Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 10 uku. 24-29
  • Usisahau Kusali Juu ya Bengine

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Usisahau Kusali Juu ya Bengine
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • JUU YA NINI TUSALI JUU YA BENGINE?
  • BIKO NA LAZIMA YA SALA ZETU
  • WAKATI TUNASALI KWA AJILI YA MUTU MUMOYA-MUMOYA
  • UKUWE NA KIASI WAKATI UKO NASALI
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Namna ya Kusali kwa Moyo Wote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 10 uku. 24-29

HABARI YA KUJIFUNZA YA 43

WIMBO 41 Tafazali, Sikia Sala Yangu

Usisahau Kusali Juu ya Bengine

‘Musali kwa ajili ya mutu na mwenzake . . . Sala ya kumulilia Mungu ya mwenye haki iko na nguvu nyingi.’—YAK. 5:16.

WAZO KUBWA

Juu ya nini ni jambo ya maana kusali juu ya bengine na namna tunaweza kufanya vile.

1. Tunajua namna gani kama Yehova anaona sala zetu kuwa za maana?

SALA ni zawadi ya pekee sana. Juu ya nini tunasema vile? Juu Yehova yeye peke tu njo anasikilizaka sala zetu. Yehova ameachia bamalaika makazi fulani lakini hakubapatia ile pendeleo. (Zb. 91:11) Tena amepatia Mwana wake madaraka ya maana lakini hakumupatia ile pendeleo. (Mt. 28:18) Ni Yehova tu njo “Musikiaji wa sala.”—Zb. 65:2.

2. Mutume Paulo alituachia mufano gani kuhusu kusali juu ya bengine?

2 Tuko huru kuzungumuza na Yehova juu ya mambo yetu ya kipekee, lakini hatupaswe kusahau kusali juu ya bengine. Mutume Paulo alikuwa nasali juu ya Bengine. Kwa mufano aliandikia hivi kutaniko ya Baefeso: “Ninaendelea kuwataja katika sala zangu.” (Efe. 1:16) Paulo hakusali tu juu ya kutaniko muzima lakini alisali pia juu ya mutu mumoya-mumoya. Kwa mufano, aliandikia hivi Timoteo: “Ninamushukuru Mungu, . . . siache hata kidogo kukukumbuka katika sala zangu za kumulilia Mungu usiku na muchana.” (2 Ti. 1:3) Paulo alikuwa na mahangaiko yake ya kuambia Yehova. (2 Ko. 11:23; 12:7, 8) Lakini alikumbuka pia kusali juu ya bengine.

3. Juu ya nini tunaweza kusahau kusali juu ya bengine?

3 Wakati fulani tunaweza kusahau kusali juu ya bengine. Juu ya nini? Dada mwenye jina yake Sabrinaa anazungumuzia sababu moya. Anasema hivi: “Tunakuwaka na mambo mingi ya kufanya kila siku. Tunaweza kukazia akili mahangaiko yetu mupaka tunaanza tu kusali juu ya mahitaji yetu.” Ile inakufikiaka na weye? Kama ni vile hii habari itakusaidia. Tutaona (1) juu ya nini ni jambo ya maana kusali juu ya bengine, na (2) namna ya kufanya vile.

JUU YA NINI TUSALI JUU YA BENGINE?

4-5. Namna gani sala zenye tunatoa kwa ajili ya bengine zinaweza kuwa na “nguvu nyingi”? (Yakobo 5:16)

4 Kusali juu ya bengine kuko na “nguvu nyingi.” (Soma Yakobo 5:16.) Sala zenye tunatoa kwa ajili ya bengine zinaweza kusaidia kubadilisha mambo? Ndiyo. Kwa mufano juu Yesu alijua kama mutume Petro alikuwa karibu kumukana, alimuambia hivi: “Nimemulilia Mungu kwa ajili yako ili imani yako isififie.” (Lu. 22:32) Paulo naye alijua kama sala inaweza kusaidia kubadilisha mambo. Njo maana wakati balimufunga Roma bila sababu, aliandikia hivi Filemoni: “Ninatumaini kuwa kupitia sala zenu nitarudishwa kwenu.” (Flm. 22) Na ni vile mambo ilipitikana, Paulo aliachiliwa na akaanza tena kuhubiri.

5 Lakini ile haimaanishe kama wakati tunasali tunaweza kumulazimisha Yehova atende kulingana na byenye tunamuomba. Yehova anaona mambo yenye inahangaisha batumishi yake. Na wakati fulani anaamua kutenda kulingana na mambo yenye banamuomba. Kujua ile kunaweza kutuchochea kusali kwa moyo wote juu ya jambo fulani, na kisha kuacha mambo yote mu mikono ya Yehova.—Zb. 37:5; 2 Ko. 1:11.

