako wa kweli atakusikiliza!
WIMBO 45 Mawazo ya Moyo Wangu
a Ona “Sifa fulani za muzuri za Yehova” zenye kuwa mu kitabu Maandiko ya Kutusaidia mu Maisha ya Kikristo chini ya kichwa “Yehova.”
b Kwa kawaida sala zenye zinatolewa mbele ya kutaniko hazipaswe kuwa za murefu.
c Mu sala yenye Hana alitoa alitumikisha maneno yenye inafanana na maneno yenye kuwa mu maandishi ya Musa. Ile inaonyesha kama alikamata wakati wa kufikiri juu ya Maandiko. (Kum. 4:35; 8:18; 32:4, 39; 1 Sa. 2:2, 6, 7) Miaka mingi kisha pale, Maria mama ya Yesu alitumikisha maneno ya kumusifu Yehova yenye inafanana na maneno yenye Hana alitumikisha.—Lu. 1:46-55.
d Kwa mufano, linganisha Yona 2:3-9 na Zaburi 69:1; 16:10; 30:3; 142:2, 3; 143:4, 5; 18:6; na 3:8. Vile hizi zaburi zinafuatana hapa njo vile Yona alifuatanisha mawazo mu sala yake.