Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 170
  • Biblia Inasema Nini Juu ya Kutoa Sehemu ya Kumi?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Biblia Inasema Nini Juu ya Kutoa Sehemu ya Kumi?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu ya Biblia
  • Sehemu ya Kumi—Mu “Agano Jipya”
  • Mashahidi wa Yehova Wanatoaka Sehemu ya Kumi?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 170
Mwanaume fulani iko natia makuta mu bahasha juu aende kuitia mu kisanduku ya michango.

Biblia Inasema Nini Juu ya Kutoa Sehemu ya Kumi?

Jibu ya Biblia

Waisraeli waliombwa watoe sehemu ya kumia ya mapato yao ya kila mwaka juu ya kutegemeza ibada ya kweli. Mungu aliwaambia hivi: “Unapaswa kabisa kutoa sehemu moja ya kumi (1/10) ya kila kitu chenye mbegu yako inazaa katika mashamba mwaka kwa mwaka.”​—Kumbukumbu la Torati 14:22.

Amri ya kutoa sehemu ya kumi ilikuwa kati ya amri zenye Mungu alipatia Waisraeli, zenye kuitwa Sheria ya Musa. Wakristo hawaombwe kufuata Sheria ya Musa. Njo maana haiko lazima walipe sehemu ya kumi. (Wakolosai 2:13, 14) Kila Mukristo anaweza kutoa makuta “kama vile alikusudia katika moyo wake, haiko kwa kutokupenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mutu mwenye anatoa kwa furaha.”​—2 Wakorinto 9:7.

  • Sehemu ya Kumi​—Mu “Agano la Kale”

  • Sehemu ya Kumi​—Mu “Agano Jipya”

Sehemu ya Kumi​—Mu “Agano la Kale”

Sehemu ya kumi inazungumuziwa mara mingi mu sehemu ya Biblia yenye inaitwa Agano la Kale. Inazungumuziwa zaidi sana kisha Mungu kupatia Waisraeli sheria kupitia Musa (Sheria ya Musa). Lakini inazungumuziwa pia mu maandiko fulani mbele Mungu apatie Waisraeli Sheria.

Mbele Sheria ya Musa Itolewe

Mu Biblia, mutu wa kwanza kutoa sehemu ya kumi ni Abramu mwenye anaitwa pia Abrahamu. (Mwanzo 14:18-20; Waebrania 7:4) Inaonekana Abramu alitoaka sehemu ya kumi mara moya tu wakati alipatiaka mufalme mwenye alikuwa pia kuhani wa Salemu zawadi. Mu Biblia, hakuna andiko yenye inaonyesha kama Abrahamu na watoto wake walitoaka tena sehemu ya kumi.

Mutu wa pili mwenye Biblia inasema kama alitoaka sehemu ya kumi ni Yakobo, mujukuu wa Abrahamu. Alitoa naziri kama, ikiwa Mungu anamubariki, angemutolea sehemu ya kumi ya kila kitu yenye angepata. (Mwanzo 28:20-22) Watu fulani wenye elimu wanasema kama, inawezakana Yakobo alitoa ile sehemu ya kumi kwa kutolea Mungu zabihu za wanyama. Hata kama Yakobo alitimiza naziri yake ya kutoa sehemu ya kumi, hakulazimisha familia kufanya vile.

Chini ya Sheria ya Musa

Waisraeli waliombwa watoe sehemu ya kumi juu ya kutegemeza ibada ya Yehova.

  • Sehemu ya kumi ilisaidia makuhani na Walawi wapate mahitaji yao ya lazima kusudi waweze kutumia wakati yao yote mu utumishi wao kwa Yehova, juu hawakukuwa na mashamba ya kulima. (Hesabu 18:20, 21) Walawi wenye hawakukuwa makuhani walikuwa wanapokea sehemu ya kumi yenye watu walikuwa wanatoa, kisha wao pia walikuwa wanatolea makuhani “sehemu moja ya kumi (1/10).”​—Hesabu 18:26-29.

  • Biblia inaonyesha kama kuko ingine sehemu ya kumi yenye watu walikuwa natoa. Ile sehemu ya kumi ilisaidia walawi na pia watu wenye hawakukuwa walawi. (Kumbukumbu la Torati 14:22, 23) Familia za Waisraeli zilikuwa zinaitumia wakati wa sikukuu fulani, na wakati fulani ilitegemeza watu wenye walikuwa maskini.​—Kumbukumbu la Torati 14:28, 29; 26:12.

Namna gani sehemu ya kumi yenye Waisraeli walipaswa kutoa ilikadiriwa? Waisraeli walipaswa kutoa sehemu ya kumi ya mavuno yao ya kila mwaka. (Mambo ya Walawi 27:30) Kama Mwisraeli alipenda, angeweza kuleta makuta pa nafasi ya vitu vyenye alivuna. Lakini ikiwa angefanya vile, alipaswa kuongeza kidogo (20%). (Mambo ya Walawi 27:31) Tena, Waisraeli waliombwa watoe “kila sehemu moja ya kumi (1/10) ya mifugo na kundi.”​—Mambo ya Walawi 27:32.

