panitan/stock.adobe.com
Yesu Atamaliza Umaskini
Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alionyesha kama anapenda watu sana na alihangaikia sana maskini na wagonjwa. (Matayo 9:36) Yesu alitoa hata uzima wake juu ya wengine. (Matayo 20:28; Yohana 15:13) Hivi karibuni, Yesu ataonyesha tena kama anapenda watu sana, atatumia mamlaka yake akiwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu juu ya kumaliza umaskini mu dunia yote.
Ona vile Biblia inaonyesha mambo yenye Yesu atafanya:
“Acha atetee watu wa hali ya chini katika taifa, acha aokoe wana wa maskini.”—Zb. 72:4.
Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye Yesu alishatufanyia na mambo yenye atatufanyia? Njia moya ya kuonyesha shukrani ni kujifunza mambo mingi zaidi juu ya “habari njema ya Ufalme wa Mungu;” ile habari njo Yesu alikuwa anahubiri. (Luka 4:43) Soma habari “Ufalme wa Mungu Ni Nini?”