6. Kusali juu ya Bengine kuko na matokeo gani juu yetu? (1 Petro 3:8)

6 Kusali juu ya bengine kunaweza kutusaidia tukomalishe sifa ya “huruma yenye upole.” (Soma 1 Petro 3:8.) Kusikilia bengine huruma ni kujua magumu yabo na kuwa tayari kufanya jambo fulani juu ya kubasaidia. (Mk. 1:40, 41) Muzee mwenye jina yake Michael anasema hivi: “Wakati ninasali juu ya bengine, ile inafanya nielewe muzuri magumu yabo na nibapende zaidi. Na ninajisikia kuwa karibu yabo hata kama abo habajue.” Muzee mwenye jina yake Richard anazungumuzia faida ingine. Anasema hivi: “Wakati unasali juu ya mutu utapenda sana kufanya jambo fulani juu ya kumusaidia. Wakati unafanya jambo fulani juu ya kusaidia mutu mwenye ulisali kwa ajili yake ni sawa vile uko nasaidia kujibia sala yenye ulisali juu yake.”

7. Namna gani kusali juu ya bengine kunaweza kutusaidia tusifikirie tu magumu yetu? (Wafilipi 2:3, 4) (Ona pia picha.)

7 Kusali juu ya bengine kunaweza kutusaidia tusione tu magumu yetu. (Soma Wafilipi 2:3, 4.) Juu tunaishi mu dunia yenye inatawaliwa na Shetani Ibilisi, kila mutu iko na magumu yake. (1 Yo. 5:19; Ufu. 12:12) Wakati tunazoea kusali juu ya bengine ile inatusaidia kukumbuka kama “mateso yaleyale yanapata ushirika muzima wa ndugu.” (1 Pe. 5:9) Dada Katherine mwenye ni painia anasema hivi: “Kusali juu ya bengine kunanikumbusha kama nabo biko na magumu. Ile inafanya nisifikirie tu magumu yangu.”

Picha: Bandugu na dada benye biko na magumu yabo biko nasali juu ya bengine. 1. Mutoto mwanamuke anaikala ku kitanda yake na iko nasali; yulu yake kuko picha ya familia yenye iko naacha nyumba yabo juu mayi ya mingi inayala fasi yote. 2. Familia ya mu picha yenye ilitangulia iko nasali pamoya; yulu yabo kuko picha ya ndugu mwenye iko mu gereza. 3. Ndugu mwenye iko mu gereza wa mu picha yenye ilitangulia iko nasali; dada mulemavu mwenye kuzeeka iko ku kitanda ku hopitali. 4. Ule dada wa mu picha yenye kutangulia iko nasali; picha ya mutoto mwanamuke wa picha ya kwanza, anaikala yeye peke wakati benzake biko nafanya fete ya siku ya kuzaliwa.

Kusali juu ya bengine kunatusaidia tusione tu magumu yetu (Ona fungu ya 7)d


BIKO NA LAZIMA YA SALA ZETU

8. Tunaweza kusali kwa ajili ya nani?

8 Tunaweza kusali kwa ajili ya nani? Tunaweza kusali juu ya batu mingi ku limoya. Kwa mufano, tunaweza kusali juu ya bagonjwa, juu ya benye kuzeeka, na juu ya vijana ao batoto benye banafunzi benzabo banachekelea na kubakaza kufanya mambo ya mubaya. Tena Bakristo bamingi biko navumilia upinzani kutoka kwa batu ya familia ao kutoka kwa serikali. (Mt. 10:18, 36; Mdo. 12:5) Bakristo bengine bameacha manyumba yabo juu ya mivurugo mu mambo ya politike, na bengine bamepatwa na misiba ya asili. Pengine hatujuane nabo. Lakini wakati tunasali juu yabo tunaonyesha kama tunafuata hii amri ya Yesu: “Mupendane.”—Yoh. 13:34.