Waisraeli walikuwa wanachagua kila munyama wa kumi mwenye alitoka mu lupango yao ya wanyama ili akuwe sehemu ya kumi. Sheria ilionyesha kama hawakupaswa kuchunguza ao kubadilisha wanyama wenye walichaguliwa, na tena hawakupaswa kutoa makuta pa nafasi ya wale wanyama. (Mambo ya Walawi 27:32, 33) Lakini wangeweza kutoa makuta kwa ajili ya ile ingine sehemu ya kumi yenye walikuwa wanatoa kwa ajili ya sikukuu za kila mwaka. Ile ilifanya mambo ikuwe mwepesi juu Waisraeli walikuwa nafanya safari ya murefu ili kuenda kuhuzuria zile sikukuu.​—Kumbukumbu la Torati 14:25, 26.

Waisraeli walikuwa natoa sehemu ya kumi mara ngapi? Walikuwa natoa sehemu ya kumi kila mwaka. (Kumbukumbu la Torati 14:22) Lakini hawakukuwa nafanya vile kila mwaka wa saba. Ule mwaka ulikuwa mwaka wa sabato, ao mwaka wa mapumuziko, mwaka wenye Waisraeli hawakukuwa nalima mashamba. (Mambo ya Walawi 25:4, 5) Njo maana hakuna sehemu ya kumi yenye ilikuwa inakusanywa mu kipindi ya mavuno. Ile kipindi ya miaka saba, mwaka wa tatu na wa sita, Waisraeli walikuwa natoa ile sehemu ingine ya kumi juu ya kusaidia Walawi na watu maskini.​—Kumbukumbu la Torati 14:28, 29.

Mutu angepewa malipizi gani kama angekosa kutoa sehemu ya kumi? Sheria ya Musa haikusema kama watu wenye walikosa kutoa sehemu ya kumi walipaswa kupewa malipizi. Waisraeli walipaswa kuitoa juu ya kumupendeza Mungu. Walipaswa kuambia Mungu kama wametoa sehemu ya kumi na kumuomba awabariki juu walifanya vile. (Kumbukumbu la Torati 26:12-15) Mungu aliona kama kukosa kutoa sehemu ya kumi ilikuwa sawa vile kumuiba.​—Malaki 3:8, 9.

Kutoa sehemu ya kumi ilikuwa muzigo? Hapana. Mungu aliahidi Waisraeli kama ikiwa wangetoa sehemu ya kumi, angewamwangia baraka zake na hawangekosa kitu. (Malaki 3:10) Lakini waliteseka wakati hawakutoa sehemu ya kumi, pia Mungu aliacha kuwabariki. Na makuhani na Walawi wenye walikuwa nawasaidia kumuabudu Yehova, waliacha kuwasaidia juu nao walipaswa kuenda kujitafutia.​—Nehemia 13:10; Malaki 3:7.

Sehemu ya Kumi—Mu “Agano Jipya”

Wakati Yesu alikuwa ku dunia, watumishi wa Mungu walikuwa wangali wanaombwa kutoa sehemu ya kumi. Lakini kisha Yesu kufa, hawakulazimika tena kufanya vile.

Wakati ya Yesu

Mu sehemu ya Biblia yenye inaitwa Agano Jipya, Biblia inaonyesha kama Waisraeli waliendelea kutoa sehemu ya kumi wakati Yesu alikuwa ku dunia. Hakuna siku Yesu aliwakataza kufanya vile. Hata vile, alilaumu viongozi wa dini wenye walikazia sana kutoa sehemu ya kumi lakini walikuwa ‘wamepuuza mambo mazito zaidi ya Sheria, ni kusema, haki, rehema, na uaminifu.’​—Matayo 23:23.

Kisha kifo ya Yesu

Kisha Yesu kufa, watu hawakulazimika tena kutoa sehemu ya kumi. Kifo ya Yesu ilikuwa mwisho wa Sheria ya Musa, ni kusema ilikuwa pia mwisho wa “amri ya kukusanya sehemu moja za kumi (1/10).”​—Waebrania 7:5, 18; Waefeso 2:13-15; Wakolosai 2:13, 14.

Sehemu ya kumi mu “Kanisa ya Kwanza-kwanza”

“Mu kanisa ya kwanza-kwanza, desturi ya kutoa sehemu ya kumi juu ya kutegemeza mambo ya dini, ilikuwa ya kujipendea. Ni kisha Mukutano wa Matembezi wenye ulifanywa mu mwaka wa 567, njo Kanisa ililazimisha watu kukuwa natoa sehemu ya kumi.”​—Cyclopedia of Biblical, Theological, and, Ecclesiastical Literature, by McClintock and Strong, Volume X, ukurasa wa 436.

a “Sehemu ya kumi ya mapato inatiwaka pembeni juu ya matumizi fulani. . . . Mu Biblia, mara mingi sehemu ya kumi inatumiwaka mu mambo ya dini.”​—Harper’s Bible Dictionary, ukurasa wa 765.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine