Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/02 uku. 6
  • Barua Kutoka Kwa Baraza Linaloongoza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Barua Kutoka Kwa Baraza Linaloongoza
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Endelea Kubakia mu Tengenezo ya Yehova
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • ‘Muache Uvumilivu Ukamilishe Kazi Yake’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Namna ya Kuendelea Kuwa na Furaha Wakati wa Majaribu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 3/02 uku. 6

Barua Kutoka Kwa Baraza Linaloongoza

Tunapoanza miaka ya kwanza-kwanza ya karne ya 21, tunafurahi kuwaandikia nyinyi mnaofanyiza “ushirika mzima wa ndugu” ulimwenguni pote, na kuwasifu kwa kazi yenu yenye bidii. (1 Pet. 2:​17) Karibu miaka 2,000 iliyopita, Yesu aliuliza: “Mwana wa binadamu awasilipo, je, kwa kweli ataipata hiyo imani duniani?” (Luka 18:8) Kazi yenu yenye bidii mnamo mwaka wa utumishi uliopita inajibu ndiyo kwa ulizo la Yesu! Wengine kati yenu wamedharauliwa au kudhihakiwa kwa sababu ya imani yenu. Mahali pengi, mnavumilia ijapokuwa vita, misiba, magonjwa, na njaa. (Luka 21:​10, 11) Kwa sababu ya bidii yenu kwa ajili ya kazi za uadilifu, Yesu anaweza bado ‘kukuta imani duniani.’ Hakika, kuna furaha mbinguni kwa sababu ya hilo!

Tunajua kwamba kuvumilia si jambo jepesi. Fikirieni majaribu ya ndugu zetu katika nchi moja ya Asia ya magharibi. Jeuri inayovizia Mashahidi wa Yehova ni jambo la kawaida katika nchi hiyo. Juzijuzi, polisi ilikatiza kusanyiko lenye amani la karibu watu 700. Vizuizi vya barabarani vilifanya wengine 1,300 wasihudhurie. Kikundi cha watu wenye kuvaa vitu vya kuficha uso, wengine kati yao wakiwa polisi, waliingia kwa jeuri mahali pa kusanyiko, wakapiga wengi wa wajumbe, na wakaunguza jengo lililopaswa kutumiwa kwa ajili ya kusanyiko. Kwenye pindi nyinginezo, watu wenye imani za kidini zenye kupindukia walipiga kinyama ndugu zetu wakitumia fimbo zenye kupigiliwa misumari.

Mashambulio kama hayo ni yenye kushtua lakini si ya kushangaza. Mtume Paulo aliongozwa na roho kuandika: “Wote wale wanaotamani kuishi kwa ujitoaji-kimungu katika ushirika na Kristo Yesu watanyanyaswa pia.” (2 Tim. 3:​12) Katika karne ya kwanza, Wakristo walivumilia mateso ya mdomoni na ya kimwili, na wengine hata waliuawa. (Mdo. 5:​40; 12:2; 16:​22-​24; 19:9) Jambo hilohilo lilikuwa kweli katika karne ya 20, na bila shaka itaendelea kuwa hivyo katika karne ya 21. Hata hivyo, Yehova anatuambia: “Kila silaha inayotengenezwa juu yako haitasitawi.” (Isa. 54:​17) Huo ni uhakikisho wa ajabu kama nini! Kwa kweli, sisi ni wenye thamani sana kwa Yehova hivi kwamba alisema kupitia nabii wake Zekaria: “Mwenye kuwagusa ninyi anagusa mboni ya jicho [langu].” (Zek. 2:8) Maadui wa waabudu wa Yehova hawatapata ushindi mwishowe. Ibada safi itashinda!

Kwa mfano, katika nchi iliyotajwa hapo mbele, Mashahidi wa Yehova walifurahia vilele viwili vipya katika hesabu ya wahubiri katika mwaka wa utumishi wa 2001. Ndiyo, ndugu zetu huko wanavumilia ijapokuwa magumu, kama wanavyofanya mahali penginepo. Ulimwenguni pote katika mwaka wa utumishi uliopita, watu 5,066 walibatizwa kila juma ili kuonyesha kwamba wamejiweka wakfu kwa Yehova. Sasa wapya hao wanaazimia, pamoja na wengine wetu, “kusimama [wakiwa] kamili na kwa usadikisho imara katika mapenzi yote ya Mungu.”​—Kol. 4:​12.

Fikiria pia mambo yaliyotukia karibuni huko Ugiriki. Ijapokuwa miaka mingi ya upinzani mkubwa kutoka kwa Kanisa la Othodoksi la Ugiriki, Mashahidi wa Yehova sasa wametambuliwa na serikali kuwa “dini yenye kujulikana.” Kwa kuongezea, hati iliyotoa utambuzi huo inasema kwamba majengo ya Betheli ya Ugiriki ni “mahali patakatifu, palipowekwa wakfu kwa ajili ya ibada ya Mungu.” Tunafurahi pia kuwajulisha kwamba katika mwaka wa utumishi uliopita, mahakama zimetoa maamuzi yenye kufaa yanayokuwa na uvutano juu ya ibada yetu huko Bulgaria, Japani, Kanada, Rumania, Russia, Shirikisho la Amerika, na Ujerumani. Tunamshukuru Yehova kama nini kwa kufanya mlango unaoongoza kwenye utendaji uendelee kuwa wenye kufunguliwa katika nchi hizo!

Tunapofikiria jinsi Yehova anavyotegemeza watu wake katika siku hizi za mwisho, tunaona kwamba yeye ndiye Rafiki bora zaidi tunayeweza kuwa naye. Tunafurahia uhusiano wetu pamoja naye, tukijua kwamba anatupenda, anatufundisha, na anatusahihisha. Ndiyo, tutaendelea kukutana na majaribu ya imani. Lakini imani isiyotikisika katika Yehova itatutegemeza. Yakobo aliandika: “Fikirieni yote kuwa shangwe, ndugu zangu, mkutanapo na majaribu ya namna mbalimbali, kama mjuavyo kwamba ubora huu uliojaribiwa wa imani yenu hutokeza uvumilivu.” (Yak. 1:​2, 3) Kwa kuongezea, uvumilivu wetu unaonyesha kwamba tunampenda Yehova, na hilo linatuletea furaha kubwa! Iweni hakika, ndugu wapendwa, kwamba Yehova atasaidia kila mmoja wetu. Ikiwa tunabaki waaminifu, bila shaka atatusaidia tuingie katika ulimwengu mpya. Anataka tufanikiwe.

Kwa hiyo, tunawasihi nyinyi ndugu na dada, vijana na wazee, mlinde karibuni katika akili zile baraka nzuri ajabu zilizo mbele yetu. Mtazamo wetu na uwe kama ule wa mtume Paulo, aliyeandika: “Nahesabu kwamba mateso ya majira yaliyopo si kitu kwa kulinganisha na utukufu utakaofunuliwa katika sisi.” (Rom. 8:​18) Tegemeeni Yehova mnapopambana na taabu ya aina yoyote. Vumilieni, wala msikubali kukata tamaa. Hamtajuta kamwe kuona mmefanya hivyo. Neno la Mungu linatuhakikishia: “Mwenye haki ataishi kwa imani yake.”​—Hab. 2:4.

Ndugu zenu,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine