Siku ya Kwanza, 1 Mwezi wa 9
Mwangaza wa asubui utatufikia kutoka juu.—Lu. 1:78.
Mungu amepatia Yesu nguvu ya kumaliza magumu yote ya wanadamu. Miujiza yenye Yesu alifanya ilionyesha kama iko na nguvu ya kumaliza magumu yenye hatuwezi kumaliza siye wenyewe. Kwa mufano, iko na nguvu ya kutosha jambo yenye imefanya wanadamu wakuwe mu magumu, ni kusema, zambi yenye waliriti na pia matokeo yake, yenye ni magonjwa na kifo. (Mt. 9:1-6; Ro. 5:12, 18, 19) Kupitia miujiza yake, alionyesha kama iko na nguvu ya kuponyesha “kila namna ya” magonjwa na kama iko na nguvu ya kufufua wafu. (Mt. 4:23; Yoh. 11:43, 44) Tena, iko na nguvu ya kutuliza zoruba yenye upepo mukali na kufukuza pepo wachafu. (Mk. 4:37-39; Lu. 8:2) Inatia moyo kabisa kuona kama Yehova amepatia Mwana wake nguvu ya kufanya ile mambo yote! Tuko hakika kabisa kama ahadi zote za mambo ya muzuri yenye Ufalme wa Mungu utaleta, zitatimia. Miujiza yenye Yesu alifanya wakati alikuwa mwanadamu hapa ku dunia, inatufundisha kama wakati ataanza kutawala dunia, atatufanyia mambo mingi sana ya muzuri. w23.04 3 fu. 5-7
Siku ya Pili, 2 Mwezi wa 9
Roho inachunguza ndani ya mambo yote, hata mambo mazito ya Mungu.—1 Ko. 2:10.
Kama uko mu kutaniko ya munene na ile inafanyaka kiongozi asikutaye, unaweza kuvunjika moyo. Lakini, usiache kutoa maelezo. Tayarisha maelezo mingi ku kila mukutano. Na kama haupate nafasi ya kutoa maelezo ku mwanzo wa funzo, utakuwa na nafasi ingine ya kutoa maelezo wakati mukutano uko naendelea. Wakati uko natayarisha Funzo ya Munara wa Mulinzi fikiria namna kila fungu inapatana na kichwa ya ile habari. Kama unafanya vile, pengine utapata maelezo ya muzuri yenye unaweza kutoa. Zaidi ya ile, unaweza kutayarisha maelezo yenye kuwa mu mafungu yenye kuzungumuzia mafundisho mazito yenye iko nguvu kufasiria. Juu ya nini? Juu kutakuwa watu kidogo wenye watapenda kutoa maelezo mu ile sehemu. Sasa utafanya nini kama kisha mikutano mingi haupewe tu nafasi ya kutoa maelezo? Mbele mukutano uanze, umuambie kiongozi kama unapenda kuleta jibu ya ulizo fulani. w23.04 21-22 fu. 9-10
Siku ya Tatu, 3 Mwezi wa 9
Yosefu . . . alifanya kama vile malaika wa Yehova alimuambia, akamuchukua bibi yake na kuenda naye kwake.—Mt. 1:24.
Yosefu alikuwa tayari kutumikisha muongozo wa Yehova, na ile njo ilifanya akuwe bwana muzuri zaidi. Zaidi ya mara tatu, Mungu alimupatia maagizo kuhusu familia yake. Kila mara alitii palepale hata kama ilikuwa nguvu. (Mt. 1:20; 2:13-15, 19-21) Juu Yosefu alitii muongozo wa Mungu, alimulinda Maria, alimutegemeza na kumuhangaikia. Fikiria namna mambo yenye Yosefu alifanya ilimusaidia Maria amupende na amuheshimie hata zaidi! Bwana, unaweza kuiga Yosefu kwa kutafuta mashauri yenye inategemea Biblia yenye inaonyesha namna unaweza kuhangaikia familia yenu. Kama unatumikisha ile mashauri hata kama ni nguvu, utaonyesha kuwa unamupenda bibi yako na utafanya ndoa yenu ikuwe muzuri zaidi. Dada wa Vanuatu, mwenye alishafanya zaidi ya miaka 20 mu ndoa, anasema hivi: “Wakati bwana yangu anatafuta muongozo wa Yehova na kuutumikisha, ile inafanyaka nimuheshimie zaidi. Najisikiaka kuwa salama na natumainiaka maamuzi yake.” w23.05 21 fu. 5