Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mrt habari 121
  • Ni Nani Unaweza Kutumainia?—Biblia Inasema Nini?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni Nani Unaweza Kutumainia?—Biblia Inasema Nini?
  • Habari Zingine
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ule mwenye unaweza kutumainia
  • Watu Hawaaminie Tena Watu wa Politike​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zingine
  • Yesu Atamaliza Umaskini
    Habari Zingine
  • Tutumainie Ndugu na Dada Zetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Yesu Atamaliza Vita
    Habari Zingine
Ona Habari Zaidi
Habari Zingine
mrt habari 121
Picha: Watu wenye mara mingi wanaonwa kuwa wenye kutumainika: 1. Mutu wa politike anasimama mbele ya mikro. 2. Padri anafunga mikono. 3. Mwanasayansi anakamata kitu ya kuandikia.

Kushoto: Olena Yefremkina/stock.adobe.com; katikati: lunamarina/stock.adobe.com; kuume: Rido/stock.adobe.com

MUENDELEE KUKESHA!

Ni Nani Unaweza Kutumainia?​—Biblia Inasema Nini?

Watu wanavunjika moyo wakati wale wenye wanaonwa kuwa wenye kutumainika hawawahangaikie. Watu wengi hawatumainie tena . . .

  • wakubwa wa politike wenye wanahangaikia kwanza faida zao kuliko kuhangaikia mambo yenye watu wako nayo lazima.

  • vyombo vya habari vyenye havitoe habari zenye kutumainika na za kweli.

  • wanasayansi wenye kusudi yao haiko kusaidia watu.

  • viongozi wa dini wenye wanategemeza viongozi wa politike kuliko kusaidia watu wamutumikie Mungu.

Watu wako na sheria ya kuona kama haiko kila mutu njo wa kutumainia. Biblia inatupatia hii angalisho:

  •  “ Musitumainie wakubwa wala mwana wa binadamu, mwenye hawezi kuleta wokovu.”​—Zaburi 146:3.

Ule mwenye unaweza kutumainia

 Biblia inatuonyesha ule mwenye tunaweza kutumainia: Yesu Kristo. Yesu haiko tu mwanaume muzuri mwenye aliishi ku dunia kumepita miaka mingi. Mungu alimuweka Yesu kuwa “Mufalme . . . , na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (Luka 1:32, 33) Yesu ni Mufalme wa Ufalme wa Mungu, ni kusema guvernema yenye iko natawala sasa mbinguni.​—Matayo 6:10.

  • Juu ujue juu ya nini unaweza kumutumainia Yesu, soma habari “Ni Nani Mufalme wa Ufalme wa Mungu?” na “Ufalme wa Mungu Utafanya Nini?”

Kitabu yenye unaweza kutumainia

Mu Biblia muko habari za mingi juu ya maisha ya Yesu na juu ya mambo ingine ya mingi ya maana. Mu hii kitabu ya pekee muko habari za kweli zenye unaweza kutumainia. Juu ujionee ile weye peke, tunakutia moyo ulomba funzo ya Biblia bila kulipa. Wakati utalomba ile funzo, watakupatia pia vichapo vyenye utakuwa navyo lazima na mutu mwenye utajifunza naye kwa njia ya mazungumuzo. Utajifunza mambo mingi, kati ya ile mambo utajifunza Yesu ni mutu wa namna gani, utajifunza juu ya mambo yenye alishafanya, yenye iko nafanya, na yenye atafanya mu siku zenye ziko nakuya.

Jaribu Programu Yetu ya Kujifunza Biblia

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine