MUENDELEE KUKESHA!
Juu ya Nini Mambo ya Politike Inatenganisha Sana Watu?—Biblia Inasema Nini?
Mambo ya politike inatenganisha watu mu dunia yote. Kulingana na uchunguzi wa Pew Research Center wenye ulifanywa mu 2022, “65% ya watu wakubwa wenye kuwa mu inchi 19 tofauti wanasema kama kuko kutokuelewana sana mu inchi yao kati ya watu wenye kutegemeza vyama vya politike tofauti.”
Fasi kwenye unaishi, ulishajionea namna mambo ya politike inatenganisha watu? Juu ya nini mambo iko vile? Kuko siku ile itaishaka? Ona mambo yenye Biblia inasema.
Tabia zenye zinatenganisha watu
Biblia ilisemaka kama mu siku zetu, ni kusema, “siku za mwisho,” watu wengi watakuwa na tabia zenye zitawatenganisha.
“Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, . . . wenye hawataki makubaliano yoyote.”—2 Timoteo 3:1-3.
Hata kama watu wengi wanajikaza sana kutegemeza serikali, mambo iko tu mubaya. Haiwezekane kwa watu wenye kuwa na mawazo tofauti kuungana mukono ili kumaliza mambo ya mubaya. Ile inatimiza mambo yenye Biblia ilisemaka tangu zamani.
“Mwanadamu ametawala mwanadamu mwenzake ili kumuumiza.”—Muhubiri 8:9.
Lakini, Biblia inaonyesha kama serikali yenye kuongozwa na mutu mwenye kuwa na uwezo wa kumaliza magumu yenye iko natesa watu leo njo yenye itamalizaka mambo ya mubaya.
Kiongozi mwenye kustahili na mwenye kuhangaikia watu
Biblia inasema kama Yesu Kristo tu njo kiongozi mwenye kustahili. Iko na nguvu, mamlaka, na anapenda kufanya watu wote waishi kwa umoja na amani.
“Katika siku zake mwenye haki atasitawi, na amani itakuwa nyingi.”—Zaburi 72:7.
“Wafalme wote watainama mbele yake.”—Zaburi 72:11.
Yesu ni kiongozi muzuri juu anahangaikia watu na anapenda kuwasaidia, zaidi sana wale wenye wametendewa bila haki.
“Kwa maana ataokoa maskini mwenye kulilia musaada, pia mutu wa hali ya chini na mutu yeyote mwenye hana musaidizi. Atamusikilia huruma mutu wa hali ya chini na maskini, na ataokoa uzima wa maskini. Atawaokoa katika ukandamizaji na katika jeuri.”—Zaburi 72:12-14.
Ujifunze mambo mingi zaidi kuhusu Ufalme wa Mungu, ni kusema, serikali ya mbinguni yenye Yesu njo kiongozi. Ona mambo yenye unaweza kufanya juu ile serikali ikuletee faida na namna unaweza kuitegemeza.
Angalia video Ufalme wa Mungu Ni Nini?
Soma habari “Ufalme wa Mungu—Serikali Yenye Haina Rushwa”