9. Juu ya nini tunapaswa kusali juu ya benye kuongoza mu tengenezo na juu ya babibi yabo?

9 Tunapaswa pia kusali juu ya benye kuongoza mu tengenezo, ni kusema bandugu ya Baraza Yenye Kuongoza na basaidizi yabo, bandugu ba mu Halmashauri za Tawi, bandugu benye kusimamia kazi mbalimbali ku biro ya tawi, baangalizi ya muzunguko, bazee ya kutaniko, na batumishi ya huduma. Bale bandugu biko na magumu yabo, lakini biko natumika sana kwa ajili yetu. (2 Ko. 12:15) Kwa mufano, mwangalizi moya wa muzunguko mwenye jina yake Mark anasema hivi: “Haiko mwepesi kwangu kuwa mbali na bazazi yangu benye balishazeeka na biko na magumu ya afya. Hata kama dada yangu na bwana yake biko nabahangaikia, ninajisikiaka mubaya juu kuko mambo yenye siwezi bafanyia juu siko pale.” Ikuwe tunajua ao hapana magumu ya bale bandugu, ni muzuri tuendelee kusali kwa ajili yabo. (1 Te. 5:12, 13) Tunaweza pia kusali kwa ajili ya babibi yabo juu biko nategemeza babwana yabo ili baendelee kutimiza muzuri migao yabo.

10-11. Yehova anafurahi wakati tunasali kwa ajili ya ndugu na dada zetu kwa ujumla? Fasiria.

10 Sawa vile tumeona, mara mingi tunakuwaka tunasali kwa ajili ya bandugu na dada mbalimbali ku limoya. Kwa mufano, bila kutaya mutu, tunaweza kuomba Yehova asaidie benye biko mu magereza, ao benye balifiwa. Muzee moya wenye kuitwa Donald anasema hivi: “Bandugu na dada ba mingi biko navumilia magumu mbalimbali. Njo maana saa moya tunatoaka sala kwa ajili ya bote kwa ujumla, juu Yehova ategemeze batumishi yake bote benye biko nateseka.”

11 Yehova anafurahiaka sala za vile? Ndiyo. Siye hatujue mahitaji ya kila ndugu ao dada. Kwa hiyo ni muzuri kusali kwa ajili ya bandugu na dada bote kwa ujumla. (Yoh. 17:20; Efe. 6:18) Zile vile zinaonyesha namna ‘tunapenda ushirika muzima wa ndugu.’—1 Pe. 2:17.

WAKATI TUNASALI KWA AJILI YA MUTU MUMOYA-MUMOYA

12. Namna gani kuwa baangalifu kunatusaidia tujue bya kusema wakati tunasali juu ya bengine?

12 Ukuwe muangalifu. Zaidi ya kusali kwa ajili ya ndugu na dada kwa ujumla, tunapaswa pia kusali kwa ajili ya mutu mumoya-mumoya. Kwa mufano, mu kutaniko yenu muko ndugu ao dada mwenye iko na ugonjwa wenye hauponake? Kuko kijana mwenye alishavunjika moyo juu benzake biko namukaza kufanya mambo ya mubaya? Kuko muzazi mwenye iko nakomalisha yeye peke batoto “katika nizamu na maonyo ya Yehova”? (Efe. 6:4) Kama uko muangalifu utaweza kuona ile mambo yote, na ile itafanya ujitie pa nafasi yabo na upende kusali juu yabo.b—Ro. 12:15.

13. Namna gani tunaweza kusali kwa ajili ya bale benye hatujuane nabo?

13 Taya majina ya bengine mu sala. Tunaweza kutaya hata majina ya bale benye hatuyaonanaka nabo. Kwa mufano kuko bandugu na badada yetu benye biko mu gereza mu Krimea, Eritrea, Urusi, na Singapour. Majina yabo inapatikana ku jw.org.c Mwangalizi wa muzunguko mwenye jina yake Brian anasema hivi: “Nimeona kama kuandika jina ya ndugu ao dada mwenye iko mu gereza na kuisema kwa sauti kunanisaidia nimukumbuke na nimutaye mu sala zangu.”

14-15. Nini njo itatusaidia tutaye waziwazi mambo yenye tunapenda kuomba Yehova?

14 Tutaye waziwazi mambo yenye tunapenda kuomba. Michael mwenye tulizungumuzia anasema jambo yenye inamusaidiaka. Anasema hivi: “Wakati niko nasoma ku jw.org habari juu ya bandugu yetu benye biko mu gereza, ninajikazaka kuwazia namna ningejisikia kama ningekuwa mu hali yabo. Ninajua kama ningekuwa mu gereza ningekuwa na mahangaiko juu ya bibi yangu. Ningependa kuwa hakika kama iko napata kila kitu yenye iko nayo lazima. Kujikaza kuwazia vile kunanisaidia nijue byenye ninaweza kuomba Yehova wakati niko nasali kwa ajili ya bandugu benye balishaoa benye biko mu gereza.”—Ebr. 13:3, maelezo ya chini.

15 Wakati tunafikiria maisha ya mu gereza yenye bandugu yetu biko naishi kila siku, tunapata bingine bya kuambia Yehova mu sala saa tuko nasali juu yabo. Kwa mufano tunaweza kusali kama balinzi ya gereza babatendee muzuri, na benye biko na mamlaka babapatie uhuru wa kuabudu. (1 Ti. 2:1, 2) Tunaweza pia kusali kama mufano wabo muzuri utie moyo bandugu na badada ba mu makutaniko yabo, ao kama benye habiko Mashahidi baone mwenendo wabo muzuri na ile ibachochee bakuwe tayari kusikiliza ujumbe wetu. (1 Pe. 2:12) Tunaweza kufanya vile hata wakati tunasali kwa ajili ya ndugu na dada benye biko navumilia magumu ingine. Wakati tuko baangalifu, wakati tunataya majina ya bengine mu sala, na wakati tunataya waziwazi mambo yenye tunapenda kuomba, tunaonyesha kama ‘tunajaa sana katika upendo kwa mutu na mwenzake.’—1 Te. 3:12.

UKUWE NA KIASI WAKATI UKO NASALI

16. Namna gani tunaweza kuwa na kiasi wakati tuko nasali? (Matayo 6:8)

16 Sawa vile tuliona, sala zetu zinaweza kusaidia mambo ibadilike. Lakini tunapaswa kuwa na kiasi. Wakati tuko nasali tujue kama hatuko najulisha Yehova jambo fulani, juu tayari anajua kila kitu. Tena hana lazima ya mashauri yetu juu ajue namna ya kushugulikia hali fulani. Yehova anajua mambo yenye batumishi yake biko nayo lazima mbele hata abo baijue ao mbele hata siye tuijue. (Soma Matayo 6:8.) Kama ni vile, juu ya nini sasa tusali juu ya bengine? Mu hii habari tulishazungumuzia sababu mbalimbali, lakini kuko sababu ingine: Kusali juu ya bengine kunaonyesha kama tunabahangaikia. Upendo unatuchochea kusali juu ya bengine na Yehova anafurahi wakati tunaiga upendo wake.

17-18. Leta mufano wenye unaonyesha kama ni muzuri kusali juu ya baabudu benzetu hata kama hatuone matokeo ya sala zetu?

17 Hata kama tunaona kama sala zetu hazibadilishe mambo, zinaonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu; na Yehova anaona ile. Fikiria hii mufano: Mu familia muko batoto bawili badogo-badogo, mutoto mwanaume na mutoto mwanamuke. Mutoto mwanaume anagonjwa, kisha ule mutoto mwanamuke analilia hivi baba yake: “Papa, saidia kaka apone. Anagonjwa sana!” Tayari baba iko natunzisha mutoto wake. Anamupenda na iko namuhangaikia. Lakini anafurahi kuona vile mutoto wake mwanamuke anahangaikia sana kaka yake na anamuomba amusaidie juu apone.

18 Ni vile Yehova naye anapenda tufanye. Anapenda tuhangaikie bengine na tusali kwa ajili yabo. Wakati tunafanya vile tunaonyesha kama hatujihangaikie tu siye peke. Tunapenda na kuhangaikia bandugu na badada yetu, na Yehova anaona ile. (2 Te. 1:3; Ebr. 6:10) Zaidi ya ile, sawa vile tuliona, sala zetu zinaweza kusaidia hali ya mutu ibadilike. Kwa hiyo basi, tusisahau kusali kwa ajili ya bengine.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Ni mu maana gani sala zetu zinaweza kuwa na “nguvu nyingi”?

  • Juu ya nini tunapaswa kusali kwa ajili ya ndugu na dada zetu kwa ujumla?

  • Tunaweza kufanya nini juu tujue mambo ya kusema wakati tuko nasali kwa ajili ya mutu mumoya-mumoya?

WIMBO 101 Tutumike kwa Umoja

a Majina fulani imebadilishwa.

b Angalia ku jw.org video Takeshi Shimizu: Yehova Ni “Musikiaji wa Sala.”

c Juu ya kujua majina ya baabudu benzetu benye biko mu gereza, ona sehemu “Mashahidi wa Yehova Wenye Kufungwa kwa Sababu ya Imani Yao—Kulingana na Eneo.”

d MAFASIRIO YA PICHA: Bandugu na dada biko na magumu yabo lakini biko nasali juu ya bengine.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine